Mbunge Dr. Mary Mwanjelwa amekanusha vikali kuwa anataka kuhamia CHADEMA

Duble Chris

JF-Expert Member
May 28, 2011
3,481
564
DSC00045.JPG


MBUNGE wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mbeya Dr.Mary Mwanjelwa amekanusha uvumi ulioripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kuwa anatarajia kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).


Alisema taarifa hizo ni uzushi na uongo kwa sababu yeye ni kada wa CCM wa siku nyingi ambaye amepewa dhamana na chama hicho kugombea ubunge kupitia jumuiya ya wanawake hivyo hatarajii kuwageuka kwa sababu bado anayo dhamana ya kuendelea kuwa Mbunge.


Alisema, taarifa hizo zimenishtua sana, na hata wapiga kura wangu nao wamepata mshtuko mkubwa na wakanipigia simu ili kutaka kupata ukweli kutoka kwangu hivyo nimeona ni vizuri nitoe ufafanuzi.



Alisema yeye ni mbunge wa wananchi wote mkoani hapa, hana matatizo yeyote na chama hivyo haielewi sababu za kumfanya ahame chama chake na kujiunga na CHADEMA, kwa sababu ya uteuzi wa baraza jipya la mawaziri.



"Mimi ni mbunge kwa tiketi ya CCM na pia ni kada wa chama ambacho ndicho kilichonipitisha kugombea nafasi ya ubunge viti maalumu, na hatimaye nikafanikiwa kuchaguliwa sasa iwaje leo nikihame chama,"alihoji Mbunge huyo.



Aliongeza habari zilizoripotiwa ni za uongo, na kuwa kamwe hawezi kuingilia uteuzi wa Rais Kikwete katika kuwateua mawaziri, kwani hayo ni mambo ambayo hayamhusu kabisa.

Dk.Mary alisema yeye amekwenda Bungeni kuwawakilisha wananchi wa mkoa wa Mbeya, sikwenda Bungeni kwa sababu ya kutaka kuwa Waziri, hizo ni nafasi za uteuzi na mwenye mamlaka hiyo ni Rais Kikwete.



Mbunge huyo wa viti maalum Mbeya, aliongeza hivyo ni vyema waandishi wa habari waache kuandika habari za kuchafuana, kuharibiana bali wafuate misingi na maadiri yanayolinda tasnia ya habari.



Alisema iwapo mwandishi anakuwa amepata taarifa ni vyema amfuate muhusika ili kupata ukweli juu ya habari anayotaka kuiandika iwapo ina ukweli wowote ndani yake.

Aliongeza kama hayo yalikuwa ni maoni ya wananchi, anashindwa kuelewa yeye anaingizwaje katika habari hiyo, kwani ana mkataba wa kuwatumikia wananchi kwa miaka mitano na amebakiza miaka mitatu.



"Siwezi kuhamia CHADEMA, kwani CCM haijanifanyia kosa lolote, sikwenda Bungeni ili niteuliwe kuwa Waziri, kikubwa kwangu ni kuingia Bungeni kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi wangu wa mkoa wa Mbeya" alisema Dk.Mary.



Kwa mujibu wa Mwanjelwa alisema kuwa ni kweli alizungumza na Mwandishi aliyeandika habari hizo na kwamba mwandishi huyo alikuwa akitaka kupata ufafanuzi wa uvumi ulioenea ya kwamba kuna baadhi ya wananchi wanataka kwenda kumuona ili wamshawishi akihame chama kwa sababu ya Rais hakumteua kwenye Baraza jipya la Mawaziri.



"Mimi nilimjibu mwandishi huyo ya kwamba huo ni mtazamo wa wananchi lakini si wa kwangu "alisema Mwanjelwa huku akisisitiza kuwa hicho ni kipindi chake cha kwanza kuingia Bungeni sasa iwaje ashikwe na tamaa ya kutaka kushika madaraka ya juu .



Hata hivyo, alisema atagombea tena nafasi hiyo kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ili wanawake wampe tena kura zao kwani anajijua bado anafaa zaidi ya kufaa, hivyo atajitokeza katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 kutetea nafasi yake hiyo kwa tiketi ya Chama cha mapinduzi..


