Mgomo wa madaktari - Updates

Mgomo utapita kama ilivyopita mingine, na huu sio wa kwanza wala wa mwisho.

Ndugu yangu si kweli mgomo huu utapita bure, mgomo huu unapita na roho za watanzania maskini. Migomo mingine kweli ilipita, kwa kuwa kama shule zilifungwa kisha zikafunguliwa na watoto wakaendelea na masomo, vituo vya dala dala na vya treni vilifungwa kisha vilifunguliwa na abiria wakaendelea na safari zao. Lakini mtu aliyepatwa na mstuko wa moyo (Cardiac Arrest) na kukosa huduma ya daktari, hawezi kuamka tena na ndo maana leo Mhe. Rais amekutana na viongozi wa madaktari kuangalia jinsi gani ya kumaliza mgomo huu. Natumaini Mhe. Rais atatumia busara tena, kama kwenye Mswada wa Katiba mpya.

Mungu ibariki Tanzani.
 
Sasa kama mkuu amekutana na viongozi wa MAT hivi kwa nini alikuwa anasita toka mwanzo ?
 
Mimi nimeuliza hivi, Ikiwa Mponda na Nkya walijaribu walivyoweza lakini walikwama kutokana na mipango hiyo kuwa maamuzi yanatoka juu zaidi..Mlityaka wafanye nini? Mnakumbuka swala la Richmond jinsi Msabah alivyokuwa mdogo akisema yeye hakuwa na mamlaka! Lakini mwisho wa siku yeye ndiye akaondolewa madarakani (kujiuzuru) lakini hadi leo Umeme hatuna na ngoma imesimama pale pale. Tutafute kwa undani who is responsible kama ni JK mwenyewe tuyaelekeze malalamiko haya kwake sio waziri ambaye kasema jamani eeeh mimi ni mbunge tu ninawajibika kwa watu wangu wa Jimbo... Haya maneno yanazungumza mengi zaidi ya Ujeuri!
 
8E9U2768.JPG
Kikwete katika mkutano na madaktari ikulu.
wa kwanza kulia, Rais wa MAT Dr Mkopi,
next katibu mkuu MAT Dr Kabangila,
next Prof. Yongolo consultant urologist MNH,
mwisho kwenye kona Dr. Ulimboka
 
Rafiki,
naona unashadadia as if ni kitu kizuri sanaaaaaa.
ni mambo matatu
1. kwa serikali
act faster kwa hicho mlichojipanga(stmt from Mh. Pinda)
ushauri
-tangaza nafasi za udaktari ndani na nje ya TZ.
-privatised medical sector
2. kwa madaktari
-rudini kazini
-kwa wale wanaogoma tu kwa shinikizo la wengine be careful ulisoma peke yako na ukakaribia na kua daktari kama ww
speak out then serikal ikusaidie si kwa njia ya kusababisha mauaji/hofu kwa wagonjwa
-ninyi ambao mna channels kwenye ma NGO halafu mnawachuza wenzenu M/Mungu atawalipizia humu humu dunian, kwan hata mkifukuzwa tayari mna kazi sehem nyingine
3. wananchi
-mgomo wa madaktar unaweza kua ni sahihi ila tutazame kwa kina jamaa wamekosea,maombi yao mengi ni nadhalia zaid kuliko uhalisia na iwapo wakitimiziwa haya next watakuja na complicated things na pia je kuna halufu ya kuchochowa!!!

pole sana ndugu...mpe salamu aliyekutuma
 
8E9U2755.JPG
JJK akipeana mkono na Dr. DUX, katikati karibu na Dux ndo Dr. Ulimboka kwa msiomjua.
Nyuma ya JK anayesmile ni Rais wa MAT Dr. Namala Mkopi

Dr Ulimboka na wengine wote katika safu nimewapenda tuwe na watu wanaoweza kuficha uoga kama hawa! hii itabadili mfumo katika sakta nyingi tu!
 
