Lonestriker
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 640
- 241
Hatimaye jirani zetu wa Kenya nao watakumbwa na mgao wa umeme.Mgao wa Kenya unatokana na kampuni ya umeme ya kujipanga upya ili kuondokana na kampuni za kifisadi zilizopata tenda ya kuuza umeme.Kama ilivyo hapa kwetu,kampuni ya IPTL imetajwa na Kenya power kama moja ya kampuni tata ambazo zilipata tenda kifisadi.Hata hivyo tofauti na Tanzania,wenzetu mgao utaathiri viwanda zaidi.Viwanda vina uwezo wa kupata njia ya mbadala ya kupata nishati kutokana na uwezo wa kiuchumi ilhali watumiaji wadogo ni ngumu mno kupata njia mbadala.kwanini kampuni yetu isitumie njia hii kusaidia watumiaji wadogo hasa wa nyumbani...au tutaambiwa kuwa economy of scale hairuhusu?