Mchakato wa kisheria wa kubadili jina lako

Voice of Wisdom

JF-Expert Member
Oct 4, 2011
537
240
Heshima zenu wakuu, na poleni na majukumu ya wiki nzima.

Kuna jambo naomba kujuzwa kuhusu kubadili jina. Hii inatokana na ukweli huu "nilipokuwa std 4 tz nilihamishiwa shule huko kenya ambapo nilisoma miaka miwili ( std 4 &5) kisha nikarudi tz, ile shule niliyokuwa mwanzoni nikakuta jina langu kuna mtu analitumia naye yupo std 7. Nikahamia shule ya jirani mwalimu mkuu akanipa jina la mwanafunzi mwingine ambaye alirudia std 6 nikawa nalitumia hadi sasa nipo chuo mwaka wa 2.

Kuna tetesi nimepata kwamba mtu unaweza kubadili jina. Wajuzi naomba mnijuze, je ni hatua gani natakiwa kuzifuata na je inagharimu fedha yeyote?

Nawasilisha.
=====================
Nawasalimu Wana Jukwaa La Sheria na Wanachama wote wenzangu wa Jamiiforum!!
Zaidi Sana,niwape pole na Shughuli za Kujenga Taifa!!

Naomba nieleze kwa Muhtasari tatizo Langu halafu nisikie kutoka kwenu Kuhusu namna gani Mnaweza Kunishauri maana Peke Yangu nahisi kuishiwa Hekima Kuhusu namna gani niendee Changamoto hii!!

Mm nilimaliza Elimu ya Msingi katika Shule ya Serikali Mwaka 1997 na nikajiunga na Sekondari ya Serikali Mwaka 1998-2001,Mwaka 2002-2004 nikamaliza Kidato cha Sita,Katika hatua zote hizo nilimaliza kwa Matokeo Mazuri tu!!
Tatizo Langu ni Jina,Jina Langu La kwanza ni La Kiislamu na La Pili ni La Kikristo(Yaani Jina La Baba Yangu) Hii imetokana na Mama Yangu Kuwa Muislamu ambaye Kimsingi ndiye aliyenilea na Kunisomesha na Baba Yangu ni Mkristo!!
Sikupenda kuwa na Jina Moja La Imani hii na Lingine La Imani ile na kwa sababu hiyo Mwaka 2005(Mwaka mmoja baada ya Kumaliza kidato cha Sita) nikabadilisha Jina Langu la Kwanza kwa taratibu zote za Kisheria nikapewa Document inayoelezea Kubadilisha kwangu Jina Kisheria inaitwa Deed Poll!!


Kwa Kutumia Deed Poll nikaweza Kubadilisha Jina hadi kwenye Pasi yangu ya Kusafiria,kwenye Mchakato wa Kitambulisho cha Kupigia Kura nikaweka Jina Langu Jipya na hata Kwenye Mchakato wa Kitambulisho cha Taifa.

Shida ni kwamba Mwaka Huu nimeazimia Kuingia Chuo Kikuu na nilipokwenda Mlimani Kuulizia nilipata wakati Mgumu sana,Academic Certificate ni Msaafu hapa Tanzania,hauwezi Kubadilishwa asilani!!
Chuo kimesema kama nikitaka Kusoma nitatumia Majina yaleyale yanayo-appear kwenye Vyeti vyangu Vya O'level na A'level vinginevyo imekula kwangu,Sasa nikawauliza Kwa nini Sheria Mama iruhusu kubadili Jina Halafu taratibu za Chuo tu zikatae? Kwamba Taratibu za Chuo ni Kuu Kuliko Sheria za Nchi maana Deed Poll ni Nyaraka ya Kisheria na Utaratibu wote wa Kisheria Umefuatwa,Pamoja na Hoja zote nilizojaribu Kuzijenga Dean of Students wa Shule ya Biashara hakunielewa,Akasema HAIWEZEKANI!!

Nina Imani kubwa na Jf,Najua Wadau wengi hapa Wana Fikra Pevu,nitafanyaje kujinasua kwenye kadhia hii,Ninawezaje kwenda Chuo kwa Jina Langu Jipya maana hata NECTA niwapigia Simu Majibu ni hayohayo,hawawezi Kubadili Jina kwenye Cheti!!

