Mbunge augua ghafla bungeni

Kaitaba

JF-Expert Member
Jun 30, 2009
916
52
Ile hali ya kuugua na kuanguka ghafula kwa wabunge iliyokuwa imesimama, sasa imerudi tena baada ya mbunge wa viti maalum Mh, Maria Hewa kuanguka ghafula akiwa bungeni dodoma na kukimbizwa hospitali

Habari zaidi tutazidi kuwaletea
 
Oh ma gad, a hop its not pressure of TAKUKURU queries on doule payments.
 
oooh!
Pole zake...Ninini hii hali huko mjengoni? Au watu wanafukuzia nafasi yake huko jimboni!
 
Haya tupate habari zaidi kutoka gazeti la Alasiri:

Na Emmanuel Lengwa

30th October 2009

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mheshimiwa Maria Hewa, leo amejikuta akikosa vipindi vya maswali na majibu na pia kuweza kushiriki katika michango mbalimbali baada ya kuugua ghafla bungeni na kukimbiziwa hospitalini.

Mbunge huyo, amekutwa na masahibu hayo leo asubuhi, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Bunge, tayari kwa kuungana na wenzie katika shughuli za leo.

Akizungumza baada ya kipindi cha maswali na majibu, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Samwel Sitta, amesema Mheshimiwa huyo alifika mwenyewe bungeni, lakini aliugua ghafla na hivyo kuwahishwa katika Hospitali ya Mkoa huu (Dodoma) kwa ajili ya matibabu zaidi.

Amewataka wabunge watakaotaka kumjulia hali mheshimiwa huyo kufanya hivyo katika hospitali hiyo ya mkoa.

Hata hivyo, hakukuwa na taarifa za chanzo cha kuugua huko ghafla kwa Mheshimiwa huyo, ambaye alikuwa akihudhuria vyema bungeni tangu Jumanne na jana alionekana yu mzima wa afya.

Katika Bunge lililopita, Naibu Waziri wa Miundombinu, Mheshimiwa Hezekiel Chibulunje, aliwahi kukutwa na tatizo kama hilo la kuugua ghafla bungeni.

Yeye alikutwa na mkasa huo wakati akijibu swali la Mbunge mmojawapo kabla ya kusaidiwa na wenzie na kukimbiziwa hospitalini ambako alitibiwa na kuruhusiwa.
CHANZO: ALASIRI
 
Hivi wabunge kwa nafasi zao, huwa wana utaratibu wa kuangalia afya zao mara kwa mara kweli au ndo kama tulivojizoeza? hali kama hii ingeepukwa sana kama tugekuwa na utaratibu huo. naamini kucheki afya kwao sio tatizo kama kwa mwananchi wa kawaida so ni vema wawe wanafanya hivyo!
 
Ni nadra sana mtu kuanguka au kuumwa "ghafla". Ikitokea hivyo jua mtu alisha kua na matatizo ya kiafya ya muda aidha kwa kujua au kuto kujijua. Ndiyo maana ni muhimu sana kucheki afya kila baada ya muda fulani. Tatizo ni kwamba Watanzania hatuna utamaduni wa regular check ups hata kwa wenye uwezo. Mtu kwenda hospitali mpaka aumwe au aambiwe na daktari awe ana kuja kila baada ya muda fulani.
 
Back
Top Bottom