Salman Rushdie alimdhulumu nani?
Kwani mapadri wanavaa nini au shimizi?
Mkuu naheshimu sana michango yako...
Na mimi pia Mkuu.
Chanzo cha habari yako ni kipi??
Hata hivyo kwenye uislam HAKUNA KITU KINACHOITWA ALBADILI AU DUA YA ALBADILI
ETI UMSOMEEE MTU AGEUKE CHIZI AU AFE,,HUO NI UHUNI NA USHIRIKINA KAMA ULIVYO USHIRIKINA MWINGINE TUH
UISLAM NI DINI SAFI ISIYOAMIN NGUVU YA UCHAWI WALA MASHETANI
Sasa "jihad"huwa za nini kung'ang'ania mabomu ya west wakati kumbe hii kitu ipo "albadir"_msomeeni obama+netanyahu
View attachment 214123View attachment 214124SHEIKH Maarufu jijini Dar es Salaam na nchini, Ali Bassaleh ametishia kusoma kisomo (albadiri) dhidi ya mfanyibiashara maarufu nchini Reginald Mengi iwapo hatalipwa fidia anayodai.
Sheikh Bassaleh amemfahamisha Mwandishi wiki hii kwamba, amefanya subira ya muda mrefu hivyo ameona wakati umefika kwa yeye kumlilia Mwenyezi Mungu (SW) dhidi ya dhuluma aliyodai kuwa imefanywa na mfanyabishara huyo.
Amesema anakusudia kusoma kisomo hicho muda wowote na atatangaza siku maalum kwa waumini wa dini ya kiislamu na watanzania kwa ujumla.
Amesema, madai ya fedha dhidi ya Reginald Mengi yanafuatia kumalizika kwa kesi ya kashfa dhidi ya chombo cha habari kinachomilikiwa na moja ya makampuni ambayo Mengi ana hisa.
Amesema, kufuatia kukashifiwa na chombo hicho cha habari, aliwasilisha malalamiko yake Baraza la habari ambako alishinda na kupewa ruhusa ya kwenda mahakamani.
"Nilimtumia Wakili Profesa Saffari, nikafungua madai, tukashinda kesi, chombo hicho na mmiliki wake wametakiwa kunilipa fidia ya shilingi Milioni 49", ameeleza Sheikh
Amesema, tangu wakati huo amekuwa akisumbuliwa, hali inayoashiria mwenye fedha ndiye mwenye haki ambaye hata vyombo vya sheria vinaashiria kutokuwa tayari kukunjua makucha dhidi yake.
Akizungumzia kisomo cha Albadiri Sheikh Bassaleh amesema, ni dua maalum, yenye utekelezaji maalum wa maombi ya mdhulumiwa ambayo huelekezwa kwa Muumba wa Mbingu na Ardhi, Mmiliki wa vyote, ambaye ndiye Mmiliki wa uhai wa Mwanadaamu, huweza kuuchukua wakati wowote atakapo.
Amesema katika mafunzo ya dini ya kiislamu, Dua ya mdhulumiwa inapoombwa kinyenyekevu haina pazia, hupokelewa moja kwa moja na kwa haraka na Mwenyezi Mungu dhidi ya aliyedhulumu na kwamba zipo aina tofauti za kujibiwa.
Miongoni mwa majibu ya Mwenyezi Mungu kwa dua hiyo ni pamoja na kuondosha uhai wa aliyedhulumu ili asiendelee kukera waja wema wanyonge au kumpa maradhi yasiyotibika kwa dawa za Hospitali wala mitishamba ili iwe ujumbe wa wazi kwa wengine.
Majibu mengine ni pamoja na kumpa aliyedhulumiwa nafasi ya juu ili kumfedhehesha aliyedhulumu au mbadala mwingine ulio bora zaidi kuchukua nafasi ya alichodhulumiwa kama mali, wasifu au heshima katika jamii.
Katika madai yake dhidi ya taarifa iliyochapishwa na chombo kinachosemekana kumilikiwa na Mengi ni kwamba, ilichapishwa taarifa yenye kumkashifu na kumshushia hadhi na heshima yake kama kiongozi wa Dini na jamii kwa ujumla.
Hata hivyo, baadhi ya watu wameendelea kumsihi Sheikh Bassaleh asichukue hatua hiyo kwa haraka kutokana na madhara yake kuto komea kwa mtu mmoja bali huusisha mlolongo wa watu wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine.
Albadiri ni faraja kwa wajinga tu.
Labda mseme mtamlipua kwa suicide bomber.
Kama albadiri inafanya kazi wanisomee mimi niliyesema mungu hayupo.
Frankly speaking when it comes to the issue of God Kiranga you make me sick!
Ulijiumba mwenyewe?