SOURCE: - HAPA

MY TAKE waandishi muwe makini sana
 
huyo kimoyo moyo anataka kuhama ila anaogopa......yaani magamba wanawaogopa mabosi wao balaa
 
Gamba mkubwa huyo tena mchumia tumbo na kamwe kwa hali ya uroho wa madaraka na kupenda bata za kijinga jinga hawezi kujiunga na makamanda wa millenia kama CDM ktk harakati hizi kwani CDM tunataka watu waliojizabihu nafsi zao kwa ajili ya maslahi ya wengi ikiwemo pa1 na kutokuogopa, kuwa tayar kupinga kila aina ya unyonyaji ikibidi hata kufa, sasa huyo ataweza kweli?
YUPO TAYARI KUPIGANIA WANYONGE ATAWEZA KUHATARISHA MAISHA YAKE KWA KUCHINJWA KAMA iIP MWENYEKITI USER RIVER? Jibu ni kwamba hawezi so tumache amalize bata za mwisho huko ccm kwani almost wana miaka 3 tu ya kula bata koz baada 2015 wote wataingia gerezani kwa wizi wa rasilimali zetu.
 
Ukisoma katikati ya mistari utaona kuwa majibu yake yamejikita zaidi kwenye kuongelea uteuzi wa mawaziri, lakini hajaisema vibaya wala kuikandia CDM hata kidogo, jambo linaloashiria ana hisia chanya na chama hiki. Zaidi sana maneno yake yanamuonyesha kama mtu ambaye ana wasiwasi na ikiwa kwa mfano atafuatwa na mtu kama Halima Mdee naamini anaweza kutetereka. Lakini kwa namna yoyote ile hawa ni suala la muda tu kabla mmoja mmoja hawajaanza kubisha hodi CDM.
 
Alisema, taarifa hizo zimenishtua sana, na hata wapiga kura wangu nao wamepata mshtuko mkubwa na wakanipigia simu ili kutaka kupata ukweli kutoka kwangu hivyo nimeona ni vizuri nitoe ufafanuzi.

Alisema yeye ni mbunge wa wananchi wote mkoani hapa, hana matatizo yeyote na chama hivyo haielewi sababu za kumfanya ahame chama chake na kujiunga na CHADEMA, kwa sababu ya uteuzi wa baraza jipya la mawaziri.

"Mimi ni mbunge kwa tiketi ya CCM na pia ni kada wa chama ambacho ndicho kilichonipitisha kugombea nafasi ya ubunge viti maalumu, na hatimaye nikafanikiwa kuchaguliwa sasa iwaje leo nikihame chama,"alihoji Mbunge huyo.

Hapo kwenye RED, huyu ni mbunge wa viti maalum, sasa hao wapiga kura wa ni kina nani?

Inampasa atambue kuwa yeye amechaguliwa na magamba na sio wananchi wa Mbeya mjini, wananchi wa Mbeya mjini walimchagua Sugu..
 
sijamwelewa amesema wapiga kura wake yeye si mbunge wa viti maalumu hao wapiga kura wake toka mbeya wametokea wapi?na sugu amechaguliwa kuongoza wapi aache unafiki kwani ameshaona ni vigumu kumng'oa sugu kwa jinsi anavyokubalika
 
hakusema anahamia cdm bali anapima upepo kwanza. Ila nadhani akiungana na sugu watafika mbali
 
Hapo kwenye RED, huyu ni mbunge wa viti maalum, sasa hao wapiga kura wa ni kina nani? Inampasa atambue kuwa yeye amechaguliwa na magamba na sio wananchi wa mbeya mjini, wananchi wa mbeya mjini walimchagua Sugu..
wapiga kura wake ni wale wa ndani nadhani UWT huwapigia kura wote wanao hitaji ubunge kupitia viti maalum
 
hakusema anahamia cdm bali anapima upepo kwanza. Ila nadhani akiungana na sugu watafika mbali
Mafuta na maji havichangamani hata siku moja. Na hapo ndipo CDM inatakiwa kuwa makini sana na wote wanaohamia huko sasa hivi.
 
mwanbie akanushe kuwa ni mzazi mwenza na Jk!!!tunalojua ni kuwa ndoa yake na ccm IPO kulinda ndoa yake na jk!!
 
hizi viti maalaam tolea mbali kabisa ni moja kati ya vitu vinavyotudididimiza bure ,kaazi yao kubwa malumbano majimboni huko wanajipanga na 2015
 
swali langu ni kwamba,mwandishi wa habari ile hakumungunya maneno,alimtaj hadi kwa jina na akafanya hadi nukuu ya baadhi ya maneno ya mheshimiwa mary mwanjelwa ,sasa je ujasiri huu mwandishi wa habari aliupata wapi?iwapo habari ni ya uongo?
 
