BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
Date::10/7/2008
Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa
Na Jackson Odoyo
Mwananchi
UMOJA wa Vyuo Vikuu nchini (Tahiliso) umepanga kufanya mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini utakaofanyika Oktoba 27 mwaka huu serikali itakapo kubali kubadili sera ya elimu nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Katibu Mkuu wa umoja huo, Mtatiro Julius alisema katika mgomo wanafunzi hawataingia darasani mpaka hapo serikali itakapo kubali mapendekezo yao.
Alisema lengo la mgomo huo ni kuishinikiza serikali ibadili sera zote zinachangia kudidimiza maendeleo ya elimu nchini ili usawa wa elimu uwepo kati ya mtoto aliyezaliwa katika familia isiyokuwa na kipato kizuri na familia yenye kipato kizuri.
Aliongeza kuwa moja ya mambo watakayo yapinga katika sera hiyo ni kitendo cha wanafunzi kufukuzwa chuoni kufukuzwa wasimafanye mitihani ama kunyimwa matokeo yao baada kufanya mitihani.
''Sera inayosimamia maendelea ya elimu nchini inachangia kudidimiza elimu ya nchi na hasa kwenye suala la ada ya wanafunzi ambalo husababisha wanafunzi kufukuzwa chuo kwa kushindwa kulipa ada,'' alisema Mtatiro.
Alifafanua kuwa kitendo cha serikali kumpunguzia ama kumfutia ada mwanafunzi aliyetoka katika familia isiyokuwa na uwezo wakati akisoma elimu ya chini lakini anapingia elimu ya juu alipie sawa na wale wenye uwezo haileti uwiano wa elimu nchini.
Aliongeza kuwa hali hiyo ndiyo inayosababisha wanafunzi wa vyuo vikuu kufukuzwa chuo kila wakati, kama ilivyotokea katika Chuo Kikuu cha Ardhi mwaka huu.
''Kitendo cha serikali kuwafukuza wanafunzi 227 wa chuo hicho ni kuongeza migogoro vyuoni, makazini na hata kuongeza utitiri wa vyeti bandia maofisini,'' alalamika Mtatiro.
Hata hivyo, alisema serikali inashindwa kuwajali wasomi watakaoisaidia nchi baadaye na badala yake inawakumbatia wawekezaji wasiokuwa na uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.
Alifafanua kitendo cha serikali kushindwa kuwatetea wasomi wanaotoka katika familia maskini bila kujali kwamba wao pia ni sehemu ya jamii ya watanzania nikuwanyima haki yao ya msingi.
Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa
Na Jackson Odoyo
Mwananchi
UMOJA wa Vyuo Vikuu nchini (Tahiliso) umepanga kufanya mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini utakaofanyika Oktoba 27 mwaka huu serikali itakapo kubali kubadili sera ya elimu nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Katibu Mkuu wa umoja huo, Mtatiro Julius alisema katika mgomo wanafunzi hawataingia darasani mpaka hapo serikali itakapo kubali mapendekezo yao.
Alisema lengo la mgomo huo ni kuishinikiza serikali ibadili sera zote zinachangia kudidimiza maendeleo ya elimu nchini ili usawa wa elimu uwepo kati ya mtoto aliyezaliwa katika familia isiyokuwa na kipato kizuri na familia yenye kipato kizuri.
Aliongeza kuwa moja ya mambo watakayo yapinga katika sera hiyo ni kitendo cha wanafunzi kufukuzwa chuoni kufukuzwa wasimafanye mitihani ama kunyimwa matokeo yao baada kufanya mitihani.
''Sera inayosimamia maendelea ya elimu nchini inachangia kudidimiza elimu ya nchi na hasa kwenye suala la ada ya wanafunzi ambalo husababisha wanafunzi kufukuzwa chuo kwa kushindwa kulipa ada,'' alisema Mtatiro.
Alifafanua kuwa kitendo cha serikali kumpunguzia ama kumfutia ada mwanafunzi aliyetoka katika familia isiyokuwa na uwezo wakati akisoma elimu ya chini lakini anapingia elimu ya juu alipie sawa na wale wenye uwezo haileti uwiano wa elimu nchini.
Aliongeza kuwa hali hiyo ndiyo inayosababisha wanafunzi wa vyuo vikuu kufukuzwa chuo kila wakati, kama ilivyotokea katika Chuo Kikuu cha Ardhi mwaka huu.
''Kitendo cha serikali kuwafukuza wanafunzi 227 wa chuo hicho ni kuongeza migogoro vyuoni, makazini na hata kuongeza utitiri wa vyeti bandia maofisini,'' alalamika Mtatiro.
Hata hivyo, alisema serikali inashindwa kuwajali wasomi watakaoisaidia nchi baadaye na badala yake inawakumbatia wawekezaji wasiokuwa na uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.
Alifafanua kitendo cha serikali kushindwa kuwatetea wasomi wanaotoka katika familia maskini bila kujali kwamba wao pia ni sehemu ya jamii ya watanzania nikuwanyima haki yao ya msingi.