Nashukuru Bulesi; Sina fikra za kutafuta uongozi wa kisiasa na hata kama fikra zitabadilika, kwa fikra zangu, jina langu litakatwa mapema sana na wanalumumba kwani wanawaita watanzania wenye kuangalia zaidi maslahi ya taifa kwamba "sio wenzao";
Naamini kwamba njia za kusaidia kutetea wananchi zipo nyingi, sio lazima iwe kupitia nafasi ya uongozi;ni kwa njia hizo nitakuwa nyuma ya mgombea yoyote ambae wana rungwe watamwona anatosha bila ya kujalisha anatokea chama gani cha siasa;
Vinginevyo wana rungwe wameumizwa sana na siasa za ccm, wakifanya maamuzi ya kuachana nayo 2015, itakuwa ni haki yao;
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Ni kweli kabisa kuwa iwapo utaomba ubunge kwa kupitia chama tawala jina lako litakatwa kwani hao jamaa wanawaogopa wasomi kuwa watawayumbisha na ndio maana nikakushauri kwamba in the event you have a change of heart and decide to run , you stand a better chance of winning through Chadema kwasababu ni chama cha wasomi na welewa wa mambo!!! Moreover ukiwa mgombea wa Chadema huna haja ya kutumia pesa ili uchaguliwe kama wafanyavyo huko ccm; ccm bila pesa hupiti hata ujumbe wa nyumba kumi!!!