Mgomo wa madaktari wa kigeni wanukia...

Chal

Senior Member
Oct 7, 2010
128
52
wakuu!
kuna tetesi zimezagaa mtaani na humu jamvini kuwa serikali ina mpango wa kuleta madaktari kutoka nje ya nchi, hasa nchi ya Irani ikitajwa zaidi. Hawa ni madaktari wa kigeni ambao kama mpango huo utafanikiwa watakuja nchini ili kunusuru sekta ya afya.

kwa maoni yangu ujio wa madaktari hawa (kama ni kweli wataletwa) utapelekea mgomo mwingine mkubwa zaidi katika sekta ya afya kuwahi kutokea. Mgomo huu ambao sasa utaratibiwa na kutekelezwa na madaktari wa kigeni utakuwa kwa sababu zifuatazo.

Kwanza, madaktari wa kigeni watagoma kutokana na kuwako kwa vifaa duni vya kutolea tiba katika hospitali za umma hapa nchini ikiwamo hosp ya taifa muhimbili. Hili ni miongoni mwa mambo ambayo madaktari wazalendo wamekuwa wakilililia kila mara.

Madaktari wa kigeni watagoma wakihitaji viletwe vifaa vya kisasa katika hosp watakazopelekwa ili kuendana na ujuzi na taaluma zao jambo litakalowawezesha kutoa tiba stahiki kwa wagonjwa.

Suala la mishahara na posho za madaktari wapya (wa kigeni) litazua mjadala mzito zaidi kwani malipo kwa madaktari hao ni mara tatu zaidi ya yale ya madaktari wazalendo. Serikali itashindwa kuwalipa madaktari hawa kwani kwa maelezo yake ni kuwa haina fedha na kulingana na huko inapotarajiwa kuwaleta (Irani) kuna uwezekano wakajitoa muhanga pale muhimbili na kwingineko.

Madaktari wa kigeni pia watagoma ili serikali ipeleke vitanda kwa ajili ya wagonjwa mahospitalini ili wagonjwa wasilale chini ama wawili wawili wodini hii ikiwa sambamba na kuhakikisha kuwa zipo dawa na vifaa tiba vya kutosha mahospitalini ili waweze kutoa huduma kwa wagonjwa.

Hivyo basi suala la kuleta madaktari wa kigeni linaweza lisiwe suluhisho la mgomo wa madaktari iwapo mazingira ya kufanyia kazi na maslahi kwa madaktari hayataboreshwa! Serikali iliwahi kukiri kupitia waziri mkuu kuwa madai ya madaktari ni ya msingi nashauri msingi huo pia uzingatiwe katika majadiliano ili kufikiwe muafaka

Serikali isitafute njia ya mkato kulishughulikia hili....
kwani tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliahirisha au kulikimbia...
 
Kingine lugha, hao madaktari wa iran isije kuwa kama wachina na wajapan wanatumia lugha zao sasa wakija hapa kiarabu tutaweza? Watalala wapi, watafikaje hospitali ili hali ni wageni kabisa. Hata kama hawatalipwa lakini bado utata upo.
 
Kingine lugha, hao madaktari wa iran isije kuwa kama wachina na wajapan wanatumia lugha zao sasa wakija hapa kiarabu tutaweza? Watalala wapi, watafikaje hospitali ili hali ni wageni kabisa. Hata kama hawatalipwa lakini bado utata upo.

hapo kwenye lugha umenena kabisa, itabidi wagome wapelekwe swahili course ya mwaka mmoja ndiyo waje watoe huduma
 
wakuu!
kuna tetesi zimezagaa mtaani na humu jamvini kuwa serikali ina mpango wa kuleta madaktari kutoka nje ya nchi, hasa nchi ya Irani ikitajwa zaidi. Hawa ni madaktari wa kigeni ambao kama mpango huo utafanikiwa watakuja nchini ili kunusuru sekta ya afya.

kwa maoni yangu ujio wa madaktari hawa (kama ni kweli wataletwa) utapelekea mgomo mwingine mkubwa zaidi katika sekta ya afya kuwahi kutokea. Mgomo huu ambao sasa utaratibiwa na kutekelezwa na madaktari wa kigeni utakuwa kwa sababu zifuatazo.

