Mgombea ubunge wa chadema afukuzwa kazi serikalini

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Jul 1, 2008
10,564
7,973
Wadau,
Kama mnavyofahamu kuna baadhi ya watumishi wa serikali walioamua kutumia haki yao ya kidemokrasia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi yetu kwenye uchaguzi mkuu wa 2010.Wapo waliogombea kupitia ccm na wengine vyama vya upinzani.

Miongoni mwa wengi waliogombea kupitia vyama vya upinzani ni mwalimu Marwa Ryoba(Mwalimu wa shule ya sekondari Tarime) anayefundisha masomo ya sayansi (fizikia na kemia). Huyu bwana 'inasemekana" amefukuzwa kazi mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 kwakuwa aligombea kupitia chama cha upinzani.

Binafsi nimeongea naye, ameniambia serikali imesitisha mshahara wake tangu mwezi novemba mwaka jana, pamoja na kwamba alirejea kazini kwake mara tu baada ya uchaguzi.Pamoja na juhudi alizofanya kutaka kujua sababu ya kusitishwa mshahara wake, hajapewa majibu ya kueleweka na wala hajapewa barua rasmi kumjulisha kama amefukuzwa kazi, ama kasimamishwa kazi ama kuna tatizo gani lililosababisha kufikiwa kwa uamuzi huo.

Kwakuwa hili jambo linaweza kuwa limewatokea watumishi wa umma wengi, kama ilivyomtokea Pro.Baregu mwaka juzi, nadhani kuna sababu za msingi hili jambo likawekwa wazi, kama ni muongozo wa utumishi wa umma uwekwe wazi ili kila mtu ajue.Ni jambo la ajabu kwamba mtumishi wa umma akiwania nafasi ya kisiasa kupitia ccm inakuwa halali lakini akifanya hivyo kupitia vyama vya upinzani inakuwa haramu.

Hii tabia ya serikali kuleta ubaguzi miongoni mwa watanzania inabidi tuipinge kwa nguvu zote. Ili kila mwananchi awe na uhuru wa kweli wa kushiriki zoezi la demokrasia pasipo na kificho wala wasiwasi.

Nawasilisha.
 
Wadau,
Kama mnavyofahamu kuna baadhi ya watumishi wa serikali walioamua kutumia haki yao ya kidemokrasia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi yetu kwenye uchaguzi mkuu wa 2010.Wapo waliogombea kupitia ccm na wengine vyama vya upinzani.

Miongoni mwa wengi waliogombea kupitia vyama vya upinzani ni mwalimu Marwa Ryoba(Mwalimu wa shule ya sekondari Tarime) anayefundisha masomo ya sayansi (fizikia na kemia). Huyu bwana 'inasemekana" amefukuzwa kazi mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 kwakuwa aligombea kupitia chama cha upinzani.

Binafsi nimeongea naye, ameniambia serikali imesitisha mshahara wake tangu mwezi novemba mwaka jana, pamoja na kwamba alirejea kazini kwake mara tu baada ya uchaguzi.Pamoja na juhudi alizofanya kutaka kujua sababu ya kusitishwa mshahara wake, hajapewa majibu ya kueleweka na wala hajapewa barua rasmi kumjulisha kama amefukuzwa kazi, ama kasimamishwa kazi ama kuna tatizo gani lililosababisha kufikiwa kwa uamuzi huo.

Kwakuwa hili jambo linaweza kuwa limewatokea watumishi wa umma wengi, kama ilivyomtokea Pro.Baregu mwaka juzi, nadhani kuna sababu za msingi hili jambo likawekwa wazi, kama ni muongozo wa utumishi wa umma uwekwe wazi ili kila mtu ajue.Ni jambo la ajabu kwamba mtumishi wa umma akiwania nafasi ya kisiasa kupitia ccm inakuwa halali lakini akifanya hivyo kupitia vyama vya upinzani inakuwa haramu.

Hii tabia ya serikali kuleta ubaguzi miongoni mwa watanzania inabidi tuipinge kwa nguvu zote. Ili kila mwananchi awe na uhuru wa kweli wa kushiriki zoezi la demokrasia pasipo na kificho wala wasiwasi.

Nawasilisha.
Huo ndio ujinga wa serikali yetu. Unamfukuza kazi mwalimu wa Fizikia na Kemia aliyejitolea kufanya kazi ktk mazingira magumu kuikomboa nchi na janga la ujinga!
 
Lkn si waliambiwa kabla ya uchaguzi kua sheria ya utumishi haiwaruhusu kugombea na wakigombea watafukuzwa kazi? Sijaona kosa mie hapo.

Ikiwa wana ccm wanagombea na hawafukuzwi kazi basi ni wajibu wetu kuilazimisha serikali ifate sheria na si kuendelea na sisi kuvunja sheria. Na hapa ndio napata shaka ya hoja ya chadema kweli inaweza kusimamia uadilifu.
 
Huo ndio ujinga wa serikali yetu. Unamfukuza kazi mwalimu wa Fizikia na Kemia aliyejitolea kufanya kazi ktk mazingira magumu kuikomboa nchi na janga la ujinga!

Pamoja na mambo yote, hilo ndo jambo lililonishangaza nami kwa kweli,
wakati huu tunaposhuhudia uhaba mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi lakini serikali yetu inafanya siasa za majitaka kwa kutowatumia vizuri hata hao wachache waliopo. Hii ni aibu kubwa sana kwa serikali yetu kwa kweli.
 
Lkn si waliambiwa kabla ya uchaguzi kua sheria ya utumishi haiwaruhusu kugombea na wakigombea watafukuzwa kazi? Sijaona kosa mie hapo.

Ikiwa wana ccm wanagombea na hawafukuzwi kazi basi ni wajibu wetu kuilazimisha serikali ifate sheria na si kuendelea na sisi kuvunja sheria. Na hapa ndio napata shaka ya hoja ya chadema kweli inaweza kusimamia uadilifu.

Na ndio sababu nikaleta hii hoja ili tuweze kutafuta hii mizania, kwamba mtu akigombea kupitia ccm inakubalika lakini akigombea kupitia vyama vya upinzani haikubaliki. ccm na vyama vya upinzani vyote ni vyama vya siasa, sasa kwa nini kunakuwa na ubaguzi wa namna hii, na wote wanaitumikia nchi yao.
Hebu tujaribu kutafuta suluhu ya hili jambo kwa ustawi wa nchi yetu na watanzania wote kutoka katika makundi mbalimbali. Vinginevyo kuna ulazima wa kuruhusiwa mgombea huru kama sheria za utumishi wa umma zinawzuia watumishi wake kugombea uongozi kupitia vyama vya upinzani, na kwahiyo bado suala la katiba mpya itakayoleta demokrasia ya kweli na uhuru wa kweli ni ya lazima kwa sasa kuliko kipindi kingine chechote.
 
Wadau,
Kama mnavyofahamu kuna baadhi ya watumishi wa serikali walioamua kutumia haki yao ya kidemokrasia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi yetu kwenye uchaguzi mkuu wa 2010.Wapo waliogombea kupitia ccm na wengine vyama vya upinzani.

Miongoni mwa wengi waliogombea kupitia vyama vya upinzani ni mwalimu Marwa Ryoba(Mwalimu wa shule ya sekondari Tarime) anayefundisha masomo ya sayansi (fizikia na kemia). Huyu bwana 'inasemekana" amefukuzwa kazi mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 kwakuwa aligombea kupitia chama cha upinzani.

Binafsi nimeongea naye, ameniambia serikali imesitisha mshahara wake tangu mwezi novemba mwaka jana, pamoja na kwamba alirejea kazini kwake mara tu baada ya uchaguzi.Pamoja na juhudi alizofanya kutaka kujua sababu ya kusitishwa mshahara wake, hajapewa majibu ya kueleweka na wala hajapewa barua rasmi kumjulisha kama amefukuzwa kazi, ama kasimamishwa kazi ama kuna tatizo gani lililosababisha kufikiwa kwa uamuzi huo.

Kwakuwa hili jambo linaweza kuwa limewatokea watumishi wa umma wengi, kama ilivyomtokea Pro.Baregu mwaka juzi, nadhani kuna sababu za msingi hili jambo likawekwa wazi, kama ni muongozo wa utumishi wa umma uwekwe wazi ili kila mtu ajue.Ni jambo la ajabu kwamba mtumishi wa umma akiwania nafasi ya kisiasa kupitia ccm inakuwa halali lakini akifanya hivyo kupitia vyama vya upinzani inakuwa haramu.

Hii tabia ya serikali kuleta ubaguzi miongoni mwa watanzania inabidi tuipinge kwa nguvu zote. Ili kila mwananchi awe na uhuru wa kweli wa kushiriki zoezi la demokrasia pasipo na kificho wala wasiwasi.

Nawasilisha.

Pumbavu sana hawa.
Wapo wengi wanagombea kwa tiketi ya ccm tena hawachukui hata likizo na mshahara wao wanapata kama kawaida.
Peter Kuga Mzirai aligombea Urais na ni mfanyakazi wa wizara ya kilimo makao makuu. Kwa zaidi ya miezi 2 alikuwa kwenye kampeni, na hadi sasa bado ni mwenyekiti wa chama chake. Hatujasikia hata kupewa onyo na bado anaendelea kupeta. Yana mwisho haya.
 
Pamoja na mambo yote, hilo ndo jambo lililonishangaza nami kwa kweli,
wakati huu tunaposhuhudia uhaba mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi lakini serikali yetu inafanya siasa za majitaka kwa kutowatumia vizuri hata hao wachache waliopo. Hii ni aibu kubwa sana kwa serikali yetu kwa kweli.

watoto wao hawasomi huko. But nina uhakika huyo teacher ni marketable masomo yake yanauzika. a solution must be found imediately Im sure wapo wengi wanakumbwa na tatizo kama hilo, Mpe polezake
 
Wadau,

Binafsi nimeongea naye, ameniambia serikali imesitisha mshahara wake tangu mwezi novemba mwaka jana, pamoja na kwamba alirejea kazini kwake mara tu baada ya uchaguzi.Pamoja na juhudi alizofanya kutaka kujua sababu ya kusitishwa mshahara wake, hajapewa majibu ya kueleweka na wala hajapewa barua rasmi kumjulisha kama amefukuzwa kazi, ama kasimamishwa kazi ama kuna tatizo gani lililosababisha kufikiwa kwa uamuzi huo.
Ulimuuliza kama alitoa taarifa kwa mwajili wake kama hatokuwepo katika kituo cha kazi wakati wa uchaguzi? Ama aliomba likizo ili aingie kwenye siasa? Kisha kurudi baada ya uchaguzi? Na kama alichukua likizo ni aina gani ya likizo aliyochukua?
 
Namshauri huyo mwalimu apeleke suala lake katika vyombo vya sheria akianzia kwenye chama cha wafanyakazi. Nawahakikishieni kama tapitia chama cha waalimu au TUGHE kesi hiyo atashinda na akishinda na serikali ikakaidi kumlipa haki zake, kesi inaendelea hadi kufikia mahali pa kumshtaki kiongozi binafsi kwa kukataa kulipa - rejea kesi ya tazara ambapo ilifika mahali meneja akashtakiwa kibinafsi.

Mwalimu, kwa wakati huu utakapokuwa unapambana na serikali huwezi kufa njaa, zipo shule nyingi zinakuhitaji (tena fizikia na kemia!).

Pole sana, hiyo ndiyo gharama ya DOMOcrasia ya Tanzania, lakini TUTASHINDA.
 
huo ni uhuni kama kawaida yao, ila viburi na jeuri siku zote umuumbua mwenye dharau, siku moja hata sisi tutawaosha for the sake of our children.:roll:
 
Na mimi nilisikia tu kwamba kama mfanyakazi wa serikalini unataka kuingia siasani basi unatakiwa kujiuzulu! Hilo kwangu siyo tatizo, ila kinachonisikitisha ni utekelezaji wa hilo tamkwo la waziri yan ni double standard, ninawagusa tu wale waliogombea kuwapinga CCM. Prof Baregu UD) kanyimwa mkataba, Prof. Mlambiti wa SUA nae kanyimwa mkataba! Hili halikubaliki, ni uonevu ila ukiwabana wanasema ni sheria ila ndo hivyo ya upande mmoja
 
sheria ya utumishi iko wazi wala haijafishwa, mtumishi wa umma anaweza kuwa mwanachama cha chama cha siasa lakini hatakiwi kugombea uongozi au kufanya kampeni za kisiasa lakini kwa upande wa vyombo vya dola hawatakiwi kabisa kuwa wanachama wa chama cha siasa isipokuwa kupiga kura tu.

kama kuna wanaCCM walikiuka sheria hii na bado wanafanya kazi, tupeane taarifa ili tutoe ushauri ili waondolewe kazini mara moja.
 
Wadau,
Kama mnavyofahamu kuna baadhi ya watumishi wa serikali walioamua kutumia haki yao ya kidemokrasia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika nchi yetu kwenye uchaguzi mkuu wa 2010.Wapo waliogombea kupitia ccm na wengine vyama vya upinzani.

Miongoni mwa wengi waliogombea kupitia vyama vya upinzani ni mwalimu Marwa Ryoba(Mwalimu wa shule ya sekondari Tarime) anayefundisha masomo ya sayansi (fizikia na kemia). Huyu bwana 'inasemekana" amefukuzwa kazi mara tu baada ya uchaguzi mkuu wa 2010 kwakuwa aligombea kupitia chama cha upinzani.

Binafsi nimeongea naye, ameniambia serikali imesitisha mshahara wake tangu mwezi novemba mwaka jana, pamoja na kwamba alirejea kazini kwake mara tu baada ya uchaguzi.Pamoja na juhudi alizofanya kutaka kujua sababu ya kusitishwa mshahara wake, hajapewa majibu ya kueleweka na wala hajapewa barua rasmi kumjulisha kama amefukuzwa kazi, ama kasimamishwa kazi ama kuna tatizo gani lililosababisha kufikiwa kwa uamuzi huo.

Kwakuwa hili jambo linaweza kuwa limewatokea watumishi wa umma wengi, kama ilivyomtokea Pro.Baregu mwaka juzi, nadhani kuna sababu za msingi hili jambo likawekwa wazi, kama ni muongozo wa utumishi wa umma uwekwe wazi ili kila mtu ajue.Ni jambo la ajabu kwamba mtumishi wa umma akiwania nafasi ya kisiasa kupitia ccm inakuwa halali lakini akifanya hivyo kupitia vyama vya upinzani inakuwa haramu.

Hii tabia ya serikali kuleta ubaguzi miongoni mwa watanzania inabidi tuipinge kwa nguvu zote. Ili kila mwananchi awe na uhuru wa kweli wa kushiriki zoezi la demokrasia pasipo na kificho wala wasiwasi.

Nawasilisha.

Huyu mwalimu ninamfahamu aisee kwa kweli inasikitisha.

Amekuwa akifundisha shule za vijijini ambako walimu wengi hawapendi kwenda. Nadhani aliamua kurudi nyumbani kwao serengeti kujaribu kuchangia maendeleo ya elimu kwa kufundisha huko vijijini kusikokalika na walimu wengi.

Baada ya kuhitimu shahada yake ya ualimu chuo kikuu kishiriki cha elimu mkwawa ndo akahamishiwa tarime secondary. Nafikiri hapo ccm wameamua kusitisha ajira yake kama kulipiza kisasi cha mwalimu huyu kumpa tabu sana mgombea wao wa ubunge ambaye alikuja kushinda ubunge baada ya kazi nzito sana. Hapa sijui demokrasia yetu inakwenda wapi.

Nadhani hapa ndipo panahitaji kuangaliwa kwa umakini, kwanini mtanzania mtumishi wa umma aonekane adui ama msaliti anapotumia haki yake ya kisiasa kupitia chama cha upinzani lakini inakuwa ni kheri na inakubalika kwa mwingine kutumia haki yake hiyo ya kisiasa kupitia ccm?
 
Mkataba ni tofauti sana na ajira. Prof Baregu hakufukuzwa katika ajira bali mkataba wake haukuongezwa jambo ambalo ni la hiari ya aliyetoa mkataba huo ( serikali) ama kuendelea na mkataba au la na ndio maana mkataba pia huvunjwa muda/wakati wowote.

