Tukundane
JF-Expert Member
- Apr 17, 2012
- 11,455
- 8,249
Mgombea Ubunge aliyeshindwa katika kura za maoni kupitia chama cha mapinduzi ambaye jina lake halijatajwa katika jimbo mojawapo la wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.
Akiwa amepandwa na hasira kutokana na kushindwa kwenye kura za maoni amewapiga mkwara wapiga kura wa jimbo hilo kwa kuwataka wamrudishie fedha na mali mbalimbali ambazo alikuwa amewahonga ili wamchague kuwa mgombea kupitia chama hicho na kama watashindwa kurudisha mali zake basi wajiandae kufa kwa uchawi.
Baada ya muda mfupi baadhi ya wananchi walionekana wakiwa wamebeba mabati wakiwa wanayapeleka nyumbani kwa mgombea huyo,mabati ambayo yalitajwa na wahusika kuwa walikuwa wamenunuliwa na mgombea huyo kwa makubaliano ya kumpigia kura.
Chanzo: Bomba FM.
Akiwa amepandwa na hasira kutokana na kushindwa kwenye kura za maoni amewapiga mkwara wapiga kura wa jimbo hilo kwa kuwataka wamrudishie fedha na mali mbalimbali ambazo alikuwa amewahonga ili wamchague kuwa mgombea kupitia chama hicho na kama watashindwa kurudisha mali zake basi wajiandae kufa kwa uchawi.
Baada ya muda mfupi baadhi ya wananchi walionekana wakiwa wamebeba mabati wakiwa wanayapeleka nyumbani kwa mgombea huyo,mabati ambayo yalitajwa na wahusika kuwa walikuwa wamenunuliwa na mgombea huyo kwa makubaliano ya kumpigia kura.
Chanzo: Bomba FM.