Mhariri Mtendaji wa Gazeti la MwanaHALISI, Saed Kubenea avamiwa na kumwagiwa tindikali akiwa ofisini kwake

Kubenea amekwishafika Delhi na ameshaanza matibabu.
 
Kubenea kaenda kutalii hakuna cha accid wala nini,mbona mwenzie haijamzuru?eti kwa kuwa alikuwa amevaa miwani,unaweza ukacharangwa mapanga vile alafu bado mawani yakabaki na kuzuiaacid isiingie.Nimeongea na dk Kinabo anasema kama ile ni acid basi itakuwa ni ndogo sana kwa kiwango ambacho ni sawa na acid ambayo inaweza kuwa imetengenezwa kwa majani ya chai..ata hivyo akasisitiza kuwa hakuona umuhimu wa kumpeleka india labda kutembea.
 
Kubenea kaenda kutalii hakuna cha accid wala nini,mbona mwenzie haijamzuru?eti kwa kuwa alikuwa amevaa miwani,unaweza ukacharangwa mapanga vile alafu bado mawani yakabaki na kuzuiaacid isiingie.Nimeongea na dk Kinabo anasema kama ile ni acid basi itakuwa ni ndogo sana kwa kiwango ambacho ni sawa na acid ambayo inaweza kuwa imetengenezwa kwa majani ya chai..ata hivyo akasisitiza kuwa hakuona umuhimu wa kumpeleka india labda kutembea.

Fisadi Mtoto, acha utani kwenye mambo ya msingi...kaenda kutalii !!! hainingii akilini hii, umeona alivyochalangwa mapanga Mzee Dimara? ama unataka kutuambia wewe unahusika ...umejua hata kiwango cha acid ile? JF imeingiliwa haswaaa....Fisadi Mtoto huoni haka muungwana alieenda mpa pole pale Muhimbili wewe hapa unaleta ngojera zisizo na kichwa wala miguu...eti nimeongea na Dr Kinabo....kaaa kimya Fisadi Mtoto........labda India kutembea.....kazi kweli kweli...
 
Kubenea kaenda kutalii hakuna cha accid wala nini,mbona mwenzie haijamzuru?eti kwa kuwa alikuwa amevaa miwani,unaweza ukacharangwa mapanga vile alafu bado mawani yakabaki na kuzuiaacid isiingie.Nimeongea na dk Kinabo anasema kama ile ni acid basi itakuwa ni ndogo sana kwa kiwango ambacho ni sawa na acid ambayo inaweza kuwa imetengenezwa kwa majani ya chai..ata hivyo akasisitiza kuwa hakuona umuhimu wa kumpeleka india labda kutembea.


His name says it all

Mungu ibariki Tanzania
 
Mpaka sasa najiuliza sababu za ki-taratibu na ki-sera za kiserikali za kumtibu huyu mhariri!!! sijazipata, kwa kuwa ni rais wengi wakitanzania wanakumbana na matatizo kama haya na serikali haihusiki na lolote?

Sasa wasije wakatufikisha mahali tukaamini walihusika?
 
Kubenea kaenda kutalii hakuna cha accid wala nini,mbona mwenzie haijamzuru?eti kwa kuwa alikuwa amevaa miwani,unaweza ukacharangwa mapanga vile alafu bado mawani yakabaki na kuzuiaacid isiingie.Nimeongea na dk Kinabo anasema kama ile ni acid basi itakuwa ni ndogo sana kwa kiwango ambacho ni sawa na acid ambayo inaweza kuwa imetengenezwa kwa majani ya chai..ata hivyo akasisitiza kuwa hakuona umuhimu wa kumpeleka india labda kutembea.

kweli we fisadi... mtu anapasuliwa jicho, wewe unasema mtalii? unajua nani kalipia? hata kama ni utalii, sisi waandishi wa habari na wamiliki tuliohakikisha anaenda India, tuko radhi hata kama ni kutalii, maana kazi ni kubwa na bora akatalii yeye kuliko hao wanaotalii kwenda kula Mbuzi Monduli na mafisadi wa BoT
 
Serikali Haijatoa Hata Senti Tano, Labda Kama Watatoa Sasa Lakini Hazihitajiki
 
ES
Mawazo yako hayana tofauti na baadhi ya watu wanaopenda kupata majibu ya haraka bila kutumia muda kutafakari.