Kwanza, madaktari wa kigeni watagoma kutokana na kuwako kwa vifaa duni vya kutolea tiba katika hospitali za umma hapa nchini ikiwamo hosp ya taifa muhimbili. Hili ni miongoni mwa mambo ambayo madaktari wazalendo wamekuwa wakilililia kila mara.

Madaktari wa kigeni watagoma wakihitaji viletwe vifaa vya kisasa katika hosp watakazopelekwa ili kuendana na ujuzi na taaluma zao jambo litakalowawezesha kutoa tiba stahiki kwa wagonjwa.

Suala la mishahara na posho za madaktari wapya (wa kigeni) litazua mjadala mzito zaidi kwani malipo kwa madaktari hao ni mara tatu zaidi ya yale ya madaktari wazalendo. Serikali itashindwa kuwalipa madaktari hawa kwani kwa maelezo yake ni kuwa haina fedha na kulingana na huko inapotarajiwa kuwaleta (Irani) kuna uwezekano wakajitoa muhanga pale muhimbili na kwingineko.

Madaktari wa kigeni pia watagoma ili serikali ipeleke vitanda kwa ajili ya wagonjwa mahospitalini ili wagonjwa wasilale chini ama wawili wawili wodini hii ikiwa sambamba na kuhakikisha kuwa zipo dawa na vifaa tiba vya kutosha mahospitalini ili waweze kutoa huduma kwa wagonjwa.

Hivyo basi suala la kuleta madaktari wa kigeni linaweza lisiwe suluhisho la mgomo wa madaktari iwapo mazingira ya kufanyia kazi na maslahi kwa madaktari hayataboreshwa! Serikali iliwahi kukiri kupitia waziri mkuu kuwa madai ya madaktari ni ya msingi nashauri msingi huo pia uzingatiwe katika majadiliano ili kufikiwe muafaka

Serikali isitafute njia ya mkato kulishughulikia hili....
kwani tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliahirisha au kulikimbia...
Kuna faida gani ya kuwepo kwa madaktari wazawa wasiomthamini mgonjwa na wanaogoma kila baada ya mawiki kadhaa?
 
wakuu!
kuna tetesi zimezagaa mtaani na humu jamvini kuwa serikali ina mpango wa kuleta madaktari kutoka nje ya nchi, hasa nchi ya Irani ikitajwa zaidi. Hawa ni madaktari wa kigeni ambao kama mpango huo utafanikiwa watakuja nchini ili kunusuru sekta ya afya.

kwa maoni yangu ujio wa madaktari hawa (kama ni kweli wataletwa) utapelekea mgomo mwingine mkubwa zaidi katika sekta ya afya kuwahi kutokea. Mgomo huu ambao sasa utaratibiwa na kutekelezwa na madaktari wa kigeni utakuwa kwa sababu zifuatazo.

Kwanza, madaktari wa kigeni watagoma kutokana na kuwako kwa vifaa duni vya kutolea tiba katika hospitali za umma hapa nchini ikiwamo hosp ya taifa muhimbili. Hili ni miongoni mwa mambo ambayo madaktari wazalendo wamekuwa wakilililia kila mara.

Madaktari wa kigeni watagoma wakihitaji viletwe vifaa vya kisasa katika hosp watakazopelekwa ili kuendana na ujuzi na taaluma zao jambo litakalowawezesha kutoa tiba stahiki kwa wagonjwa.

Suala la mishahara na posho za madaktari wapya (wa kigeni) litazua mjadala mzito zaidi kwani malipo kwa madaktari hao ni mara tatu zaidi ya yale ya madaktari wazalendo. Serikali itashindwa kuwalipa madaktari hawa kwani kwa maelezo yake ni kuwa haina fedha na kulingana na huko inapotarajiwa kuwaleta (Irani) kuna uwezekano wakajitoa muhanga pale muhimbili na kwingineko.

