wakuu!
kuna tetesi zimezagaa mtaani na humu jamvini kuwa serikali ina mpango wa kuleta madaktari kutoka nje ya nchi, hasa nchi ya Irani ikitajwa zaidi. Hawa ni madaktari wa kigeni ambao kama mpango huo utafanikiwa watakuja nchini ili kunusuru sekta ya afya.
kwa maoni yangu ujio wa madaktari hawa (kama ni kweli wataletwa) utapelekea mgomo mwingine mkubwa zaidi katika sekta ya afya kuwahi kutokea. Mgomo huu ambao sasa utaratibiwa na kutekelezwa na madaktari wa kigeni utakuwa kwa sababu zifuatazo.
Kwanza, madaktari wa kigeni watagoma kutokana na kuwako kwa vifaa duni vya kutolea tiba katika hospitali za umma hapa nchini ikiwamo hosp ya taifa muhimbili. Hili ni miongoni mwa mambo ambayo madaktari wazalendo wamekuwa wakilililia kila mara.
Madaktari wa kigeni watagoma wakihitaji viletwe vifaa vya kisasa katika hosp watakazopelekwa ili kuendana na ujuzi na taaluma zao jambo litakalowawezesha kutoa tiba stahiki kwa wagonjwa.
Suala la mishahara na posho za madaktari wapya (wa kigeni) litazua mjadala mzito zaidi kwani malipo kwa madaktari hao ni mara tatu zaidi ya yale ya madaktari wazalendo. Serikali itashindwa kuwalipa madaktari hawa kwani kwa maelezo yake ni kuwa haina fedha na kulingana na huko inapotarajiwa kuwaleta (Irani) kuna uwezekano wakajitoa muhanga pale muhimbili na kwingineko.
Madaktari wa kigeni pia watagoma ili serikali ipeleke vitanda kwa ajili ya wagonjwa mahospitalini ili wagonjwa wasilale chini ama wawili wawili wodini hii ikiwa sambamba na kuhakikisha kuwa zipo dawa na vifaa tiba vya kutosha mahospitalini ili waweze kutoa huduma kwa wagonjwa.
Hivyo basi suala la kuleta madaktari wa kigeni linaweza lisiwe suluhisho la mgomo wa madaktari iwapo mazingira ya kufanyia kazi na maslahi kwa madaktari hayataboreshwa! Serikali iliwahi kukiri kupitia waziri mkuu kuwa madai ya madaktari ni ya msingi nashauri msingi huo pia uzingatiwe katika majadiliano ili kufikiwe muafaka
Serikali isitafute njia ya mkato kulishughulikia hili....
kwani tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliahirisha au kulikimbia...
kuna tetesi zimezagaa mtaani na humu jamvini kuwa serikali ina mpango wa kuleta madaktari kutoka nje ya nchi, hasa nchi ya Irani ikitajwa zaidi. Hawa ni madaktari wa kigeni ambao kama mpango huo utafanikiwa watakuja nchini ili kunusuru sekta ya afya.
kwa maoni yangu ujio wa madaktari hawa (kama ni kweli wataletwa) utapelekea mgomo mwingine mkubwa zaidi katika sekta ya afya kuwahi kutokea. Mgomo huu ambao sasa utaratibiwa na kutekelezwa na madaktari wa kigeni utakuwa kwa sababu zifuatazo.
Kwanza, madaktari wa kigeni watagoma kutokana na kuwako kwa vifaa duni vya kutolea tiba katika hospitali za umma hapa nchini ikiwamo hosp ya taifa muhimbili. Hili ni miongoni mwa mambo ambayo madaktari wazalendo wamekuwa wakilililia kila mara.
Madaktari wa kigeni watagoma wakihitaji viletwe vifaa vya kisasa katika hosp watakazopelekwa ili kuendana na ujuzi na taaluma zao jambo litakalowawezesha kutoa tiba stahiki kwa wagonjwa.
Suala la mishahara na posho za madaktari wapya (wa kigeni) litazua mjadala mzito zaidi kwani malipo kwa madaktari hao ni mara tatu zaidi ya yale ya madaktari wazalendo. Serikali itashindwa kuwalipa madaktari hawa kwani kwa maelezo yake ni kuwa haina fedha na kulingana na huko inapotarajiwa kuwaleta (Irani) kuna uwezekano wakajitoa muhanga pale muhimbili na kwingineko.
Madaktari wa kigeni pia watagoma ili serikali ipeleke vitanda kwa ajili ya wagonjwa mahospitalini ili wagonjwa wasilale chini ama wawili wawili wodini hii ikiwa sambamba na kuhakikisha kuwa zipo dawa na vifaa tiba vya kutosha mahospitalini ili waweze kutoa huduma kwa wagonjwa.
Hivyo basi suala la kuleta madaktari wa kigeni linaweza lisiwe suluhisho la mgomo wa madaktari iwapo mazingira ya kufanyia kazi na maslahi kwa madaktari hayataboreshwa! Serikali iliwahi kukiri kupitia waziri mkuu kuwa madai ya madaktari ni ya msingi nashauri msingi huo pia uzingatiwe katika majadiliano ili kufikiwe muafaka
Serikali isitafute njia ya mkato kulishughulikia hili....
kwani tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliahirisha au kulikimbia...