Jana nilisikitika nilipoanagalia Taarifa ya Habari na leo niliposoma Tamko La BAVICHA,Mzee Mengi,Makunga,Sakina Datoo hawa nao niliona ni kwa kiwango gani walivokua wavivu wakufikiri pale walipo toa hukumu kabisa kua Kuvamiwa kwa kubenea kuna Uhusiano wa moja kwa moja na UANDISHI wake,hawa watu ktk matamko yao walitoa hukumu kabisa kua kubenea amehujumiwa,kama ilivo kwa JOHN MNYIKA ( ingiwa najua tatizo lake ni uanaharakati,na tabia yao nikutafuta majibu rahisi)kudai kua

Nakubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa kuwa badala ya kunyosha kidole moja kwa moja kuwa fulani anahusika kama alivyofanya Haji Duni juzi ni kutokuwa mwajibikaji.


vijana waliofanya tukio wametumiwa na mafisadi so wasitumike, bila kukumbuka kua mmoja alie kamatwa ana miaka 65 sijui kama ni kijana.

Umezungumza kama mtu mwenye mamlaka ya kujua unachosema. Na nikisoma vizuri unasema hakukuwa na MZEE aliyefanya kitu hicho. Na hutumii maneno ya "madai" ya vijana.. ila unasema vijana waliofanya hivyo na unashangazwa kwanini Bw. Mushi wa Kinondoni atajwe miongoni mwa vijana hao! mmmh...

RIOBA ktk waongeaji alikua more objective na hakutaka kuhukumu ingawa Prof wangu Shivji nae jana kidogo nilijiuliza is it uzee unamuanza au ni bcs nae ameaminishwa kua kubenea amehujumiwa na mafisadi, Mengi yeye simshangai ni mzee wa kuchukua oppprtunities na always hua ni mtu wa kukurupuka.

KUna kitu ambacho hukukisema alichosema Mengi ambacho ni kuwa kushambulia waandishi wa habari ni sawa na kushambulia kioo kwa vile tu kinakuonesha jinsi ulivyo mchafu! Hiyo ndiyo ilikuwa message yake. Na kuhusu being opportunist kweli unaweza kulinganisha na CCM.. kisa na mkasa wa serikali kuingilia kati na kumgharimia Kubenea ni nini? Ina maana leo hii kila Mtanzania anayepatwa na janga na anataka kwenda India au kwingine kwa matibabu serikali itaingilia kati..?


JANA NILIULIZA MASWALI HAPA JF KUA KAMA KWELI KUBENEA AMEKUA ANAKUMBANA NA VITISHO (JE ALISHINDWA KUWEKA ANGALAU MLINZI WA KIMASAI KTK OFISI YAKE? PIA WHY WATU WANAKIMBILIA KUDAI KUA AMEHUJUMIWA BCS YA UANDISHI WAKE NA TUSIJIULIZE MASWALI MADOGO MAY BE KADHULUMU,KACHUKUA MKE WA MTU,AU WALIOVAMIA NI VIBAKA,OR NI MATEJA BCS HATA SILAHA ZAO NI MAARUFU MIONGONI MWA MATEJA,etc)

Katika Tanzania jukumu la kulinda raia na mali zao haliko kwa wamasai ama wamakonde. Wenye haki na jukumu hilo kisheria ni Polisi. Hivyo swali lako lina makosa ndani yake. Ungeuliza "Hivi Kubenea alishindwa kutoa taarifa Polisi za vitisho hivi kwa muda huu wote na Polisi wakashindwa kumpatia ulinzi wa uhakika au kumshauri hatua za kuchukua?" Ungeuliza swali hilo jibu lake lingekutisha.. but your are too smart for that.. you had to ask the "wrong" question to imply a correct answer!


