Meya adai fidia ya Sh100 mil kwa kudhalilishwa na mbunge wa CHADEMA (Mch. Peter Msigwa)

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,573
lissu.jpg

Wakili wa mlalamikiwa mbunge wa Iringa , Tundu Lisu ameshindwa kuhudhuria mahakamani hivyo , ameomba shauri hilo lisikilizwe kwa njia ya maandishi uamuzi uliokubaliwa. maandishi,Lisu awasilishe ushahidi wake Machi 26,mwaka huu,upande wa mlalamikiwa ujibu Aprili 9,maelezo ya awamu ya pili Aprili 16 na Aprili 30 uamuzi." Waziri Mkuu, Mizengo Pinda

Iringa. Meya wa Manispaa ya Iringa,Aman Mwamwindi amemfungulia kesi ya madai Mbunge wa Jimbo la Iringa, Mchungaji Peter Msigwa akidai fidia ya Sh100 milioni na kuombwa radhi kwa njia ya maandishi .

Kesi hiyo inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Mwandimizi Mfawidhi wa Mahakama Mkoa wa Iringa, Juma Hassan imefunguliwa mahakamani hapo Desemba 20,mwaka jana katika Mahakama ya Wilaya ya Iringa.
Ilidaiwa mahakamani hapo jana kuwa, mlalamikiwa akiwa na nia mbaya dhidi ya mlalamikaji alitamka maneno ya kashfa mbele ya umati wa watu huku akijua kuwa maneno yote ni ya uongo na yamelenga kumharibia sifa.

Pia mahakama hiyo jana ilikubali ombi la upande wa mlalamikiwa la kutaka pingamizi la kesi hiyo ya madai inayomkabili mbunge wa jimbo hilo kusilikizwa kwa njia ya maandishi ambapo ilipangwa Aprili 30,mwaka huu kuwa siku ya kutoa uamuzi wa pingamizi hilo.

Machi 26,mwaka huu upande wa mlalamikiwa unatakiwa ujibu na Aprili 9, maelezo ya awamu ya pili yanatakiwa kuwasilishwa .
 
katika ukoo wao wameshawahi kumiliki kiasi hicho cha pesa au ni ukuzi tu......jinga.
 
Masisiem bhana pesa zoooote za meno ya tembo na madili kibao na ma10% bado haziwatoshi mnadai mlipwe na mafidia thru mahakama zenu???hivi nyie mtaishi milele mkiwanyanyasa watanganyika hivi kweli???
Time will tell...
 
Milioni Mia? Anyway labda kwa vile hakuna ajue thamani ya utu, kwani hata kama ukilipwa bilioni 1000 inafanana na utu wako? Ushauri wa bure kwa wanasiasa wetu, heshimianeni na msikomoane!!
 
Atajipangiaje?thamani ya mtatusi ni m100?sasa hapati hata robo ya robo kwani kuambiwa ukweli ndio kutukanwa?hakimu atakae toa uwamzi wakulipwa pesa huyo mnyalukolo ntamshangaa sana na tunataka uhuru wa mahakama nasio kuteuwana tumechoka chadema andaeni maandamano nch nzima ya kumtoa huyu fedhuri alieko ikulu.tupeane namba za sim vijiji kwa kiji kata kwa kata ili kila atakae amka aungane nawenzie wa sehemu nyingine ili tukusanyike mjini nakazi zisifanyike na wakituchokoza tu tupachimbe wakose wakumtawala.inauma sana mi nishachoka bora kufa tu
 
Anazitaka kiulaini kupitia mahakama, namshauri afanye kazi atazipata
 
kwanza huyu mlalamikaji si ni mtoto wa mzee mwamwindi yule muuaji wa dr. Kleruu aliyekuwa mkuu wa mkoa?
 
Back
Top Bottom