LeopoldByongje
JF-Expert Member
- Apr 28, 2008
- 372
- 13
Wadau. Mtapenda kufahamu kuwa SHIVACOM na ALPHATEL ni wakala wa VODACOM kwa kuchapisha na kusambaza vocha na bidhaa za simu za viganjani. Wamiliki wa SHIVACOM na ALPHATEL ndio waasisi wa dili ya kitapeli ya RICHMOND na DOWANS ambazo zinaendelea kulifilisi taifa hili. Kampuni hizi zinatengeneza pesa mabilioni kwa siku kupitia mgongoni mwa waTZ. Wamiliki wa makampuni haya si wengine bali ni ROSTAM AZIZI na EDWARD LOWASSA. Watu hawa Wanajigamba kutengeneza mabilioni hayo hasa lile tamko la mwaka jana la kijeuri kutetea mwanae Lowassa alipotaka kununua nyumba huko UK na watu wakahoji pesa hizo zote alikokuwa amezipata.
Kubwa zaidi hao akina Lowassa na Rostam Aziz wanafanya kila liwezekanalo kushika hatamu za uongozi wa nchi hii 2015 ili waendelee kutuibia na kupora mali za nchi hii liulaini. Wameishafanikiwa kuliteka Bunge. Lowassa sasa ni Mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wameiteka NEC ya CCM. Kwa hiyo njia ya kuingia IKULU ni nyeupe. Magazeti yao hususani RAI, MTANZANIA yameishaanza kazi ya kuwasafisha. Tusikubali hali hii iendelee. Tuwazuie mapema kwa kutumia nguvu ya umma kwa kuendesha kampeini za kususia kununua bidhaa zao na za washirika wao. Kazi hii ianze mara moja.
Kubwa zaidi hao akina Lowassa na Rostam Aziz wanafanya kila liwezekanalo kushika hatamu za uongozi wa nchi hii 2015 ili waendelee kutuibia na kupora mali za nchi hii liulaini. Wameishafanikiwa kuliteka Bunge. Lowassa sasa ni Mwenyekiti wa kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wameiteka NEC ya CCM. Kwa hiyo njia ya kuingia IKULU ni nyeupe. Magazeti yao hususani RAI, MTANZANIA yameishaanza kazi ya kuwasafisha. Tusikubali hali hii iendelee. Tuwazuie mapema kwa kutumia nguvu ya umma kwa kuendesha kampeini za kususia kununua bidhaa zao na za washirika wao. Kazi hii ianze mara moja.