Mh. Rais tengua uteuzi wa Msajili wa Hazina kwa sababu hizi

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
Wana- jamvi,

Kutokana na kulegalega kwa hali ya vyama vya mikopo kama vile Vicoba, Saccos na hali ya mabenki, hali ya fedha katika jumuiya mbalimbali au vikundi vilivyojiunga kupata fedha kutoka taasisi hizo kuwa mbaya,
hali hii inamgusa moja kwa moja kwani yeye ndio Msajili wa Hazina ndio Msajili wa hizo taasisi na msimamizi mkuu wa kuendesha fedha katika maeneo h
ayo.

Hali ya fedha katika taasisi hiyo ni mbaya, wakopaji wanakosa mikopo vilevile Vicoba au Saccos kukosa fedha za kukopesha wanavikundi, kwa maana hiyo Msajili ameshindwa kusimamia taasisi hizo hasa katika kutoa mgao wa fedha kwenda kwenye taasisi na vikundi hivyo.

Kama kweli Mh. Rais unampango wa kuwaneemesha wananchi kupitia vikundi na taasisi hizo basi tengua uteuzi wa Msajili wa hazina na utafute atakae kuwa mbunifu ili hali ya uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja ili nzuri.
 
Nakushaurii siku nyingine kabla ya kupost ufanye utafiti kujua majukumu ya Msajili wa Hazina

Wewe ndio hujui baadhi ya majukumu na kazi za Msajili wa hazina toa tafsiri hata tano ya majukumu yake sio kujifanya unajua hapa
 
Huyu jamaa achana nae ana fanya kazi yake kwa weledi mkubwa, mkuu kila mnapojitahidi kumshusha jamaa Mungu ndio anazidi kumpaisha ya nini kujitia umaskini kwa dhambi za kijinga zisizo na benefit kwako? Bora ukaibe au ukavunje amri ya sita utakuwa umeenjoy dhambi, kuliko kupika Jungu unajiumiza nafsi burreeee.
 

Hii ndiyo jamii forum ukumbi wa great thinkers.Mtu anaandika jambo asilolijua hata chembe,moderators wanaipitisha kama
ilivyo,akipelekwa mahakamani mtalia serikali ya kidikteta.
SACCOS zinasajiliwa na kusimamiwa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika.Vikishindwa kukopesha wanachama wao ni kwa uzembe wao wa kutosimamia marejesho ya fedha walizokopesha au kushindwa kujenga mtaji wao wenyewe.SACCOS vina hadhi ya kisheria ya kushtaki na kushtakiwa.Vinaweza kukopa na kukopesha mahitaji yao yanapokuwa makubwa kuliko uwezo wao. SACCOS ni lazima zikaguliwe kila mwaka,zina Mkaguzi anayetambuliwa kisheria.Kuna hatua za kuchukua zisipokaguliwa.
Msajili wa hazina hana uwezo wa kisheria kugusa chochote cha SACCOS.Zinaoongozwa na Sheria ya Ushirika Na.6 ya mwaka 2013.

VICOBA havina hadhi ya kisheria ya kushtaki wala kushtakiwa.Vinaweza kusajiliwa BRELA,Mambo ya ndani au katika ngazi ya halmashauri ya eneo husika.VICOBA ni sawa na SACAS siyo SACCOS,vina hadhi sawa na kikundi chochote cha kijamii.Havikaguliwi na yeyote,na ukuvikopesha ni kwa matakwa ya wewe unayevikopesha huwezi kuvibana kwa sheria yeyote.VICOBA havina jukumu la kupeleka taaifa zake kwa yeyote.Hakuna sheria yeyote inayotaka vikaguliwe na kuelekeza visipokaguliwa hatua zipi zichukuliwe.

Mtoa mada aeleze nini jukumu la Msajili wa hazina kwenye maeneo aliyoyataja,na kwa nini asichukuliwe hatua kwa upotoshaji? Au ndiyo tunarudi enzi za utotoni ukiniacha unaniogopa ukinipiga unanionea.
 