DSC00045.JPG


MBUNGE wa viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mbeya Dr.Mary Mwanjelwa amekanusha uvumi ulioripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari hapa nchini kuwa anatarajia kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).


Alisema taarifa hizo ni uzushi na uongo kwa sababu yeye ni kada wa CCM wa siku nyingi ambaye amepewa dhamana na chama hicho kugombea ubunge kupitia jumuiya ya wanawake hivyo hatarajii kuwageuka kwa sababu bado anayo dhamana ya kuendelea kuwa Mbunge.


Alisema, taarifa hizo zimenishtua sana, na hata wapiga kura wangu nao wamepata mshtuko mkubwa na wakanipigia simu ili kutaka kupata ukweli kutoka kwangu hivyo nimeona ni vizuri nitoe ufafanuzi.



Alisema yeye ni mbunge wa wananchi wote mkoani hapa, hana matatizo yeyote na chama hivyo haielewi sababu za kumfanya ahame chama chake na kujiunga na CHADEMA, kwa sababu ya uteuzi wa baraza jipya la mawaziri.



"Mimi ni mbunge kwa tiketi ya CCM na pia ni kada wa chama ambacho ndicho kilichonipitisha kugombea nafasi ya ubunge viti maalumu, na hatimaye nikafanikiwa kuchaguliwa sasa iwaje leo nikihame chama,"alihoji Mbunge huyo.



Aliongeza habari zilizoripotiwa ni za uongo, na kuwa kamwe hawezi kuingilia uteuzi wa Rais Kikwete katika kuwateua mawaziri, kwani hayo ni mambo ambayo hayamhusu kabisa.

Dk.Mary alisema yeye amekwenda Bungeni kuwawakilisha wananchi wa mkoa wa Mbeya, sikwenda Bungeni kwa sababu ya kutaka kuwa Waziri, hizo ni nafasi za uteuzi na mwenye mamlaka hiyo ni Rais Kikwete.



Mbunge huyo wa viti maalum Mbeya, aliongeza hivyo ni vyema waandishi wa habari waache kuandika habari za kuchafuana, kuharibiana bali wafuate misingi na maadiri yanayolinda tasnia ya habari.



Alisema iwapo mwandishi anakuwa amepata taarifa ni vyema amfuate muhusika ili kupata ukweli juu ya habari anayotaka kuiandika iwapo ina ukweli wowote ndani yake.

Aliongeza kama hayo yalikuwa ni maoni ya wananchi, anashindwa kuelewa yeye anaingizwaje katika habari hiyo, kwani ana mkataba wa kuwatumikia wananchi kwa miaka mitano na amebakiza miaka mitatu.



"Siwezi kuhamia CHADEMA, kwani CCM haijanifanyia kosa lolote, sikwenda Bungeni ili niteuliwe kuwa Waziri, kikubwa kwangu ni kuingia Bungeni kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi wangu wa mkoa wa Mbeya" alisema Dk.Mary.



Kwa mujibu wa Mwanjelwa alisema kuwa ni kweli alizungumza na Mwandishi aliyeandika habari hizo na kwamba mwandishi huyo alikuwa akitaka kupata ufafanuzi wa uvumi ulioenea ya kwamba kuna baadhi ya wananchi wanataka kwenda kumuona ili wamshawishi akihame chama kwa sababu ya Rais hakumteua kwenye Baraza jipya la Mawaziri.



"Mimi nilimjibu mwandishi huyo ya kwamba huo ni mtazamo wa wananchi lakini si wa kwangu "alisema Mwanjelwa huku akisisitiza kuwa hicho ni kipindi chake cha kwanza kuingia Bungeni sasa iwaje ashikwe na tamaa ya kutaka kushika madaraka ya juu .



Hata hivyo, alisema atagombea tena nafasi hiyo kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ili wanawake wampe tena kura zao kwani anajijua bado anafaa zaidi ya kufaa, hivyo atajitokeza katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 kutetea nafasi yake hiyo kwa tiketi ya Chama cha mapinduzi..


SOURCE: - HAPA

MY TAKE waandishi muwe makini sana

Taarifa yake inadokeza uwaziri siyo issue ila kama ushawishi wa kujiunga na movement for change utamfikia kikamilafu atasepa,
 
maajabu haya tena inamaana taarifa zilizoletwa hapa juzi zilikuwa zauongo? au ameongopa ma boss wake? tuweni makini na hawa mamruki
 
Back
Top Bottom