alsaidy
JF-Expert Member
- Feb 23, 2009
- 334
- 88
Ndugu yangu hebu acha kumuonea mzanzibari mwenzangu...
hilo sekeseke ni wengi tulilishuhudia, wengine walikuwepo uwanjani na wengine kupitia runinga.
kwanza hayo maneno ya kipumbavu ni yepi? unaweza kuya-quote hayo maneno?
Mie nilikuwa nimekaa upande wa orange straight kulia kwa jukwaa kuu na hilo tukio nililishuhudia.
Abdulhalim hakumfanyia chochote kibaya Aruna Dindane, isipokuwa Dindane ndiye alionyesha dharau kwa abdulhalim. Na kama unakumbuka vizuri abdulhalim ndiye alimfuata Dindane kumpa mkono na kuyamaliza kutokana na purukushani iliyokuwa imetokea hapo kabla. Sasa unadai afundishwe adabu ipi?
baada ya dindane kuonyesha kumpandishia na kumsukuma ndipo jamaa nae akawa anakomaa nae, isingekuwa rahisi katika hali ile wenyewe wayamalize bila mtu mwingine kuingilia kati na ndio sabau ya refa kuingilia kati kuwatenganisha, so usimlaumu bure kijana wa watu hakufanya jambo lolote baya la kufaa kufundishwa adabu, labda utafute jambo lingine.
au unataka kumfagilia maximo kiujanja ujanja?
Uko sahihi Mwita nilikuwa na mawazo kama ya kwako nilichoelewa mimi Abdulhalim alimfuata jamaa wamalizane kwa kuwa ndio mpira ulivyo. Lakini jamaa ndio akaanza kumaindi.
Inawezekana jana ana mapungufu kidogo kwenye nidhamu na anatakiwa ajirekebishe ila binafsi nimemkubali ana kiwango cha holding midfielder!!