Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Kwa mujibu wa taarifa ya habari ya saa mbili usiku wa jana, ni wazi kwamba madaktari wametangaza rasmi kuanza mgomo leo na hata hapa Mwanza katika hospitali ya BUGANDO tayari matangazo yamebandikwa kuarifu kuanza rasmi kwa mgomo huo.
Ushauri wangu kwa Serikali:
1. Ulinzi uimarishwe katika hospitali zote na Madaktari wasiruhusiwe tena kufika maeneo hayo kwa vile siyo watumishi kwa wakati huo na kama ni vikao watafute maeneo mengine.
2. Dispensari zote binafsi zinazomilikiwa na Madaktari waliogoma zifungwe Kwa vile Madaktari wengi walio na dispensari hizo wamekuwa wakitumia vifaa, madawa na raslimali za walipa kodi katika dispensari hizo.
3. Takukuru wasambazwe katika Hospitali zote ambazo kuna mgomo ili kubaini vitendo vya rushwa ili kufanya matibabu pale wanapohongwa, tatizo lililolalamikiwa na wengi katika mgomo uliotangulia.
NB. Wananchi sasa tutambue kuwa nchi yetu haina Madaktari bali Magaidi na tukumbuke pia kuwa mara kadha tumekuwa tukikosa huduma kwa madai kuwa hakuna dawa huku wakituelekeza kwenda kutibiwa katika dispensari zao nahata kununua dawa katika maduka wanayomiliki wao , dawa ambazo wamekuwa wakizihamisha kutoka maeneo yao ya kazi. Hivyo ni aibu kubwa kuwatetea Madaktari hawa wakati hata katika mazingira ya kawaida wamekuwa wakituonesha hawana utu.
Ushauri wangu kwa Serikali:
1. Ulinzi uimarishwe katika hospitali zote na Madaktari wasiruhusiwe tena kufika maeneo hayo kwa vile siyo watumishi kwa wakati huo na kama ni vikao watafute maeneo mengine.
2. Dispensari zote binafsi zinazomilikiwa na Madaktari waliogoma zifungwe Kwa vile Madaktari wengi walio na dispensari hizo wamekuwa wakitumia vifaa, madawa na raslimali za walipa kodi katika dispensari hizo.
3. Takukuru wasambazwe katika Hospitali zote ambazo kuna mgomo ili kubaini vitendo vya rushwa ili kufanya matibabu pale wanapohongwa, tatizo lililolalamikiwa na wengi katika mgomo uliotangulia.
NB. Wananchi sasa tutambue kuwa nchi yetu haina Madaktari bali Magaidi na tukumbuke pia kuwa mara kadha tumekuwa tukikosa huduma kwa madai kuwa hakuna dawa huku wakituelekeza kwenda kutibiwa katika dispensari zao nahata kununua dawa katika maduka wanayomiliki wao , dawa ambazo wamekuwa wakizihamisha kutoka maeneo yao ya kazi. Hivyo ni aibu kubwa kuwatetea Madaktari hawa wakati hata katika mazingira ya kawaida wamekuwa wakituonesha hawana utu.