Ndugu yangu si kweli mgomo huu utapita bure, mgomo huu unapita na roho za watanzania maskini. Migomo mingine kweli ilipita, kwa kuwa kama shule zilifungwa kisha zikafunguliwa na watoto wakaendelea na masomo, vituo vya dala dala na vya treni vilifungwa kisha vilifunguliwa na abiria wakaendelea na safari zao. Lakini mtu aliyepatwa na mstuko wa moyo (Cardiac Arrest) na kukosa huduma ya daktari, hawezi kuamka tena na ndo maana leo Mhe. Rais amekutana na viongozi wa madaktari kuangalia jinsi gani ya kumaliza mgomo huu. Natumaini Mhe. Rais atatumia busara tena, kama kwenye Mswada wa Katiba mpya.

Mungu ibariki Tanzani.

anatumia busara leo wakati watu wamekufa ,,,halafu ni vichekesho tuamini la nani ..mahakama ,pinda au jk nachanganyikiwa sijui nchi inaongozwaje.
hakuna maamuzi ya pamoja
 
Acha wafe kabisa, na wafe kweli hata kama mie nikifa acha nife lakini najua kwa hili mtanzania atakuwa kaniua. Hakuna kuilaumu serikali wala ma-dr. Watanzania wenyewe mmeiweka serikali madarakani. Upumbavu wenu acha uwagharimu. Mtu anasema chagua ccm chagua chama cha nyerere. What a hel r u thnkng? Kufa, kufa kabisa. Na inflation acha ifike 100%. Unga, petrol na umeme vipande bei zaidi ili mjue kuwa mliweka madarakani matapishi yenu. Can u imagine, awamu ya 2 imechukua sukari tsh.450/= imetuachia sukari tsh.650/=. Awamu ya 3 imechukua tsh. 650/= miaka 6.5 sukari ni 2200+ bado 2015 hatujafka. Nyie mnailaumu serikali. JILAUMUNI WENYEWE NA UJINGA WENU WA KUFIKIRI km 2 ahead wenzenu wanafkiri km 1000 ahead.
 
8E9U2755.JPG
JJK akipeana mkono na Dr. DUX, katikati karibu na Dux ndo Dr. Ulimboka kwa msiomjua.
Nyuma ya JK anayesmile ni Rais wa MAT Dr. Namala Mkopi

Hivi JK anapotoa mkono kwa hawa madaktari wakati mkono wake uko mfukoni ana maana gani?? Pamoja na kwamba yeye ni Rais, hii kwa kiasi fulani ni dharau kwa mtu unayemsalimia.
 
Nashindwa kuelewa hv swala la ministerial responsibility haliaply Tz au ndo tunalindana maana cdhan kama inahtaj mgomo mpya kwa waziri kujiuzur knapotokea makosa ya wazi kwenye wizara yake! Viva madoct najua itatucost watz wakawaida lakn hakuna kizur kscho na sacrifice! I support doctors and i curse th gvt
 
Acha wafe kabisa, na wafe kweli hata kama mie nikifa acha nife lakini najua kwa hili mtanzania atakuwa kaniua. Hakuna kuilaumu serikali wala ma-dr. Watanzania wenyewe mmeiweka serikali madarakani. Upumbavu wenu acha uwagharimu. Mtu anasema chagua ccm chagua chama cha nyerere. What a hel r u thnkng? Kufa, kufa kabisa. Na inflation acha ifike 100%. Unga, petrol na umeme vipande bei zaidi ili mjue kuwa mliweka madarakani matapishi yenu. Can u imagine, awamu ya 2 imechukua sukari tsh.450/= imetuachia sukari tsh.650/=. Awamu ya 3 imechukua tsh. 650/= miaka 6.5 sukari ni 2200+ bado 2015 hatujafka. Nyie mnailaumu serikali. JILAUMUNI WENYEWE NA UJINGA WENU WA KUFIKIRI km 2 ahead wenzenu wanafkiri km 1000 ahead.

