n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
-Kuhakikisha wanapora mali za Watanzania walizozalisha na kuzifanya za familia.
-Kuhakikisha wanatoa elimu mbovu isiyomsaidia mtoto wa Kitanzania kuihoji Serekali.
-Kuhakikisha inabariki rushwa rohoni lakini mdomoni wanapiga vita na kukemea.
-Kuhakikisha inawaua waandishi wote wenye kutaka kuvuruga utawala wao wa kifisadi.
-Kuhakikisha Demokrasia Tanzania haipati nafasi kabisa.
-Kuhakikisha rasilimali za Tanzania zinanufaisha watoto wao tu.
-Kuhakikisha wanawagawa Watanzania kwa imani za kidini waendelee kutawala.
-Kuhakikisha wanawagawa Watanzania kwa imani za Kikabila waendelee kutawala.
-Kuhakikisha wanawagawa Watanzania Kikanda waendelee kutawala.
-Kuhakikisha wanakuwa na mfumo wa fedha chafu ziwasaidie kwenye chaguzi.
-Kuhakikisha kila muwekezaji anayewekeza Tanzania anaigia kwenye mfumo wao.
-Kuhakikisha Rais wa Tanzania anapatikana kwenye mfumo wao.
-Kuhakikisha kila Wizara inakuwa na kijana wao anayetokana na mtandao wao.
-Kuhakikisha Tanzania biashara zote kubwa ni mali yao.
-Kuhakikisha wanaua viwanda vyote kuwanyima Watanzania ajira.
-Kuhakikisha biashara zote za uagizaji bidhaa nje wanafanya wao.
-Kuhakikisha Watanzania wanazidi kuwa wajinga ndio maana wakaua elimu ya watu wazima.
-Kuhakikisha elimu ya uraia haitolewi Tanzania ili wasijue Mtandao wa utawala wa CCM
ONYO KWA WATANZANIA.
-CCM inatumia Udini ili kubakisha mtandao wa rushwa unabaki madarakani mwaka 2015.
-CCM imewaingiza watoto wao kwenye nafasi muhimu za chama kulinda mtandao wao.
-CCM inawatumia wawekezaji wakubwa kupata fedha za kuimarisha mtandao wao.
-CCM inawanyima watu kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015
-CCM inawanyima Watanzania elimu ya uraia ili kuimarisha mtandao wao.
-CCM inawaua waandishi wa habari wanaojaribu kuwaelemisha Watanzania.
-CCM inawatumia Polisi kuwatia hofu Watanzania kupata haki zao za msingi.
-CCM imeuza ardhi za Watanzania kwa wawekezaji ili kuwadhoofisha kiuchumi.
-CCM inatumia fedha chafu kuwapa rushwa Watanzania ili wabaki madarakani.
-CCM inafanya biashara ya mafuta, yakipungua bei yanafichwa.
TUFANYE NINI WATANZANIA
-Lazima tuwe na mshikamano bila kujali Dini zetu, kabila zetu, jinsia zetu na rangi zetu kuhakikisha haturuhusu Mtandao wa Mafisadi kufanya Tanzania ni koloni lao. Chukua fedha zao na piga kimya maana ni sehemu ya kodi yako unarudishiwa.
-Lazima kuishitaki Serekali nzima ya CCM na washirika wake kwenye Mahakama ya Kimataifa ICC kwa kuwaua Watanzania zaidi ya 24 bila hatia yoyote na kuvunja Makazi ya watu kwa ajili ya kuweka wawekezaji.
-Lazima kuishitaki Serekali nzima ya CCM na washirika wake kwa kuendekeza rushwa na kuifanya iwe ndio sala yao.
-Lazima kuishitaki Serekali ya CCM na washirika wake kwa kuua viwanga na mashirika ya umma na kujiuzia mali za Taifa kwa bei za kutupa. Angalia ulikotoka, au uklikozaliwa watu wanavyotaabika. Watanzania tuko tayari kutoa ushahidi kama Waliberia walivyotoa kwa CHARLES TAYLOR.
