Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Kila Mtu Ana Haki Ya Kusimamia Anachoamini Ni Kweli,hata Kama Wewe Unaona Si Kweli.namjua Mh Serukamba,ni Kijana Anaesema Kweli Na Haogopi Kusimamia Ukweli Anaohamini,ni Mpiganaji Hasiechoka,ndio Maana Alimwangusha Kaburu Kigoma....unajua Zamani Inasekana Kuna Mwanafalsafa Mmoja Alidai Kuwa Dunia Ni Duara Na Sio Bapa,alibishana Na Watu Wote Mpaka Wakamuua.lakini Leo Historia Imeona Nani Ni Kweli,leo Hii Mnaweza Kuona Serukamba Hayuko Sawa Lakini Ni Kwa Mtazamo Wa Masafa Mafupi,historia Itamuona Tofauti Na Hayo Mnayowaza.
Nchimbi,
Mtu kweli ana haki ya kusimamia anachoamini. Hata Charles Taylor, Mugabe, Amin, Hitler, Musolini nk na wao walisimamia wanachokiamini. Ila binadamu wa kawaida hawezi kuwafuga watu kama hawa maana baadaye kuja kuwatoa inakuwa kazi sana. Ndiyo maana USA walipoona Savimbi kawa na Al-Qaid wakamuuwa palepale.
Juu ya Mwana-Falsafa unayesema ni Mikolaj Kopernik (Nicolaus Copernicus) aliyekuwa akiishi Torun, mji mmoja Poland ambaye kitabu chake ni jana tu kimeuzwa mnadani kama sikosei UK kwa zaidi ya dola milioni mbili. Huyu bwana alisema kuwa dunia ni duara. Ila ukweli ni kuwa dunia SI DUARA ila ni ELPSI (Umbo la yai). Hivyo hata yeye alirekebishwa kidogo. Sasa huyu kijana wako ambaye unamwona yuko sawa na msimamo wake, mwangalie vizuri. Hapa kuna watu kibao na wenye muono wa mbali. Inawezekana wakawa wote wrong. Ila uwezekano huo ni mdogo sana. Kuna watu walijua kuwa Hitler ni TISHIO ila tayari ilikuwa too laite. Kama huyu kijana ni KIRAFI namna hiyo basi naogopa CIA wakimuona tu basi ujuwe atakuwa wao. Watampanda huyo kichwani hadi awe wao na baadaye kuwa RAIS (Mabutu design). Kwa hili nawapenda Ma-Jews. Wangelimfuata kijana kama huyu na kumficha sehemu.