Katika kuelekea kilele cha miaka 50 ya Uhuru, hebu tujiulize chama kikuu cha upinzani nchini Chadema kimefanya nini cha msingi kwa taifa la Tanzania ukiondoa maandamono ambayo yameshindwa kuleta ukombozi wa kweli kama maandamano yaliyofanyika Egypt na Tunisia. Viongozi wa Chadema katika miaka 50 ya Uhuru wamefanya nini cha Maendeleo kwa Taifa letu cha kukumbukwa na Watanganyika ? nini leo Chadema wanaweza kuwaeleza Wananchi wamefanya katika miaka 50 ya Uhuru? Kama wamefanikiwa kuwa chachu ya maendeleo tunawapongeza sana lakini kama hawajafanya kitu cha Maendeleo wanapaswa kulaumiwa na Watanganyika.