Waswahili walisema ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni anaweza fanana na ndugu yako, mjomba wako, au vinginevyo. Watanzania tusitumiwe na CCM katika Dini zetu, Kabila zetu ili kuendelea kuwaweka madarakani. Jiulize watu wana mabilioni wameficha ulaya, majumba ya kifahari, magari ya kifahari, mashamba, viwanda, makampuni je wewe Mmatengo, Msukuma, Mhaya, Mmakua, Mkerewe, Mdigo, Mzaramo, Mrangi, Mmbulu, Mmatumbi, Mpogoro, Mdengereko, Mchagga, Mpare, Msambaa, Mmwera, Mnyiramba, Mnyaturu, Muikizu, Mjita, Mha, Mholoholo, Mvinza, na wengine wengi kama mimi Mhaya tuna nini wametuwekezea CCM kwa ajili ya watoto wetu na wajukuu zetu kwa miaka 50. Mbaya kabisa wanamtania mtani wangu wanamwambia ukitaka mzigo ufike mpe Mnyamwezi.
Hivi kweli Watanzania tumekosa kabisa mtu wetu muaminifu kama Mwalimu Julius Kambara Nyerere wa kumuweka Ikulu. Hebu tuache udini, ukabila, ukanda, tufanye maamuzi sahihi. Dunia inatucheka, majirani zetu wanatucheka kwa utajiri tulio nao lakini hatuna mikakati ya kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi. Rwanda wamepigana vita leo hii wana mandege yanakuja mpaka Tanzania.
Kuanzia sasa mgeukie mwenzako alieko karibu nawe na mwambie acha Udini, acha ukabila, acha ukanda, acha kukumbatia rushwa na mafisadi wa CCM. Watanzania kwa pamoja tunaweza kuifanya Tanzania ikazaliwa upya. Nchi imeoza kwa utawala wa Kifisadi. Hivi mtoto wako akila chakula bila ridhaa yako mbona unamkanya. Mbona ndani ya CCM Wizi, rushwa, ubadhirifu, unyang'anyi, mauaji, uporaji, uhamishaji fedha za umma, udhalimu, vimetawala lakini mwenyekiti wao yuko kimya. Watanzania Tuchukueni tahadhari.
"TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA"
-Kuhakikisha wanatoa elimu mbovu isiyomsaidia mtoto wa Kitanzania kuihoji Serekali.
-Kuhakikisha inabariki rushwa rohoni lakini mdomoni wanapiga vita na kukemea.
-Kuhakikisha inawaua waandishi wote wenye kutaka kuvuruga utawala wao wa kifisadi.
-Kuhakikisha Demokrasia Tanzania haipati nafasi kabisa.
-Kuhakikisha rasilimali za Tanzania zinanufaisha watoto wao tu.
-Kuhakikisha wanawagawa Watanzania kwa imani za kidini waendelee kutawala.
-Kuhakikisha wanawagawa Watanzania kwa imani za Kikabila waendelee kutawala.
-Kuhakikisha wanawagawa Watanzania Kikanda waendelee kutawala.
-Kuhakikisha wanakuwa na mfumo wa fedha chafu ziwasaidie kwenye chaguzi.
-Kuhakikisha kila muwekezaji anayewekeza Tanzania anaigia kwenye mfumo wao.
-Kuhakikisha Rais wa Tanzania anapatikana kwenye mfumo wao.
-Kuhakikisha kila Wizara inakuwa na kijana wao anayetokana na mtandao wao.
-Kuhakikisha Tanzania biashara zote kubwa ni mali yao.
-Kuhakikisha wanaua viwanda vyote kuwanyima Watanzania ajira.
-Kuhakikisha biashara zote za uagizaji bidhaa nje wanafanya wao.
-Kuhakikisha Watanzania wanazidi kuwa wajinga ndio maana wakaua elimu ya watu wazima.
-Kuhakikisha elimu ya uraia haitolewi Tanzania ili wasijue Mtandao wa utawala wa CCM
ONYO KWA WATANZANIA.
-CCM inatumia Udini ili kubakisha mtandao wa rushwa unabaki madarakani mwaka 2015.
-CCM imewaingiza watoto wao kwenye nafasi muhimu za chama kulinda mtandao wao.
