Mgao wa umeme, Mabomu ya Mbagala na Goms na Matokeo ya Kidato cha nne, CCM imechoka!

Ngandema Bwila

JF-Expert Member
Sep 8, 2010
1,017
256
kuna msemo usemao ukila na kipofu usimshike mkono. lakini kwa matokio haya imezihilisha si kwamba serikali ya CCM si tu kwamba ahadi zake kwa watanzania ni za hadaa bali pia uwezo wao umefika kikomo. Mwaka jana Ngeleja amenukuliwa akisema mgao utakuwa historia, lakini mgao ni kama kawa na ummeimarishwa kwa nguvu zaidi na kasi zaidi. Baada ya mabomu ya mbagala Mh.Husein Mwinyi alitamka tukio hilo halita tokea tena, Miaka 2 tumeona yaliyowapata watu wa Goms. Matokeo ya kitado cha nne 51 % zero. Wito wangu wanaharakati wote nchini, vyama vya siasa na wanataaluma wote tuwasaidie CCM waondoke madarakini. Hawawezi kujiondoa, wanajua hawezi tena kuongoza nchi lakini pia uwezo wa kuondoka madarakani wao wenyewe hawana. Shime tushirikiane tuwawezeshe kuondoka tuikomboe nchi yetu na majanga yatokanayo na uchovu wao wa kufikiri.
 
Back
Top Bottom