Taratibu Mkuu, unazungumzia awamu ya tatu ipi, ya Beni? Beni ni wakupigiwa mfano, hakuwahi kupandisha inflation kiasi hicho.
 
Kama hutaki kurudi meza ya mazungumzo hadi waziri ajiuzulu, ina maana unataka mazungumzo bila waziri (common sense ni kwamba waziri hafanyi maamuzi binafsi, kuna kanuni, taratibu na maelezo mengine ambayo inabidi ayafuate wakati anafanya kazi- na hii inaaply kwa mfanyakazi mwingine yeyote). Kwa hiyo basi, Waziri akijiuzulu, au akaondolewa kwenye nafasi hiyo na Rais, basi lazima hiyo nafasi izibwe na waziri mwingine - ambaye atafanya kazi kwa kanuni, taratibu, sheria na maelekezo yale yale ambayo waziri msiyemtaka amekuwa akifanya kazi kwayo. Kumkataa waziri sio suluhisho la matatizo yeni, na hilo mnalijua fika.

Impliation ya madai ya kuondolewa waziri ili mkae meza ya mazungumzo ni kuwa hamtaki kuongozwa, mnataka mjiongoze ili mhakikishe mnapata vifaa, mazingira, posho, mishahara na stahiki zenu kadri mnavyopenda na mnavyoona inawasuit. Ingekuwa vinginevyo mngerudi meza ya mazungumzo (unless matakwa yenu mnayalazimisha kama vile sekta ya afya ndo muhimu kuliko sekta ya elimu, maji, kilimo nk ambao mnadhani wao hawana matakwa kama mliyonayo).

Wananchi malimbukeni kama mimi tunaona haina haja ya kuwa na madaktari wanaotaka kuua kwa maslahi yao binafsi badala ya kufa wao kwa ajili ya maslahi ya wengi. Mnastahili kuwajibishwa na nadhani mwenye mamlaka anachelewa sana kuwawajibisha.

Hoja zako hazina nguvu. Wanachi wamekwisha kutimizia wajibu wao kwa kukusomesha kupitia kodi zao. Bila wananchi kutimiza wajibu huo usingekuwa hapo ulipo. Unapaswa kushukuru kwa hilo kwanza. Kwa upande wa serikali, kama kuna mahali seikali yako haikukufanyia vizuri haikuhalalishii wewe kufanya kosa. Makosa mawili hayafanyi jambo kuwa sahihi. Usijenge hoja kwa kuiga kosa la mtu mwingine.

Jambo muhimu kwa pande zote kujua kanuni za majadaliano ( negotiations) Majadiliano yaweza kuwa '' hardball'' ya ushindani au '' corperative' akushirikiana. Hardball hutumika kama watu wanaojadiliana hawatahusiana kwa mara nyingine na corperative kwa wale ambao mahusiano yao niendelevu

Uhusiano wa madaktari na Serikali ni endelevu hivyo majadilino yanayofaa ni ya kushirikina ili kutatua tatizo lililopo.

Jambo lingine muhimu ni matumizi ya nguvu (powers) ambazo pande zote zinazo na jinsi ya kuzitumia. Matumizi mabaya ya nguvu yanaweza kuchelewesha kufikia mwafaka au kuharibu kabisa mwenenendo mzima wa majadiliano. soma zaidi http://web.cba.neu.edu. Madaktari na serikali kwa wakti tofauti mmetumia vitisho jambo limetufikisha hapa.

Madai ya msingi ya madaktari ni halali kabisaa.
  1. Ukosefu wa vitendea kazi
  2. Mazingira magumu ya kazi (na ya kujifunza - kwa Ma-Interns)
  3. Mishahara/posho ndogo

Tatizo la madaktari waliopo mafunzoni kutolipwa posho zao lilikuwa uzembe wa watendaji wakuu wa wizara ya afya, ambao tayari wameshawajibishwa (Katibu Mkuu - Mama Blandina Nyoni na Mganga Mkuu - Dr Deo Mtasiwa). Baada ya hapo serikali ilikubali kuwa na mazungumzo na madaktari kuhusu matatizo mengine yaliyotolewa na madaktari; vikao kadhaa tayari vimefanyika na bado mazungumzo yalikuwa hayajasitishwa.

Suala la MAT kudai kuwa viongozi wa kisiasa wa wizara wafukuzwe au wajiuzulu, vinginevyo madaktari wataendelea na mgomo ni dhana ambayo haikufanyiwa "homework" vizuri.
  1. Wizara ya afya siyo kwa ajili ya madaktari tu (Kuna madaktari (MD), Manesi, Wafamasia, Wataalamu wa maabara, wataalamu wa mama cheza (physiotherapists), Optometrists na wengine wengi tu. Sijui kama madai ya kutaka Waziri na Naibu wake wafukuzwe ni madai yanayowakilisha taaluma nyingine za tiba!
  2. Waziri na Naibu wake ni viongozi wa kisiasa kwenye wizara; kwa maana nyingine ni wawakilishi wa Rais kwenye wizara, na jukumu lao kubwa ni kusimamia utekelezaji wa sera SIYO UTENDAJI. CEO wa wizara ni Katibu Mkuu.Kudai mawaziri hawa wafukuzwe ni kumwamuru Rais afanye mabadiliko ya Cabinet!
  3. MAT siyo chama cha kutetea "Labour related issues" za madaktari. MAT ni NGO kama ilivyoainishwa kwenye tovuti yao kuwa
  4. Hili suala la mawaziri mbona halikuwa kwenye madai ya mwanzo?
  5. Duniani kote kuna taratibu za kuitisha migomo, ikiwa ni pamoja na kutoa notice ya siku kadhaa (siyo siku 4) na kuhusisha "trade union" inayowakilisha wafanyakazi hao. Je, MAT walifanya hivyo?

Ombi langu kwa madaktari wanaogoma: Jamani mwogopeni Mungu; waoneeni huruma maskini wagonjwa. madai yenu ya msingi ni halali kabisaa, lakini hili la mawaziri liangalieni upya. Rejeeni kwenye mazungumzo na serikali.


Wakuu hapo juu.......asanteni sana kwa mawazo mazuri.......

......madai ya madaktari kuhusu mazingira ya kazi ni ya msingi na yashughulikiwe tena nasema URGENTLY.....lakini madai ya eti Mawaziri wajiuzulu kwa kuwa wao ndio vikwazo.......narudia.....ni UKILAZA USIO NA KIFANI.......utafikri mijitu haifikirii au haijaenda shule.......

Yaani madaktari wanataka kutuchagulia Mawaziri..............halafu siku nyingine wahandisi wagome kwa kuwa Magufuli anakwamisha matakwa yao ya msingi..........halafu....wanasheria nao.......waje wagome wadai hawamtaki Celina.......halafu siku nyingine wanajeshi nao wagome waseme hawamtaki Dr. Hussein........THIS IS ABSOLUTE RIDICULOUS......
 
Hivi JK anapotoa mkono kwa hawa madaktari wakati mkono wake uko mfukoni ana maana gani?? Pamoja na kwamba yeye ni Rais, hii kwa kiasi fulani ni dharau kwa mtu unayemsalimia.
Hajafanya hivo makusudi.
iyo ni body language kuwaonyesha madokta kuwa ye ndo RAIS.
Kunakuwa na tatizo nyumbani kama baba unaanza kuwaambia watoto wako kuwa "unajua mi ndo baba yenu?"
 
Wakuu hapo juu.......asanteni sana kwa mawazo mazuri.......

