Wana JF,
Taarifa za uhakika ambazo nimezipata hivi sasa kutoka chanzo cha uhakika zinasema Mhariri wa Rai Masyaga Matinyi amekamatwa kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh. M 1.8, Matinyi amekutwa na kashfa hiyo wilayani Monduli akiwa na wenzake wawili.
Chanzo hicho kinasema, rushwa hiyo waliiomba kutoka kwa mfanyakazi wa TANESCO Monduli ambaye hana sifa za kuwa na nafasi ya kikazi aliyonayo hivyo, walimuomna fedha hizo ili wasiandike habari hiyo na kama angegoma kutoa basi stori hiyo ingeandikwa.
Hata hivyo mfanyakazi huyo aliomba apunguziwe na atangulize Sh. 200,000 kumbe tayari alikuwa ameshaweka mtengo na PCCB ambao walifanikiwa kuwanasa wote wakiwa ndani ya ofisi ya mfanyakazi huyo.
Kwa sasa Matinyi na wenzake Samson Mwita (32), Bora Yunus Bidiga wanashikiliwa TAKUKURU ARUSHA kwa mahojiano zaidi.
Nawasilisha wadau
Taarifa za uhakika ambazo nimezipata hivi sasa kutoka chanzo cha uhakika zinasema Mhariri wa Rai Masyaga Matinyi amekamatwa kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh. M 1.8, Matinyi amekutwa na kashfa hiyo wilayani Monduli akiwa na wenzake wawili.
Chanzo hicho kinasema, rushwa hiyo waliiomba kutoka kwa mfanyakazi wa TANESCO Monduli ambaye hana sifa za kuwa na nafasi ya kikazi aliyonayo hivyo, walimuomna fedha hizo ili wasiandike habari hiyo na kama angegoma kutoa basi stori hiyo ingeandikwa.
Hata hivyo mfanyakazi huyo aliomba apunguziwe na atangulize Sh. 200,000 kumbe tayari alikuwa ameshaweka mtengo na PCCB ambao walifanikiwa kuwanasa wote wakiwa ndani ya ofisi ya mfanyakazi huyo.
Kwa sasa Matinyi na wenzake Samson Mwita (32), Bora Yunus Bidiga wanashikiliwa TAKUKURU ARUSHA kwa mahojiano zaidi.
Nawasilisha wadau