Wana- jamvi,

Kutokana na kulegalega kwa hali ya vyama vya mikopo kama vile Vicoba, Saccos na hali ya mabenki, hali ya fedha katika jumuiya mbalimbali au vikundi vilivyojiunga kupata fedha kutoka taasisi hizo kuwa mbaya,
hali hii inamgusa moja kwa moja kwani yeye ndio Msajili wa Hazina ndio Msajili wa hizo taasisi na msimamizi mkuu wa kuendesha fedha katika maeneo h
ayo.

Hali ya fedha katika taasisi hiyo ni mbaya, wakopaji wanakosa mikopo vilevile Vicoba au Saccos kukosa fedha za kukopesha wanavikundi, kwa maana hiyo Msajili ameshindwa kusimamia taasisi hizo hasa katika kutoa mgao wa fedha kwenda kwenye taasisi na vikundi hivyo.

Kama kweli Mh. Rais unampango wa kuwaneemesha wananchi kupitia vikundi na taasisi hizo basi tengua uteuzi wa Msajili wa hazina na utafute atakae kuwa mbunifu ili hali ya uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja ili nzuri.
Unaongelea Msajili wa Hazina au Mrajisi wa vyama vya Ushirika,? Bangi kitu kibaya sana hasa ukiwa hujala.
 
Wana- jamvi,

Kutokana na kulegalega kwa hali ya vyama vya mikopo kama vile Vicoba, Saccos na hali ya mabenki, hali ya fedha katika jumuiya mbalimbali au vikundi vilivyojiunga kupata fedha kutoka taasisi hizo kuwa mbaya,
hali hii inamgusa moja kwa moja kwani yeye ndio Msajili wa Hazina ndio Msajili wa hizo taasisi na msimamizi mkuu wa kuendesha fedha katika maeneo h
ayo.

Hali ya fedha katika taasisi hiyo ni mbaya, wakopaji wanakosa mikopo vilevile Vicoba au Saccos kukosa fedha za kukopesha wanavikundi, kwa maana hiyo Msajili ameshindwa kusimamia taasisi hizo hasa katika kutoa mgao wa fedha kwenda kwenye taasisi na vikundi hivyo.

Kama kweli Mh. Rais unampango wa kuwaneemesha wananchi kupitia vikundi na taasisi hizo basi tengua uteuzi wa Msajili wa hazina na utafute atakae kuwa mbunifu ili hali ya uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja ili nzuri.
Mzee hawa wake zetu wanachangishana pesa huku mitaani na kukopeshana wana uhusiano gani na utendaji wa msajili wa hazina? VICOBA na SACCOS wanakopesha pesa bila kufanya tathmini ya ndani ya uwezo wa mkopaji kulipa sasa hapo msajili wa hazina anahusikaje?

Tuwaelimishe wake zetu wakusanyie akiba zao kwa kufungua akaunti benki badala ya vikundi na vikoba kwani wajanja wamekuwa wengi huko mitaani
 
Unajua wale mabig wa ofc za mabenk wanamchukia Jamaa sana naona kwa lile wazo LA serikali kuondoa pesa zake kwenye mabenk
 
Usikute mleta mada ni kati ya watu waliomfanyia majungu huyu msajili pindi akiwa mkuu wa NBC. Huyu jamaa kila akifanyiwa majungu nyota yake inazidi kupanda tu.

Ndio hawa hawa itakua mambo yamewabana huko wanajua kabisa akiwapisha huyu wataendelea kufanya mauozo yaoo
 
Ndio huyo amefanya hakuna mzunguuko kisa pesa kurundikana hazina sio sifa, sifa ni pesa kuzunguuka wangeweka control mechanism ya kudhibiti kilichotokea kati taasisi za umma na mabenki ona mdororo wa uchumi mpaka Tanzania inatia huruma daahh poleni huko aisee
 
Mmaaaaa!!!!! Mbona unaita ujinga mada yangu ungepita tuu bila kuchangia mkuu haikua na ulazima wa kuchangia
Ni sharti chepe liitwe chepe na sio kijiko kikubwa. Sasa wewe unakuja kumpaka matope TR eti kwasababu vicoba na mabenki yanayumba? Kana kwamba TR ana mamlaka juu yao? Halafu ulitaka ujibiwe na mapambio? Siku nyingine kabla ya kuleta mada hebu fanya research kidogo. Kwa sasa nakushauri ukatafute functions za TR ndio utajua kwanini nimeita mada kwamba ni ujinga

Sent from my SM-G7102 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom