Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari afikishwa Mahakamani; inadaiwa alimshambulia Mtendaji wa Kata mwaka 2014

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari afikishwa Mahakamani.
nas.jpg

Taarifa kutoka Arusha zilizotufikia hivi karibuni ni kuhusu Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.

Habari ambazo hazijathibitika zinadai kuwa, Nassari anakabiliwa na tuhuma za shambulio analodaiwa kulifanya kwa aliyekuwa Mtendaji wa Kata ya Makiba mwaka 2014. Mtendaji huyo bado hajatajwa jina lake.

========

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru akisubiri kusomewa shitaka linalomkabili.

Akizungumza na MCL Digital leo Jumanne Februari 6,2018, Nasari amesema jana alikwenda Kituo cha Polisi Usa River kufuatilia silaha yake iliyochukuliwa na askari wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014.

Nassari amesema alipofika polisi alielezwa kuwa ana kesi ya kumshambulia mtendaji kosa analodaiwa kutenda mwaka 2014 .

Sheki Mfinanga ambaye ni wakili wa Nassari amesema hajui mteja wake anakabiliwa na shtaka gani.

"Jana walisema alishambulia lakini hatujui leo anashitakiwa kwa kosa gani ndiyo tunasubiri," amesema.

Chanzo: Mwananchi
 
Anasema hauji kwa nini anashitakiwa!?
Mimi leo nimeona kahabari kengine hapa kamenijaza matumaini tele, achalia mbali kamati ya bunge eti hasara! Hivi kuna na ATR za abiria 300 au viBoeing vya abaria watano?
fg.jpg
 
Huo unaitwa UENDAWAZIMU, 2014 unamkamata leo, kwani alienda nje ya nchi baada ya kumshambulia, askar wetu hawa nao wanatumika vibaya, mpeni bunduki yake kuliko kutafta visingizio.
 
Spika Job Ndugai sijui lini ataburuzwa kwq pilato kwa kumshqmbulia mgombea mwenza kwq fimbo hadi kuzimia kule Kong wa.

Uchwara anataka kufunga wapinzani wote!!
Toa unafiki wako hapa, wakati anamshambulia wewe ulikuwepo? ukiambiwa uende ukatoe ushahidi utaenda? Acheni maneno ya vijiweni.
 
Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari afikishwa Mahakamani.
View attachment 691614
Taarifa kutoka Arusha zilizotufikia hivi karibuni ni kuhusu Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.

Habari ambazo hazijathibitika zinadai kuwa, Nassari anakabiliwa na tuhuma za shambulio analodaiwa kulifanya kwa aliyekuwa Mtendaji wa Kata ya Makiba mwaka 2014. Mtendaji huyo bado hajatajwa jina lake.

========

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru akisubiri kusomewa shitaka linalomkabili.

Akizungumza na MCL Digital leo Jumanne Februari 6,2018, Nasari amesema jana alikwenda Kituo cha Polisi Usa River kufuatilia silaha yake iliyochukuliwa na askari wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014.

Nassari amesema alipofika polisi alielezwa kuwa ana kesi ya kumshambulia mtendaji kosa analodaiwa kutenda mwaka 2014 .

Sheki Mfinanga ambaye ni wakili wa Nassari amesema hajui mteja wake anakabiliwa na shtaka gani.

"Jana walisema alishambulia lakini hatujui leo anashitakiwa kwa kosa gani ndiyo tunasubiri," amesema.

Chanzo: Mwananchi
Viwanda imeshindikana ni kesi za kubambika tuu sasa
 
Huo unaitwa UENDAWAZIMU, 2014 unamkamata leo, kwani alienda nje ya nchi baada ya kumshambulia, askar wetu hawa nao wanatumika vibaya, mpeni bunduki yake kuliko kutafta visingizio.
Mkuu, kiukweli KESI ZA JINAI HAZINA UKOMO yaan hazina kikwazo cha muda (rejea sheria ya ukomo wa kesi sura na 89 toleo la 2002)

Inawezekana pia (kwa hisia) baada ya diwani kupigwa aliumia na bado alikuwa anaendelea na matibabu ya maumivu/majeraha so wasingeweza kufungua kesi haraka maana hawajui Daktari angeandika nn kwenye PF3 (Police form No.3) ambayo itatumika km sehemu ya ushahidi upande wa mashitaka (PW).

Ngoja tusubiri hoja za hati ya mashtaka (Charge sheet) ili tuone kama kweli hii ni RULE OF LAW ama RULE OF WHIMS LAW.

" People's......."
 
Back
Top Bottom