Madaktari wa kigeni pia watagoma ili serikali ipeleke vitanda kwa ajili ya wagonjwa mahospitalini ili wagonjwa wasilale chini ama wawili wawili wodini hii ikiwa sambamba na kuhakikisha kuwa zipo dawa na vifaa tiba vya kutosha mahospitalini ili waweze kutoa huduma kwa wagonjwa.

Hivyo basi suala la kuleta madaktari wa kigeni linaweza lisiwe suluhisho la mgomo wa madaktari iwapo mazingira ya kufanyia kazi na maslahi kwa madaktari hayataboreshwa! Serikali iliwahi kukiri kupitia waziri mkuu kuwa madai ya madaktari ni ya msingi nashauri msingi huo pia uzingatiwe katika majadiliano ili kufikiwe muafaka

Serikali isitafute njia ya mkato kulishughulikia hili....
kwani tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliahirisha au kulikimbia...

Umefanya nimecheka sana hapo kwenye blue, wenzetu huwa hawatanii bado kazi ipo!
 
Serikali legelege, rais daifu

Na migomo itaendelea kuwepo as long as the root problem haiondolewi bali kufunikwa. Kila huo mzizi unapokuwa mkubwa lazima mgomo( halafu mnafukia tena), yaani tutaenda hivyo mpaka ifikie kipindi muone solution si kuufukia bali kuung'oa.


Chezea Mungu ya Ulimboka weye!
 
Serikali itaabika!

ng'wanakidiku mkuu,
kwanza hao magaidi wairan wakija mimi nitaishangaa sana sirkali yetu. wairan mfumo wao wa elimu toka vidudu hadi chuo kikuu ni kwa lugha yao ya taifa iitwayo Farsi au twaweza kuihta kiajemi. in that case ht hao madoc wao watakao kuja watakuwa wanaongea lugha hiyo. itabidi sirkali sikivu iajiri wakalimani kwa kila doc as per idadi ya madoc watakaokuja.

swali ni kwamba, watz wangapi wanajua lugha yd kiajemi ili waajiliwe km translators? hata km wangekuwapo gharama ya kuwaajili nani atalipa?
 
Wanatapatapa tu hawa na huku wakionyesha uwezo wao finyu katika kutatua matatizo mbali mbali yanayohusu nchi yetu. Sasa wanathubutu hata kudanganya eti madaktari 1,000 watakaoingia nchini hawatalipwa chochote!!! Pumbavu kabisa!!!
 
Akili ndogo kuongoza akili kubwa,kweli serekali legelege huzaa viongozi legelege,dhaifu,liwalo na liwe.
 
Kingine lugha, hao madaktari wa iran isije kuwa kama wachina na wajapan wanatumia lugha zao sasa wakija hapa kiarabu tutaweza? Watalala wapi, watafikaje hospitali ili hali ni wageni kabisa. Hata kama hawatalipwa lakini bado utata upo.
Hapo ndio umuhimu wa kwenda Madrasa utaonekana maana waliopitia huko hawatapata shida kuwasiliana na madaktari toka Iran. Let's wait and see
 
nikimaliza tu chuo, natimkia botswana..... huku longolongo tu
 
Wakuu hivi hao madoctor wa kiiran watacommunicate vipi bibi yangu ngw'ana mpandji wa hapa kisesa mwanza?manake nasubiri tu waanze kazi nimpeleke kwa ajil ya clinic yake ya moyo.tatizo bibi anapenda kueleza matatizo yake straight kwa doctor..cjui itakuwaje make bibi hataki upambe especially anapokuwa antaka kuongea na doctor yani hataki ukalimani..........nawasilisha
 
Hapo ndio umuhimu wa kwenda Madrasa utaonekana maana waliopitia huko hawatapata shida kuwasiliana na madaktari toka Iran. Let's wait and see

Umuhim wa madrasa hapo haupo, kumbuka Iran(Persia) si waarabu, ni waajemi, wanaongea kiajemi/farsi.
Watakuwa wanalipwa na Rostam, ni ndugu yao.
 
Back
Top Bottom