Mh. Dewji iokoe Mwenge sekondari Singida!

babayah67

JF-Expert Member
Mar 28, 2008
493
79
Wiki mbili zilizopita nilikuwa Singida Mjini kikazi, nikiwa miongoni mwa Wanafunzi waliosoma Singida kati yaa mwaka 1980 hadi 1984 (Form I - IV) nilikuwa na hamu ya kuitembelea shule yangu, ili kuangalia mandhari yake na pia kuwasalimia walimu wangu kama wangekuwa bado wapo.

Baada ya kumaliza shughuli zangu za siku, jioni moja nilitembea kuelekea Mwenge Sekondari. Nilianza kupatwa na mshtuko mara tu nilipofika pale kwenye mawe mawili ya barabarani karibu na guest ilokuwa ikijulikana kama Victoria, au Mmassy Bakery (alokuwa akisupply mikate na matunda shuleni). Shock yenyewe ni kuwa shule siku hizi haina tena uzio uliokuwa ukizunguuka shule na kupunguza vibaka. Pamoja na hilo, siku hizi hakuna ulinzi wowote magetini, yaani geti A lili linaloingilia ofisini na madarasani, au Geti B, lile linaloingilia nyumba za walimu.

Nilijisikia kutoa machozi nilipotembelea mabwenini. Ukiingia bweni la Jamhuri, Azimio na Kujitegemea hali inatisha sana. Vitanda vibovu, kuta chafu hazijapakwa rangi nafikiri sijui toka sisi tunamaliza shule. Kwa ujumla hali ni mbaya saana. Sehemu tulizokuwa tunafulia na kuogea, siku hizi hazitumiki kabisa, maji hayatoki basi ni taabu tupu.

Nikatembelea bwalo la chakula, ambalo wakati wetu lilikuwa na meza karibu 90 na kila meza ikiwa na mabenchi mawili, sasa hivi niliona meza moja tu. Nilipowauliza wanafunzi wanakaa wapi wakati wa kula walisema wanakula wakiwa wamesimama tu. Kwa ujumla jamani hali ni mbaya saana.

Kwa wanafunzi wanaosoma pale, sitarajii matokeo yao kuwa mazuri.

NB: Namwomba Mbunge wa Singida Mjini MH. AZIM DEWJI aitazame kwa jicho la huruma shule hiyo. Ninaamini anaweza japo kuwapakia rangi ndani ya Mabweni yao vijana wale. Na kuwarekebishia japo Taa za kusomea Madarasani na bwenini.
 
Mkuu pole kwa huzuni iliyokukuta.
Hali hiyo hiyo hutukuta sisi wengine tuliopita hapo.
Siungi mkono ushauri wako wa kumtaka MO aisaidie hiyo shule...
Hiyo ni shule ya SERIKALI KUU na serikali ina wajibu kuikarabati.
MO kama ana ubavu aibane serikali ndani na nje ya bunge itimize wajibu wake huo.
Pesa ambayo angetumia kuisaidia shule akaitishe mikutano na wana CCM awalishe pilau,soda na maji kama alivyozoea.
Akiamua kuisaidia shule afanye kama raia mwenye mapenzi mema...atambue hayo si moja ya majukumu ya mbunge.
 
Serikali imeshindwa, wananchi chukueni hatua wenyewe.

Wasake wote waliosoma hapo, mfanye maarifa ya kutoa usaidizi endelevu shuleni hapo

Haba na haba hujaza kibaba
 
Mkuu pole kwa huzuni iliyokukuta.
Hali hiyo hiyo hutukuta sisi wengine tuliopita hapo.
Siungi mkono ushauri wako wa kumtaka MO aisaidie hiyo shule...
Hiyo ni shule ya SERIKALI KUU na serikali ina wajibu kuikarabati.
MO kama ana ubavu aibane serikali ndani na nje ya bunge itimize wajibu wake huo.
Pesa ambayo angetumia kuisaidia shule akaitishe mikutano na wana CCM awalishe pilau,soda na maji kama alivyozoea.
Akiamua kuisaidia shule afanye kama raia mwenye mapenzi mema...atambue hayo si moja ya majukumu ya mbunge.
Huyo MO yupo kwenye hiyo nafasi kwa maslahi yake mkuu. Ufisadi na ujambazi wooote unaofanywa hapa Tanzania sasa ulishawahi kusikia hata anafanya usanii wa kukemea? Hata kama akipaka rangi asipokemea ujambazi unaoendeshwa na viongozi wa serikali ya sasa ni kama mgonjwa wa maleria kutumia asprin.... hatapona. Wabunge wa aina hii ni kiama cha walalahoi tu.
 
dah tuko wengi lakini hatujuani yaan hiyo sio shule tena hata matamasha ya mziki huwa yanafanyika hapo.mwenge ilikuwa zamani sasa hivi imebaki jina tu kama ccm
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom