Informer
JF-Expert Member
- Jul 29, 2006
- 1,582
- 6,627
Imeandikwa na Kennedy Kisula, Liwale | Habari Leo | 04 Oktoba 2012
KATIBU wa CCM wa Uchumi aliyemaliza muda wake wilayani hapa, Said Lihomba alipoteza fahamu, wakati akihesabu kura zake juzi katika uchaguzi wa ndani wa CCM.
Lihomba alikumbwa na kadhia hiyo ndani ya chumba cha kuhesabia kura, baada ya kukataa kuchagua mwakilishi wa kumh esabia kura na kuamua kwenda mwenyewe.
Kabla ya kutokewa na hali hiyo, Msimamizi wa Uchaguzi huo, Farida Kikoleka aliwataka wagombea baada ya kupigwa kura, wateue wawakilishi au waende wao wenyewe kuhakikisha kura zao katika chumba cha kuhesabia.
Kauli hiyo ya Farida, ilisababisha wagombea wote, akiwamo Lihomba kwenda kuhakikisha kura zao zikihesabiwa. Wagombea wengine ni Mdai Mahela na Amidu Likwawatu.
Hata hivyo, wakati wakihakiki kura zao, Lihomba aliyekuwa akipata kura chache huku Likwawatu akiongoza kwa kura nyingi, alianguka ghafla.
Kutokana na hali hiyo, wasimamizi wa uchaguzi huo, Farida na Mathew Makwinywa waliamuru Lihomba atolewe katika chumba hicho na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Baada ya kumaliza kuhesabu, Farida alimtangaza Likwawatu kuwa mshindi wa nafasi hiyo baada ya kupata kura 58 na kufuatiwa na Mahela aliyepata kura 43 huku Lihomba aliyekuwa hospitalini akiambulia kura 10.
Wagombea wengine Katika nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya, Mohamed Ngomambo alishinda kwa kura 510 na kufuatiwa na Nasoro Kimbendela (130) na Halima Huki (19).
Mohamed Ndemane alichaguliwa ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kwa kura 420 na kuwashinda Jafari Musa aliyepata kura 218 na Abdalah Kitura aliyeambulia kura 49.
Uchaguzi Meatu Naye Kareny Masasy anaripoti kutoka Meatu, Simiyu kwamba Juma Mwibuli amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Wilaya kwa kuwashinda wenzake watatu waliokuwa wakiwania nafasi hiyo.
Msimamizi wa uchaguzi huo Jumanne Kisote ambaye ni Katibu wa CCM wa Wilaya ya Bariadi alisema kuwa wajumbe waliopiga kura walikuwa 1,174.
Alisema Mwibuli alipata kura 693 na kufuatiwa na Juma Kisija (379) na Emmanuel Masunga (92) huku 10 zikiharibika. Kwa ujumbe wa NEC aliyeibuka na ushindi ni Salum Khamis (997) akifuatiwa na Paul Guyashi (145), Kulwa Komanya (30) huku mbili zikiharibika.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa ni Zuhura Chiluba (766), Elius Shukia (640), Anjela Milembe (450), Christina Jisena (434) na Tito Masele (428).
KATIBU wa CCM wa Uchumi aliyemaliza muda wake wilayani hapa, Said Lihomba alipoteza fahamu, wakati akihesabu kura zake juzi katika uchaguzi wa ndani wa CCM.
Lihomba alikumbwa na kadhia hiyo ndani ya chumba cha kuhesabia kura, baada ya kukataa kuchagua mwakilishi wa kumh esabia kura na kuamua kwenda mwenyewe.
Kabla ya kutokewa na hali hiyo, Msimamizi wa Uchaguzi huo, Farida Kikoleka aliwataka wagombea baada ya kupigwa kura, wateue wawakilishi au waende wao wenyewe kuhakikisha kura zao katika chumba cha kuhesabia.
Kauli hiyo ya Farida, ilisababisha wagombea wote, akiwamo Lihomba kwenda kuhakikisha kura zao zikihesabiwa. Wagombea wengine ni Mdai Mahela na Amidu Likwawatu.
Hata hivyo, wakati wakihakiki kura zao, Lihomba aliyekuwa akipata kura chache huku Likwawatu akiongoza kwa kura nyingi, alianguka ghafla.
Kutokana na hali hiyo, wasimamizi wa uchaguzi huo, Farida na Mathew Makwinywa waliamuru Lihomba atolewe katika chumba hicho na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Baada ya kumaliza kuhesabu, Farida alimtangaza Likwawatu kuwa mshindi wa nafasi hiyo baada ya kupata kura 58 na kufuatiwa na Mahela aliyepata kura 43 huku Lihomba aliyekuwa hospitalini akiambulia kura 10.
Wagombea wengine Katika nafasi ya Mwenyekiti wa Wilaya, Mohamed Ngomambo alishinda kwa kura 510 na kufuatiwa na Nasoro Kimbendela (130) na Halima Huki (19).
Mohamed Ndemane alichaguliwa ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kwa kura 420 na kuwashinda Jafari Musa aliyepata kura 218 na Abdalah Kitura aliyeambulia kura 49.
Uchaguzi Meatu Naye Kareny Masasy anaripoti kutoka Meatu, Simiyu kwamba Juma Mwibuli amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Wilaya kwa kuwashinda wenzake watatu waliokuwa wakiwania nafasi hiyo.
Msimamizi wa uchaguzi huo Jumanne Kisote ambaye ni Katibu wa CCM wa Wilaya ya Bariadi alisema kuwa wajumbe waliopiga kura walikuwa 1,174.
Alisema Mwibuli alipata kura 693 na kufuatiwa na Juma Kisija (379) na Emmanuel Masunga (92) huku 10 zikiharibika. Kwa ujumbe wa NEC aliyeibuka na ushindi ni Salum Khamis (997) akifuatiwa na Paul Guyashi (145), Kulwa Komanya (30) huku mbili zikiharibika.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa ni Zuhura Chiluba (766), Elius Shukia (640), Anjela Milembe (450), Christina Jisena (434) na Tito Masele (428).