Malafyale
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 13,813
- 11,126
MBUNGE wa Viti Maalumu wa CUF, Clara Mwatuka, amejitolea kusomesha kidato cha kwanza hadi cha nne watoto 20 kutoka kata 34 za wilayani hapa kuanzia mwaka huu.
Kwa kata hizo 34 za wilaya ya Masasi, inamaanisha kwamba, mbunge huyo atasomesha wanafunzi 680.
Ada ya kila mtoto kwa shule ya Serikali ni Sh 20,000, hali ambayo itamfanya mbunge huyo kulipa zaidi ya Sh milioni 13.6 kwa mwaka.
Mbunge huyo aliyewania ubunge wa Masasi, lakini kura zake hazikutosha mbele ya Mariam Kasembe wa CCM, ameingia bungeni baada ya CUF kumteua, akiwa mbunge pekee wa kuteuliwa kutoka Kanda ya Kusini.
Akizungumza na HABARILEO Jumapili kijijini kwake Nanganga, wilayani hapa jana, alisema dhamira yake ni kuziba pengo baina ya matajiri na masikini na hilo litawezekana iwapo watoto wa masikini watawezeshwa kupata elimu na kwa kuanzia atasomesha watoto 680 kwa wilaya nzima.
Nimetoa maelekezo kwa watendaji wa kata kuleta majina ya watoto 20 waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwakani, ambao wazazi wao hawana uwezo katika wilaya yetu kuna kata 34, hivyo jumla ya wanafunzi wote watakuwa 680, alisema Mwatuka.
Aliongeza hapa naomba nieleweke, si kuwalipia ada bali nitawasomesha kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne kwa kuwatimizia mahitaji yao yote ya shule ikiwa ni pamoja na sare, kalamu na madaftari, wazazi au walezi watanisaidia chakula, malazi na mavazi ya nyumbani, alisema.
Alisema uzoefu unaonesha watoa misaada wengi kwa watoto wa masikini, husaidia mwaka wa kwanza na kisha huwatelekeza hali inayosababisha watoto hao kukatisha masomo yao, kitendo ambacho amekilaani.
Unapoamua kuwasaidia, basi wasaidie kwa miaka yote na kwa mahitaji yao yote ya shule, ukisema umsaidie mwaka huu basi mwaka kesho ataacha shule na hivyo msaada wako utakuwa hauna maana, alifafanua Mwatuka.
Alibainisha kuwa iwapo watoto wa masikini hawatawezeshwa kupata elimu, ndoto za kuleta usawa katika kumiliki rasilimali za nchi haziwezi kufikiwa na kwamba mizizi ya ubepari itazidi kunawiri na kuhatarisha amani ya Taifa na kwamba hatua hiyo ni mwanzo kutokana na kuwa mwakilishi wa mikoa ya Lindi, Mtwara na wilaya ya Tunduru na Namtumbo mkoani Ruvuma.
Alisema ameamua kuanza na wilaya ya Masasi, kutokana na yeye mwenyewe kuwa mkazi wa wilaya hiyo hata hivyo jitihada zake za kuwakomboa wananchi wa eneo lake la kuongoza zitaenea wilaya zote 14, huku akiahidi kila mwezi kutembelea wilaya moja.
Kwa nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi, wazazi na wananchi wa wilaya ya Masasi wameelezea uamuzi wa mbunge huyo kuwa ni wa aina yake, kwani wabunge wa majimbo, viti maalumu waliopita, wameshindwa kufanya hivyo.
Kwa kata hizo 34 za wilaya ya Masasi, inamaanisha kwamba, mbunge huyo atasomesha wanafunzi 680.
Ada ya kila mtoto kwa shule ya Serikali ni Sh 20,000, hali ambayo itamfanya mbunge huyo kulipa zaidi ya Sh milioni 13.6 kwa mwaka.
Mbunge huyo aliyewania ubunge wa Masasi, lakini kura zake hazikutosha mbele ya Mariam Kasembe wa CCM, ameingia bungeni baada ya CUF kumteua, akiwa mbunge pekee wa kuteuliwa kutoka Kanda ya Kusini.
Akizungumza na HABARILEO Jumapili kijijini kwake Nanganga, wilayani hapa jana, alisema dhamira yake ni kuziba pengo baina ya matajiri na masikini na hilo litawezekana iwapo watoto wa masikini watawezeshwa kupata elimu na kwa kuanzia atasomesha watoto 680 kwa wilaya nzima.
Nimetoa maelekezo kwa watendaji wa kata kuleta majina ya watoto 20 waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwakani, ambao wazazi wao hawana uwezo katika wilaya yetu kuna kata 34, hivyo jumla ya wanafunzi wote watakuwa 680, alisema Mwatuka.
Aliongeza hapa naomba nieleweke, si kuwalipia ada bali nitawasomesha kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne kwa kuwatimizia mahitaji yao yote ya shule ikiwa ni pamoja na sare, kalamu na madaftari, wazazi au walezi watanisaidia chakula, malazi na mavazi ya nyumbani, alisema.
Alisema uzoefu unaonesha watoa misaada wengi kwa watoto wa masikini, husaidia mwaka wa kwanza na kisha huwatelekeza hali inayosababisha watoto hao kukatisha masomo yao, kitendo ambacho amekilaani.
Unapoamua kuwasaidia, basi wasaidie kwa miaka yote na kwa mahitaji yao yote ya shule, ukisema umsaidie mwaka huu basi mwaka kesho ataacha shule na hivyo msaada wako utakuwa hauna maana, alifafanua Mwatuka.
Alibainisha kuwa iwapo watoto wa masikini hawatawezeshwa kupata elimu, ndoto za kuleta usawa katika kumiliki rasilimali za nchi haziwezi kufikiwa na kwamba mizizi ya ubepari itazidi kunawiri na kuhatarisha amani ya Taifa na kwamba hatua hiyo ni mwanzo kutokana na kuwa mwakilishi wa mikoa ya Lindi, Mtwara na wilaya ya Tunduru na Namtumbo mkoani Ruvuma.
Alisema ameamua kuanza na wilaya ya Masasi, kutokana na yeye mwenyewe kuwa mkazi wa wilaya hiyo hata hivyo jitihada zake za kuwakomboa wananchi wa eneo lake la kuongoza zitaenea wilaya zote 14, huku akiahidi kila mwezi kutembelea wilaya moja.
Kwa nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi, wazazi na wananchi wa wilaya ya Masasi wameelezea uamuzi wa mbunge huyo kuwa ni wa aina yake, kwani wabunge wa majimbo, viti maalumu waliopita, wameshindwa kufanya hivyo.