......madai ya madaktari kuhusu mazingira ya kazi ni ya msingi na yashughulikiwe tena nasema URGENTLY.....lakini madai ya eti Mawaziri wajiuzulu kwa kuwa wao ndio vikwazo.......narudia.....ni UKILAZA USIO NA KIFANI.......utafikri mijitu haifikirii au haijaenda shule.......

Yaani madaktari wanataka kutuchagulia Mawaziri..............halafu siku nyingine wahandisi wagome kwa kuwa Magufuli anakwamisha matakwa yao ya msingi..........halafu....wanasheria nao.......waje wagome wadai hawamtaki Celina.......halafu siku nyingine wanajeshi nao wagome waseme hawamtaki Dr. Hussein........THIS IS ABSOLUTE RIDICULOUS......
Madaktari hawajamzuia profesheno yeyote kufanya analoliona kuwa ni sahihi,
kama ni hivo basi wahandisi na waige.
 
Mtawakomboaje watanzania kwa kutomtaka waziri? unadhani shida kubwa ya watanzania ni afya?

Assume waziri kajiuzulu na madai yenu yote mmetimiziwa kesho, je mnaweza tibu wagonjwa bila umeme, maji etc?

Mmefanya kosa kuingiza, kuingia au kuingizwa kwenye siasa na kusahau wajibu wenu.
Nimekufuatilia sana hoja zako. Ni nzuri ila zina ukomo wa fikra. Ulivyomalizia angalau ungetoa ukweli wa 'kosa kuingiza, kuingia au kuingizwa kwenye siasa na kusahau wajibu wenu" kwa kutaja bayana mazingira yaliyosababisha tukio hilo.

Pia umechangia sana upande mmoja tu wa kosa la madaktari, hivi kweli pamoja na serikali kukiri mapungufu huoni kuwa kuna kosa?

Nimefuatila michango karibu yote hapa na vyombo vingine vya habari. Linalojitokeza ni kuwa kila sekta nchini ina manung'uniko ya upungufu wa utendaji na uwajibikaji wa serikali kama unavyoshuhudia hii migogoro/

Kama sisi ni wa kweli basi ili mradi serikali inafanya kazi kwa shinikizo kwa sababu ya kutowajibika itumike njia na lugha inayoeleweka na serikali ya SHINIKIZO. Itabakia kweli hata mwisho wa dahali kuwa HAKI HAIOMBWI BALI INATAFUTWA.

Inawezekana baadhi yetu mmeshapata haki zenu kwa njia mnazojua, wengine hatuna jinsi bali kudai hizo haki kwa njia tunayoiweza.
 
Madaktari hawajamzuia profesheno yeyote kufanya analoliona kuwa ni sahihi,
kama ni hivo basi wahandisi na waige.

kuna watu either ni kwa kutokujua/utoto(not experienced)/just decided to behave awakwardly.......wenye kufikiri critically hawawezi kuiga upuuzi wa hoja ya kujiuzulu Waziri eti ndio vikwazo vitaondoka........

Kusoma sayansi haimaanishi tuwe wajinga kwenye masuala ya kiutendaji na kiutawala na mambo yote yanayo-surround issue hizo...kuanzia policies nk nk nk.........technically hata waziri wa Afya akijiuzulu leo.......haitabadilisha chochote......

notwithstanding matatizo ya msingi waliyonayo madaktari......ambayo pia yapo kwenye sekta nyingine......ninahisi madaktari wanataka kutumia mgongo wa afya za wananchi kuumia/kufa.......ili kujinufaisha.......kudai eti wanatupigania wananchi......i do not buy it........

Wananchi may be ignorant....but they ain't stupid.........
 
JK utakutana sana na ma-dr lkn ungefupisha mikutano nao hawa watu kama tu ungewasikiliza toka mapema;serikali yetu ina tabia ya kusikiliza matatizo hadi yawe makubwa;huo ni udhaifu kwenye utendaji!