Neno hili Limekuwa Kubwa kwangu nami kwa Unyenyekevu Mkubwa ninalileta kwenu!!
Ninatanguliza Shukrani!!
=====================
Habari wana JF?

Mimi ni mzima wa afya tele namshukuru Mungu kwa pumzi na afya na kila ki2(all is well) hope mko pouwa, back 2 the topic! Mimi kwa jina naitwa Frank Shedrack na nimwanafunzi kwa sasa, wakuu naomba mwongozo na ushauri kuhusu kubadili jina, I declare kuwa silipendi jina langu (Frank) na niwe wazi kuwa mimi sio muumini wa majina ya kigeni, nawaombeni ushauri na mwongozo jinsi ya kubadili Jina ambalo pia lipo kwenye cheti cha kuzaliwa na taaluma.

Kiukweli katika hili sijui nianzie wapi, mwenye ufahamu kuhusu hili naomba anisaidie. I real hate my name so please help me.

ALL IS WELL....
======================
Wadau,

Jina la ukoo mimi natumia jina la baba wa kambo, tangu shule mpaka sasa niko kwenye ajira. Makosa yalifanyika mwanzo kabisa tangu niko mdogo.

Ni hadithi ndefu sitoweza kueleza hapa, kwa sasa inawezekana kubadilisha? Na kuhusu nyaraka je?
=======================
Habari wa JF!

Kuna ndugu yangu anataka kubadili jina lakini yeye toka darasa la kwanza mpka chuo kikuu anatumia jina aliyo sawa kwenye vyeti vyake.

Sasa swali ni hivi, je, akibadili jina sasa hivi halitamsumbua wakati wa kutafuta kazi na kadhalika, yeye ndo amemaliza chuo kikuu mwezi uliopita.
==========================
==========================

Ni kazi rahisi sana na haina gharama ya kutisha.

Nenda kwa lawyer yoyote wa karibu yako.

Atakuchapia barua moja inaitwa "change of name deeds" au wakati mwingine inaitwa (deed pol) ambayo itaonyesha jina lako la zamani na jina lako jipya.

Na huwenda akakuuliza sababu ya kubadili jina. Na hio uliotoa ni sababu tosha. Hakikisha hio barua mnasaini wote, yaani wewe na huyo lawyer.

Gharama za hio barua isizidi shs 50,000/= Na lazima akupe original copy kama tano.

Uli moja iende kwenye passport na zingine utapeleka kazini kwako . Na zingine benki kama una account. Na zingine unaweka kwa ajili ya ushahidi.

Good luck.

 
wewe sema tuu ulirudia la saba,ili ufaulu!inawezekana,unaenda kuapa mahakamani,unapata certificate pia ya change of name!ila useme jina ni la kwako unataka kubadili,ukisema ulichukua la mtu utazua soo
 
wewe sema tuu ulirudia la saba,ili ufaulu!inawezekana,unaenda kuapa mahakamani,unapata certificate pia ya change of name!ila useme jina ni la kwako unataka kubadili,ukisema ulichukua la mtu utazua soo

nashukuru mkuu kwa ushauri. Kwa kifupi cjawah kurudia darasa since nimeanza vidudu. Huku nitasema kama ulivyonieleza, hapa nimekuwa mtupu ili nipate msaada
 
sasa wataka uwe na jina gani? la kwako asili ama upate jipya?
na je hilo unalolitumia una cheti chake??
kama huna cheti cha jina unalolitumia sasa waweza pata cheti cha kuzaliwa kirahisi tu,na ukaendelea kutambuliwa kwa jina hilo,lakini kama wataka kujulikana kwa majina yote basi itabidi uende mahakamani ukaape na kupata kitu kinaitwa DEED POOL ili kukutambua kuwa wa zamani ndo wewe.
sijui kama umenipata hapo
 
sasa wataka uwe na jina gani? la kwako asili ama upate jipya?
na je hilo unalolitumia una cheti chake??
kama huna cheti cha jina unalolitumia sasa waweza pata cheti cha kuzaliwa kirahisi tu,na ukaendelea kutambuliwa kwa jina hilo,lakini kama wataka kujulikana kwa majina yote basi itabidi uende mahakamani ukaape na kupata kitu kinaitwa DEED POOL ili kukutambua kuwa wa zamani ndo wewe.
sijui kama umenipata hapo