Watanzania wengi wanataka kuaminishwa kwamba tukio hilo ni hujuma kwa vigezo kua amekua akipata sms za vitisho,or ametaka kugongwa naGARI makusudi,hivi kwa siku ni wangapi wanapoteza maisha kwa kugongwa na magari either kwa uzembe wa DEREVA au wa mtumiaji wa njia mwenyewe,why tusijiulize kubenea inawezekana alikua amelewa akashindwa kufata sheria za barabarani or dereva aliemkosa alikua amelewa mzembe.

Ajali ambazo zinamfuata mtu mmoja na simu za vitisho zinazomfuata mtu mmoja na hatimaye kushambuliwa mtu huyo huyo huwezi kuweka kwenye kundi la "vitu vya kawaida". Ni wangapo ya "wanaopoteza maisha yao kwenye ajali ya gari" wanakutana na yafuatayo:

- Simu za vitisho
- Message za vitisho
- Gari kuungua katika mazingira ya kutatanisha
- Kuvamiwa na watu ambao hawataki kitu chochote zaidi ya kudhuru mwili
- Kumwagiwa tindikali?

Nioneshe mtu mwingine mmoja mwenye mkosi wa namna hiyo. Hata hivyo hoja yako ina jambo jingine la kutisha. Unataka fikra za watu zielekezwe "nje" ya uwezekano wa tukio hilo kuhusishwa na kazi yake? Kwa nini? Kwanini usiwe kama mimi na kuweka options zote wazi without excluding anything na kuacha Polisi wafanye kazi zao. Kwanini hutaki watu watoe fikra zao na kuzihusisha na sababu yoyote ile..? Unless of course.. YOU know why....

Nachoomba kuptia Forum hii WAANDISHI walifanye tukio hili kama matukio mengine mpaka pale uthibitisho utakapo kua kweli ni hujuma.

Nina habari mbaya kwako. Kwa bahati mbaya haiwezekani kulifanya tukio hili kuwa "kama matukio mengine"... naomba unisaidie tukio hili linafanana na tukio jipi jingine?.. ambalo halikuwa kutangazwa au liliwahi kutangazwa. Tukio jingine naweza kukufananisha nalo ni lile la waandishi kupigwa kule Ukonga (kina Bukuku) na serikali kulihalalisha kwa kusema ilikuwa sawa (alikuwa O. Mapuri aliyetoa baraka hizo). Ni tukio hilo ulikuwa unaliwazia uliposema "matukio mengine"?


Ni hatari kwa jamii kuwapa nafasi watu kama SAKINA DATOO wa SUNDAY CITIZEN bcs mara nyingi amekua ni mtu ambae ni opportunist wanao fanya nae kazi wanlijua hilo anapotoa kauli zake mara nyingi hana Facts,na anakua ni mtu wa kuongozwa na HISIA zaidi,MAKUNGA jana alionyesha kitu cha ajabu kua waandishi wanafanya uchunguzi kabla ya kuandika (theme ya maongezi yake) lakini nilishangaa je kabla ya kuongea alikua amefanya uchunguzi wa kiwango GANI? MAMA TAMWA sijashangaa ni NATURE ya kazi yake wana harakati mara nyingi ni watu hatari sana bcs to them kilakitu ni opportunity kama alivo wahi kusema PROF WANGU MAREHEMU CHACHAGE (TO TRUST ACTIVIST IS NOT SAFE AS TO TRUST REVOLUTIONIST)

Huwezi kuwaambia watu wasiwe na hisia kwa sababu hisia zao hazikubaliani na hisia za kwako. Hata hivyo point yako hapa ni kubwa. Ndio maana nimepiga sana kelele kuhusu Raila kwa sababu maneno huchochea hisia zaidi na hupofusha mtazamo wa ukweli. Baadhi ya yaliyosemwa na baadhi ya waandishi kama Mwitumba jana yalikuwa yanapakana na uzushi! Nilisikitika kuona waandishi wanampigia makofi Mwitumba kwa kudai wale wote walioandikwa kwenye magazeti wajitokeze kukanusha kwamba hawakuhusika kana kwamba kwa kufanya hivyo kutawafanya HAWAKUHUSIKA! Good point.