Tusichanganye dawa katika hoja ya msingi, suala la mwalimu huyo halikuwa la mkataba hivyo lisifananishwe na la prof Baregu na hata sheria ya kuhitimisha ajira zao itakuwa tofauti
 
Nasikitika sana ila mwambie anitafute nimpe kazi na mshahara mzuri. Achana na serikali inayofilisika ya Kikwete. Kama anafundisha vizuri na nyanga ni nzuri basi anione
 
Kazi moja tu ni kuwaondoa kwenye utawala wa nchi. Hayo yote maovu mwasisi wake ni makamba, elimu ha
na ndiyo sababu ya majanga yanayokikumba ccm. Makamba ana miradi michafu kwa nchi, hatushangai uwezekano wa kupanga kuingiza nchi hii ktk machafuko.

Huyu mtu si muislam wala mkristo ni mpagani anaejificha kwenye maandiko ya kupapiapapia. Ni hatari mno,inaonekana ana mkakati maalum kuhusu mstakabali wa nchi hii.

Ikumbukwe kwamba RA ndiye rafiki yake mkubwa. Kila ccm inapopanga kumngoa kwa sababu zinazo eleweka ndani ya chama RA anaingilia kati. Kwa taarifa makamba bila RA si lolote wala chochote.

Hata uchawi una mwisho.
 
sheria ya utumishi iko wazi wala haijafishwa, mtumishi wa umma anaweza kuwa mwanachama cha chama cha siasa lakini hatakiwi kugombea uongozi au kufanya kampeni za kisiasa lakini kwa upande wa vyombo vya dola hawatakiwi kabisa kuwa wanachama wa chama cha siasa isipokuwa kupiga kura tu.

kama kuna wanaCCM walikiuka sheria hii na bado wanafanya kazi, tupeane taarifa ili tutoe ushauri ili waondolewe kazini mara moja.

Unasema kugombea Uongozi! Ni ngazi ipi hiyo?

Pale Morogoro kuna mtu alilalamika kuhusu mtu mmoja aitwaye Profesa Ishengoma, aliyekuwa diwani na baadaye kuchaguliwa Meya. mtu huyu aliendelea kulamba mshahara wa u-meya na bado SUA aliendelea kula mshahara.

Wakati hayo yakiendelea, Profesa Balegu akapigwa stop! Nasikia tena kwamba hapo hapo SUA sasa hivi kuna madiwani wawili na bado ni watumishi waandamizi wako ofisini kama kawaida.


Hebu tuelelweshe ni ngazi ipi ya uongozi.
 
Jamani saa ya Ukombozi imekaribia, tusikate tamaa maana katika mapambano haya tumeanza na hakuna kurudi nyuma na kama wote tukawa wa wazi watumishi wote pamoja na vyama vyao ni kama wanachama wa CDM kwa sababu popote pale unapopinga ufisadi na kudai haki yako unaonekana umetumwa na CDM. Hii ni hatua nzuri sana na tusirudi nyuma.

Maana sasa watayafungia baadhi ya NGOs eti kwa kushiriki kwenye siasa hasa kuunga mkono mapambao dhidi ya ufisadi, na kuelimisha watu.
CCM wanataka NGOs kama REDET na zile ambazo zinaegemea tu upande wao.

Peoples Power
 
Ulimuuliza kama alitoa taarifa kwa mwajili wake kama hatokuwepo katika kituo cha kazi wakati wa uchaguzi? Ama aliomba likizo ili aingie kwenye siasa? Kisha kurudi baada ya uchaguzi? Na kama alichukua likizo ni aina gani ya likizo aliyochukua?

Kibs, Asalam aleikum,
Alitoa taarifa kwa mwajiri wake, na ndio maana mara tu baada ya uchaguzi alirudi kwenye kituo chake cha kazi.
Kitu cha ajabu hapa ni kwamba hakupewa barua wala taarifa ya mdomo hata kutoka kwa mkuu wake wa shule kama kuna uamuzi fulani umefanywa dhidi yake, yeye aliendelea kutekeleza majukumu yake hadi mwisho wa mwezi ndipo alishangaa anakwenda kwenye atm akakuta hakuna kitu, katika kufuatilia suala hilo hadi mwezi wa december ndo akaambiwa serikali imesitisha mshahara wake. Hajaambiwa kama aidha kwa barua kama ulivyo utaratibu ama kwa mdomo kama amefukuzwa kazi au amesimamishwa kazi, kilichotokea ni kusitishwa mshahara wake, sasa hapo ndipo ameshindwa kuelewa kinachoendelea.
 
Back
Top Bottom