Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,827
- 12,009
Jeshi la Polisi limemkamata Gamariel Swai (43) mfanyabiashara na mkazi wa Mbezi kwa tuhuma za kuuza spea za magari zilizoibwa kwenye magari ya watu mbalimbali. Duka lake lipo Mtaa wa Songea, Ilala.
Awali, Jeshi la Polisi tarehe 23 Julai 2022 lilipokea taarifa ya wizi wa vifaa vya gari huko maeneo ya Kivule bombambili Ukonga ambapo Sifael Msemwa (38) mkazi wa Bombambili aliibiwa vifaa vya gari yake aliyokuwa ameiegesha nyumbani kwake aina ya Toyota Prado yenye usajili namba. T. 429 BKK ambavyo ni side mirror 03, power window 04, control box na betri la gari.
Tarehe 15 Agosti 2022 baada ya upelelezi alikamatwa mtuhumiwa Gama Swai na katika upekuzi katika duka lake Namba 21 lililopo mtaa wa Songea, Ilala alikutwa na side mirror 02 na power window 04 zilizoibwa toka katika gari hilo Toyota Prado.
Aidha vilikamatwa vifaa vingine mbalimbali vya magari dukani hapo vinavyodhaniwa kuwa ni vya wizi kutokana na kutokuwepo na maelezo ya kutosha kuhusiana na vifaa hivyo. Vitu vilivyokamatwa ni .
Taa za mbele 93 za magari ya aina mbalimbali, taa za nyuma 130 za magari ya aina mbalimbali, power window 189 za magari ya aina mbalimbali, side mirror 62 za magari ya aina mbalimbali, show za mbele za magari 07 mbalimbali, show za ndani za magari 35 za aina mbalimbali, mikono ya milango (vitasa) 26 za magari, rejeta 01 na betri moja.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na oparasheni kali dhidi watu wanajihusisha na matukio ya kihalifu ikiwa ni pamoja wizi wa magari na uuzaji wa vifaa vya magari vitokanavyo na magari ya wizi.
Awali, Jeshi la Polisi tarehe 23 Julai 2022 lilipokea taarifa ya wizi wa vifaa vya gari huko maeneo ya Kivule bombambili Ukonga ambapo Sifael Msemwa (38) mkazi wa Bombambili aliibiwa vifaa vya gari yake aliyokuwa ameiegesha nyumbani kwake aina ya Toyota Prado yenye usajili namba. T. 429 BKK ambavyo ni side mirror 03, power window 04, control box na betri la gari.
Tarehe 15 Agosti 2022 baada ya upelelezi alikamatwa mtuhumiwa Gama Swai na katika upekuzi katika duka lake Namba 21 lililopo mtaa wa Songea, Ilala alikutwa na side mirror 02 na power window 04 zilizoibwa toka katika gari hilo Toyota Prado.
Aidha vilikamatwa vifaa vingine mbalimbali vya magari dukani hapo vinavyodhaniwa kuwa ni vya wizi kutokana na kutokuwepo na maelezo ya kutosha kuhusiana na vifaa hivyo. Vitu vilivyokamatwa ni .
Taa za mbele 93 za magari ya aina mbalimbali, taa za nyuma 130 za magari ya aina mbalimbali, power window 189 za magari ya aina mbalimbali, side mirror 62 za magari ya aina mbalimbali, show za mbele za magari 07 mbalimbali, show za ndani za magari 35 za aina mbalimbali, mikono ya milango (vitasa) 26 za magari, rejeta 01 na betri moja.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na oparasheni kali dhidi watu wanajihusisha na matukio ya kihalifu ikiwa ni pamoja wizi wa magari na uuzaji wa vifaa vya magari vitokanavyo na magari ya wizi.