Wana JF inawezekana ni kweli kahujumiwa,nani hatujui thats why TIBA anafanya uchunguzi tusubiri matokeo tujaribu kuangalia jambo la kubenea kwa mapana zaidi isije tukaifanya FANI YETU YA HABARI NI CHAKA LA MAOVU kila mwandishi akiguswa basi tu conclude hujuma bcs ni mwandishi ifike mahali tuliangalie jambo kwa UHALISIA WAKE kuliko HISIA.

Kwa mara nyingine tena unaandika kama mtu anayejua kilichotokea (hasa kutokana na makala yako wiki kadhaa kuhusu Kubenea hapa JF). Kufikiri kuwa Tibaigana anafanya uchunguzi ni vituko vya karne! Unataka nikupatie jibu watakalolipata? Watawakamata watu kama walivyofanya na watu hao watakiri kuhusika na tukio hilo na sababu watasema walitaka kuiba vitu na uporaji ukatoka kombo na watasema hawakuwa na mpango wowote wa mambo ya uandishi wa Kubenea. Hivyo uchunguzi umeonesha ni tukio la kijambazi tu na hakuna ushahidi kuwa lilimlenga Kubenea kama mwandishi!



KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI


ndiyo! KIGUMU!
 
Bravo Mwanakijiji na Halisi,
Mie mwenyewe CCM ila siwezi kutetea jambo la kinyama kama hili.Mzee Es busara yako umepeleka wapi?au ndio umetumwa na hao wauaji?
Je Fisadi mtoto umetumwa kuja kujisajiri hapa ili utetee maada hii,Au unadhani hatujui nyie ndio mnahusika na wizi wa pesa ya EPA ya BOT?
Kesho habari itauza sana katika Mwanahalisi.
Asante halisi kwa kutupa feedback
 
]...duh jk opportunistic kweli...alafu anaposema kuwa ""waandishi mnapoandika habari za watu mchukue tahadhari kwa kuwa kuna watu hawataki habari zao ziandikwe" hapo ana maana gani? kama amiri jeshi mkuu anasema hivyo tukimbilie wapi??....
Huyu JK apimwe akili jamani,mtu mwenye akili timamu achilia mbali mkuu wa nchi na Amiri jeshi mkuu hawezi kutamka maneno kama hayo kwenye media

Mambo mengine inabidi tupige dua kumuombea huyu jamaa apate uelewa hata wa kuona mita 50
 
Tangu jamaa kamwagiwa tingikali ambayo naamini ilikuwa too much neutralized, ndio maana haijamchubua hata ngozi, watu wamukuwa wakiolaani sana hapa but mimi naamini amepewa zawadi yake ya mwaka mpya na wale aliowachafua
Karibu Fisadi Mtoto,naona umekuja na jina lingine.Karibu sana
 
Mwanakijiji
Kula sahani moja na Mtot wa mkulima. Huyu anaonekana ana nafasi fulani CCM. Haburuzwi mtu hapa.
 
Ushirombo Hawa Wakina Fisdi Mtoto Ndio Wanotumia Fedha Za Walipa Kodi Uko India Kwa Majina Ya Wazazi Wao::::atupe Hints Zote Na Hicho Kiasi Cha Acid Anachosema
 
""waandishi mnapoandika habari za watu mchukue tahadhari kwa kuwa kuna watu hawataki habari zao ziandikwe" hapo ana maana gani? kama amiri jeshi mkuu anasema hivyo tukimbilie wapi??...".

ndio raisi wetu tutafanyaje na jamaa nasikia mudsa si mrefu alikuwa aje na list ya wauza unga aliopewa jakaya na uongozi wa polisi,kazi kwelikweli
 
Kitila,
We are slowly legalizing if not legitimizing ufisadi.
Kimekuwa kama cheo vile cha kujisifu nacho.
 
we unafanya mchezo wenzenu siku hizi wakitajwa kuwa ni mafisadi wanafikiria wanapata promotion ya aina fulani.. ni katika harakati za kudesensitize watu ili mtu akiitwa fisadi basi anacheka tu..! Inakuwa ni kama mtu anapomwita rafiki yake "huyu mshenzi sana..!" kwa maana ya ujanja na uchakaramu..
 
Back
Top Bottom