Zuia tatizo lingali bado changa na ndiyo nchi zinazojali wapiga kura wake zinavyofanya!
 
Kama hutaki kurudi meza ya mazungumzo hadi waziri ajiuzulu, ina maana unataka mazungumzo bila waziri (common sense ni kwamba waziri hafanyi maamuzi binafsi, kuna kanuni, taratibu na maelezo mengine ambayo inabidi ayafuate wakati anafanya kazi- na hii inaaply kwa mfanyakazi mwingine yeyote). Kwa hiyo basi, Waziri akijiuzulu, au akaondolewa kwenye nafasi hiyo na Rais, basi lazima hiyo nafasi izibwe na waziri mwingine - ambaye atafanya kazi kwa kanuni, taratibu, sheria na maelekezo yale yale ambayo waziri msiyemtaka amekuwa akifanya kazi kwayo. Kumkataa waziri sio suluhisho la matatizo yeni, na hilo mnalijua fika.

Impliation ya madai ya kuondolewa waziri ili mkae meza ya mazungumzo ni kuwa hamtaki kuongozwa, mnataka mjiongoze ili mhakikishe mnapata vifaa, mazingira, posho, mishahara na stahiki zenu kadri mnavyopenda na mnavyoona inawasuit. Ingekuwa vinginevyo mngerudi meza ya mazungumzo (unless matakwa yenu mnayalazimisha kama vile sekta ya afya ndo muhimu kuliko sekta ya elimu, maji, kilimo nk ambao mnadhani wao hawana matakwa kama mliyonayo).

Wananchi malimbukeni kama mimi tunaona haina haja ya kuwa na madaktari wanaotaka kuua kwa maslahi yao binafsi badala ya kufa wao kwa ajili ya maslahi ya wengi. Mnastahili kuwajibishwa na nadhani mwenye mamlaka anachelewa sana kuwawajibisha.

Bora umejitambua kuwa wewe ni LIMBUKENI katika maana halisi. Riwa achana naye, kubishana naye ni kama kujaribu kuua inzi kwa shoka!
 
Inatia uchungu saana, kama ni mgonjwa au unauguliwa na ndugu yako kipindi kama hiki. Ni vigumu kuwaelewa madaktari hata kwa bunduki.poleni saana wote.
Kilichotufikisha hapa ndio cha msingi. Historia inaonyesha kwamba, bila mgomo , serikali yetu huwa haitimizi wajibu. Manung'uniko kwenye jamii nimakubwa kuliko huo mgomo wa madaktari, fa nya ka uchunguzi ka kijinga (upeo mdogo utabaini).
1. Mara ngapi tumeshuhudia wanafunzi wa vyuo hadi waandamane wapigwe mabomu, alafu siku hiyo hiyo ndo wanawekewa pesa kwenye akaunti. Ulishasikia aliyesababisha hayo kaguswa zaidi ya wanafunzi kufukuzwa na kusimamishwa masomo?
2.hadi wanafunzi wa shule ya msingi/raia walale barabarani ndio waweke matuta.
3.pinda anasema wanaingilia mamlaka ya mkuu. Kutupadishia mafuta ya taa (500/= hadi 2100/=) kwa kushindwa kuwaadhibu wachakuaji mamlaka haikupangiwa cha kufanya na wachakachuaji.
4.ni ripoti ngapi za wizi wa waziwazi zinalipotiwa na rudovic uto, lini umesikia mtu kapandishwa karandinga .

Hivi unajua hatuna chama cha wafanya kazi tz. Kumbuka enzi za kolimba.

Madaktari na wanasiasa, ni nani muuaji mkubwa? (rwanda , iraq, liberia, siera leone, kenya,syria na kwingineko??????????

tunaombwe kubwa la uongozi tz. Huyo ndo muuaji wetu
.
Hali ya nchi si shwari.
 
Back
Top Bottom