mkuu shukrani, lengo langu ni kutaka kutumia jina langu la asili.
cheti cha kuzaliwa chenye jina ninalotumia sasa ninacho pia
 
so una vyeti viwili vya kuzaliwa vyenye majina tafauti?
Cheti cha asili tena usikitumie nenda kaape tu mahakamani upate DEED POLL ON CHANGE OF NAME coz uta renounce and abandon the use of current name na utataja jina utakalotaka utambulike,
gharama itategemea coz hilo kwa mahakama ni dili waweza ukakaa kwenye benchi ukaletewa tu ukitoa chchote kitu,bt ukitaka haki utajuta kujaribu coz utasumbuliwa tu.
 
Kwa kiswahili ni sawa kusema kubadili jina.

Nenda kwa Wakili mueleze hiyo maneno not necessary the whole stori, ila mwambie tu hilo jina ulisomea na sas unahitaji kutumia majina yako uliyopewa either kwa kubatizwa kama wewe ni mtristo au ulipozaliwa.

atukutengenezea document inaitwa DEED POLL on change of names utaapa utaipeleka kuisajili kwa msajili wa hati then baada yapo peleka kwenye chuo unachosoma, benki, na sehemu zote ambazo una kitambulisho chenye jina la zamani watakubadilishia majina yako utapata kitambulisho kipya na kuanzia hapo document zako zote zitasomeka kwa majina yako mapya.
 
Nawasalimu Wana Jukwaa La Sheria na Wanachama wote wenzangu wa Jamiiforum!!
Zaidi Sana,niwape pole na Shughuli za Kujenga Taifa!!

Naomba nieleze kwa Muhtasari tatizo Langu halafu nisikie kutoka kwenu Kuhusu namna gani Mnaweza Kunishauri maana Peke Yangu nahisi kuishiwa Hekima Kuhusu namna gani niendee Changamoto hii!!

Mm nilimaliza Elimu ya Msingi katika Shule ya Serikali Mwaka 1997 na nikajiunga na Sekondari ya Serikali Mwaka 1998-2001,Mwaka 2002-2004 nikamaliza Kidato cha Sita,Katika hatua zote hizo nilimaliza kwa Matokeo Mazuri tu!!
Tatizo Langu ni Jina,Jina Langu La kwanza ni La Kiislamu na La Pili ni La Kikristo(Yaani Jina La Baba Yangu) Hii imetokana na Mama Yangu Kuwa Muislamu ambaye Kimsingi ndiye aliyenilea na Kunisomesha na Baba Yangu ni Mkristo!!
Sikupenda kuwa na Jina Moja La Imani hii na Lingine La Imani ile na kwa sababu hiyo Mwaka 2005(Mwaka mmoja baada ya Kumaliza kidato cha Sita) nikabadilisha Jina Langu la Kwanza kwa taratibu zote za Kisheria nikapewa Document inayoelezea Kubadilisha kwangu Jina Kisheria inaitwa Deed Poll!!


Kwa Kutumia Deed Poll nikaweza Kubadilisha Jina hadi kwenye Pasi yangu ya Kusafiria,kwenye Mchakato wa Kitambulisho cha Kupigia Kura nikaweka Jina Langu Jipya na hata Kwenye Mchakato wa Kitambulisho cha Taifa.

Shida ni kwamba Mwaka Huu nimeazimia Kuingia Chuo Kikuu na nilipokwenda Mlimani Kuulizia nilipata wakati Mgumu sana,Academic Certificate ni Msaafu hapa Tanzania,hauwezi Kubadilishwa asilani!!
Chuo kimesema kama nikitaka Kusoma nitatumia Majina yaleyale yanayo-appear kwenye Vyeti vyangu Vya O'level na A'level vinginevyo imekula kwangu,Sasa nikawauliza Kwa nini Sheria Mama iruhusu kubadili Jina Halafu taratibu za Chuo tu zikatae? Kwamba Taratibu za Chuo ni Kuu Kuliko Sheria za Nchi maana Deed Poll ni Nyaraka ya Kisheria na Utaratibu wote wa Kisheria Umefuatwa,Pamoja na Hoja zote nilizojaribu Kuzijenga Dean of Students wa Shule ya Biashara hakunielewa,Akasema HAIWEZEKANI!!

Nina Imani kubwa na Jf,Najua Wadau wengi hapa Wana Fikra Pevu,nitafanyaje kujinasua kwenye kadhia hii,Ninawezaje kwenda Chuo kwa Jina Langu Jipya maana hata NECTA niwapigia Simu Majibu ni hayohayo,hawawezi Kubadili Jina kwenye Cheti!!

Neno hili Limekuwa Kubwa kwangu nami kwa Unyenyekevu Mkubwa ninalileta kwenu!!
Ninatanguliza Shukrani!!
 
Dah mkuu hii ishu yako kwa TANZANIA hii ni nzito sana...Huwezi kubadili majina ya vyeti vya elimu na hata kupata vyeti vya pili ni kazi vile vile... Chuoni hawana kosa kwani wanatakiwa wafuate majina yaliyomo kwenye vyeti na wana operate between nationa and international laws.... Sidhani kama suala lako linawzekana kwani hata kwenye ajira ni tabu tupu......
 
Dah mkuu hii ishu yako kwa TANZANIA hii ni nzito sana...Huwezi kubadili majina ya vyeti vya elimu na hata kupata vyeti vya pili ni kazi vile vile... Chuoni hawana kosa kwani wanatakiwa wafuate majina yaliyomo kwenye vyeti na wana operate between nationa and international laws.... Sidhani kama suala lako linawzekana kwani hata kwenye ajira ni tabu tupu......


Asante Asigwa,Nimekusikia Mkuu wangu,Asante kwa Kuchukua Muda wako na Kuniandikia!!
 
Usiwalaumu chuo cz uli apply kw vyeti vyenye majina tofauti na admission zao zinafuata application names. Deed poll itabaki kuonyesha ulibadili majina lakini academic certificate haziwez kubadilishwa na hii ni salama kw future yko utapoenda kuomba kaz na vyet vyenye majina manne matano tofauti matter una deed poll na affidavit bdo kw mwajiri itamjengea hali ya was was na hawa watu hawana mda wa kuanza kukuchunguza in detail while kuna watu wengne mamia waeomba kaz hyo hyo na wanavigezo. Endelea na majina yko ya zaman kwenye vyeti ila deed poll itengenezee affidavit
 
Pole sana mkuu, ulipaswa kufanya hivyo mapema kabla ujajisajili kwajili ya mitihani ya kidato cha pili. Tatizo la sheria za nchi yetu ni kama zinapingana. Umenikumbusha mbali sana nilisha teseka sana kwa tatizo kama lako kipindi cha nyuma. POLE MKUU
 
Pole sana mkuu, ulipaswa
kufanya hivyo mapema kabla ujajisajili kwajili ya mitihani ya kidato cha
pili. Tatizo la sheria za nchi yetu ni kama zinapingana. Umenikumbusha
mbali sana nilisha teseka sana kwa tatizo kama lako kipindi cha nyuma.
POLE MKUU

Mkuu,msaidie sasa,wakati ndio huu,ulilitatua vipi hilo tatizo lako ili naye apate mwangaza,ndiyo uzuri wa JF kaka,kusaidiana na kufaana hata kama hatufahamiani
 
pole sana mkuu,
ila kubadilsha jina kisa dini mimi kwangu naona haina faida! kwani kama ulkua unaitwa Mohamed John na sasa unaitwa Mohamed Hassan inakuongezea nini? Jina ni jna tu hata waweza itwa Dunia, Meza, Ngengemkeni, Bahari n.k na likawa jina lako!
Ushauri - Rudia jina lako la awali halafu acha udini
 
Kaka nakushauri hivi, usiangaike na majina ya kwenye vyeti vyako, ya kaisari mpe kaisari na ya Mungu mpe Mungu,endelea kutumia majina hayohayo kazn , alafu uchague mwenyewe kati ya hizo din 2 ni ip itakufaa ndipo uende kwenye din husika ubadilishe jina kulingana na inavyopaswa, hivyo kazn utatumia majna yale2 ya mwanzo lkn katka imani unakuwa tayar unamajina yako, lengo c ni kwenda ahela tu...eee kaka nawasilisha
 
Back
Top Bottom