Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,743
- 9,875
Asikwambie mtu, biashara ni ngumu sana, isitoshe pesa hakuna. Vyuma vimekaza ilihali mama yangu anamiliki "garage" iliyosheheni makopo kibao ya grisi
Nina shahada tatu nilizozisotea kwa muda mrefu sana. Mbali na kujibana bana kwenye matumizi ya boom langu ambalo nilihitaji kumega nusu ya pesa hiyo ili kujazilizia ada, mama hakutaka hata kugeuza shingo yake kunitazama mimi mwanae.
Niliutegemea msaada kutoka kwa baba, lakini ndo basi tena. Nikamwambia mama kama ikimpendeza anipatie nafasi ya ulinzi kwenye gereji yake, wajomba zangu wakadakia na kumshauri mama eti nijiajiri, nitafute kwa jasho langu
Inauma asikwambie mtu. Ni mara mia ningeishia kidato cha nne. Ningekuwa mbali kimaisha
Karibuni sana ndugu zangu hapa Karatu mnichangie nyanya. Fungu 500, moja mia
Ushauri: Mama, badili mfumo wa elimu nchini. Wafundishe wanetu stadi za maisha na namna ya 'kuhandle' biashara. Waandaeni na maisha ya kutokutegemea ajira. Elimu ya kidato cha nne mkiimodify inatosha. Sasa hayo ma integration, barometer, african resistance, circular motion e.t.c yatanisaidia nini kwenye matenga ya nyanya hapa Karatu?
Nina shahada tatu nilizozisotea kwa muda mrefu sana. Mbali na kujibana bana kwenye matumizi ya boom langu ambalo nilihitaji kumega nusu ya pesa hiyo ili kujazilizia ada, mama hakutaka hata kugeuza shingo yake kunitazama mimi mwanae.
Niliutegemea msaada kutoka kwa baba, lakini ndo basi tena. Nikamwambia mama kama ikimpendeza anipatie nafasi ya ulinzi kwenye gereji yake, wajomba zangu wakadakia na kumshauri mama eti nijiajiri, nitafute kwa jasho langu
Inauma asikwambie mtu. Ni mara mia ningeishia kidato cha nne. Ningekuwa mbali kimaisha
Karibuni sana ndugu zangu hapa Karatu mnichangie nyanya. Fungu 500, moja mia
Ushauri: Mama, badili mfumo wa elimu nchini. Wafundishe wanetu stadi za maisha na namna ya 'kuhandle' biashara. Waandaeni na maisha ya kutokutegemea ajira. Elimu ya kidato cha nne mkiimodify inatosha. Sasa hayo ma integration, barometer, african resistance, circular motion e.t.c yatanisaidia nini kwenye matenga ya nyanya hapa Karatu?