-CCM inawatumia wawekezaji wakubwa kupata fedha za kuimarisha mtandao wao.
-CCM inawanyima watu kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015
-CCM inawanyima Watanzania elimu ya uraia ili kuimarisha mtandao wao.
-CCM inawaua waandishi wa habari wanaojaribu kuwaelemisha Watanzania.
-CCM inawatumia Polisi kuwatia hofu Watanzania kupata haki zao za msingi.
-CCM imeuza ardhi za Watanzania kwa wawekezaji ili kuwadhoofisha kiuchumi.
-CCM inatumia fedha chafu kuwapa rushwa Watanzania ili wabaki madarakani.
-CCM inafanya biashara ya mafuta, yakipungua bei yanafichwa.
TUFANYE NINI WATANZANIA
-Lazima tuwe na mshikamano bila kujali Dini zetu, kabila zetu, jinsia zetu na rangi zetu kuhakikisha haturuhusu Mtandao wa Mafisadi kufanya Tanzania ni koloni lao. Chukua fedha zao na piga kimya maana ni sehemu ya kodi yako unarudishiwa.
-Lazima kuishitaki Serekali nzima ya CCM na washirika wake kwenye Mahakama ya Kimataifa ICC kwa kuwaua Watanzania zaidi ya 24 bila hatia yoyote na kuvunja Makazi ya watu kwa ajili ya kuweka wawekezaji.
-Lazima kuishitaki Serekali nzima ya CCM na washirika wake kwa kuendekeza rushwa na kuifanya iwe ndio sala yao.
-Lazima kuishitaki Serekali ya CCM na washirika wake kwa kuua viwanga na mashirika ya umma na kujiuzia mali za Taifa kwa bei za kutupa. Angalia ulikotoka, au uklikozaliwa watu wanavyotaabika. Watanzania tuko tayari kutoa ushahidi kama Waliberia walivyotoa kwa CHARLES TAYLOR.
Waswahili walisema ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni anaweza fanana na ndugu yako, mjomba wako, au vinginevyo. Watanzania tusitumiwe na CCM katika Dini zetu, Kabila zetu ili kuendelea kuwaweka madarakani. Jiulize watu wana mabilioni wameficha ulaya, majumba ya kifahari, magari ya kifahari, mashamba, viwanda, makampuni je wewe Mmatengo, Msukuma, Mhaya, Mmakua, Mkerewe, Mdigo, Mzaramo, Mrangi, Mmbulu, Mmatumbi, Mpogoro, Mdengereko, Mchagga, Mpare, Msambaa, Mmwera, Mnyiramba, Mnyaturu, Muikizu, Mjita, Mha, Mholoholo, Mvinza, na wengine wengi kama mimi Mhaya tuna nini wametuwekezea CCM kwa ajili ya watoto wetu na wajukuu zetu kwa miaka 50. Mbaya kabisa wanamtania mtani wangu wanamwambia ukitaka mzigo ufike mpe Mnyamwezi.
Hivi kweli Watanzania tumekosa kabisa mtu wetu muaminifu kama Mwalimu Julius Kambara Nyerere wa kumuweka Ikulu. Hebu tuache udini, ukabila, ukanda, tufanye maamuzi sahihi. Dunia inatucheka, majirani zetu wanatucheka kwa utajiri tulio nao lakini hatuna mikakati ya kuondoa Umasikini, Ujinga na Maradhi. Rwanda wamepigana vita leo hii wana mandege yanakuja mpaka Tanzania.
Kuanzia sasa mgeukie mwenzako alieko karibu nawe na mwambie acha Udini, acha ukabila, acha ukanda, acha kukumbatia rushwa na mafisadi wa CCM. Watanzania kwa pamoja tunaweza kuifanya Tanzania ikazaliwa upya. Nchi imeoza kwa utawala wa Kifisadi. Hivi mtoto wako akila chakula bila ridhaa yako mbona unamkanya. Mbona ndani ya CCM Wizi, rushwa, ubadhirifu, unyang'anyi, mauaji, uporaji, uhamishaji fedha za umma, udhalimu, vimetawala lakini mwenyekiti wao yuko kimya. Watanzania Tuchukueni tahadhari.
"TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA"