Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Hii inaonyesha jinsi wabunge wanavyolipwa pesa nyingi zaidi ya mahitaji yao. Serikali inatakiwa iwape waalimu mishahara inayotosha kukidhi huduma zao muhimu, na sio kupewa misaada na watu wanaotafuta kujiendeleza.
Mbunge aamua kuwalipia walimu kodi za nyumba
Na Thobias Mwanakatwe
3rd May 2010
Katika hatua inayotafsiriwa kuwa ni kampeni za mapema kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Mbunge wa Songwe wilayani Chunya, Mkoa wa Mbeya, Dk. Guido Sigonda, ameahidi kuwalipia kodi za nyumba walimu wa shule za sekondari na msingi wa Kata ya Galula wilayani hapa.
Mbunge huyo aliahidi kuchukua hatua hiyo kutokana na kata hiyo kutokuwa na nyumba za kuishi watumishi.
Dk. Sigonda alitoa ahadi hiyo juzi, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi ambayo ngazi ya kata yalifanyika katika Kijiji cha Magamba. Mbunge huyo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.
Uamuzi wa mbunge huyo kutangaza kuwalipia kodi ya pango la nyumba walimu wa kata hiyo, ulifuatia maelezo yaliyotolewa na walimu hao kuwa wanaishi katika nyumba za kupanga kwa muda mrefu hali inayowapa usumbufu kutokana na serikali kutowajengea nyumba za kuishi.
Walimu hao walimweleza Sigonda kwamba wanaishi katika maisha magumu kutokana na kiwango kidogo cha mishahara wanachokipata kutumia kiasi fulani kulipia kodi za pango la nyumba.
Walimweleza kuwa hali hiyo ni miongoni mwa mambo ambayo yanachangia kuzorota kwa kiwango cha elimu katika Jimbo la Songwe.
Dk. Sigonda alisema wakati serikali kwa kushirikiana na wananchi wa vijiji husika, inafanya mipango ya kujenga nyumba za kuishi kwa ajili ya walimu, yeye atawalipia kodi ya nyumba kila mwezi hadi hapo zitakapojengwa na kuwaagiza viongozi wa kata kumpelekea idadi ya walimu wanaoishi kwenye nyumba za kupanga.
Tatizo la nyumba za kuishi watumishi ni la nchi nzima, hata hivyo, mimi kama mbunge wenu, natangaza kuanzia sasa kwamba nitaanza kuwalipia kodi ya nyumba hadi hapo serikali itakapowajengea nyumba za kuishi, alisema Dk. Sigonda.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria waliichukulia ahadi hiyo kuwa huenda ni kampeni za uchaguzi mkuu ujao kwa kuwa kukosekana kwa nyumba za walimu ni tatizo la muda mrefu.
Mmoja wa wakazi wa kata hiyo ambaye hakutaka kutajwa, alihoji inakuwaje mbunge huyo awaonee huruma walimu hao kwa kuwalipia kodi za nyumba wakati hakufanya hivyo miaka mitano iliyopita.
Dk. Sigonda alitoa ahadi hiyo huku baadhi ya wananchi nchini wakiwalalamikia wanasiasa, wakiwemo wabunge wanaotoa misaada katika maeneo yao hivi sasa wakati uchaguzi mkuu ukikaribia.
Wananchi hao wanasema inakuwaje wanasiasa hao hawakutoa misaada hiyo kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne tangu waliposhika nafasi hizo.
Katika maeneo mengi nchini, ukiwemo Mkoa wa Mbeya, wanasiasa hususan wabunge, wamekuwa wakitoa misaada ya fedha taslim, vyombo vya usafiri kama pikipiki na misaada mingine kwa wapigakura wao wakidai kuwa wanatimiza ahadi walizozitoa kwao katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.
Jana mchana, Nipashe ilipowasiliana na Dk. Sigonda ili kutoa ufafanuzi wa ahadi yake kwa walimu na kampeni za uchaguzi, alisema kuwa alikuwa kwenye kikao.
Hata hivyo, alipotafutwa baadaye, mara zote simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.
Katika hatua nyingine, Dk. Sigonda alisema serikali imekubali kuwalipa wakulima fedha za pamba na kwamba zimeshapelekwa wilayani na utaratibu wa kulipa unaandaliwa.
Alisema madeni hayo yatakayolipwa ni yale ambayo yamelimbikizwa toka mwaka 1995 hadi 1996 na kuwataka wakulima ambao majina yao hayatajitokeza katika malipo hayo wawasilishe nyaraka ili walipwe.
Mbunge huyo pia alitoa Sh. 400,000 kwa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Watumishi wa Kata ya Galula ili kusaidia kutunisha mfuko wa chama kiweze kuwakopesha wanachama wake.
Mbunge aamua kuwalipia walimu kodi za nyumba
Na Thobias Mwanakatwe
3rd May 2010
Katika hatua inayotafsiriwa kuwa ni kampeni za mapema kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Mbunge wa Songwe wilayani Chunya, Mkoa wa Mbeya, Dk. Guido Sigonda, ameahidi kuwalipia kodi za nyumba walimu wa shule za sekondari na msingi wa Kata ya Galula wilayani hapa.
Mbunge huyo aliahidi kuchukua hatua hiyo kutokana na kata hiyo kutokuwa na nyumba za kuishi watumishi.
Dk. Sigonda alitoa ahadi hiyo juzi, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi ambayo ngazi ya kata yalifanyika katika Kijiji cha Magamba. Mbunge huyo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.
Uamuzi wa mbunge huyo kutangaza kuwalipia kodi ya pango la nyumba walimu wa kata hiyo, ulifuatia maelezo yaliyotolewa na walimu hao kuwa wanaishi katika nyumba za kupanga kwa muda mrefu hali inayowapa usumbufu kutokana na serikali kutowajengea nyumba za kuishi.
Walimu hao walimweleza Sigonda kwamba wanaishi katika maisha magumu kutokana na kiwango kidogo cha mishahara wanachokipata kutumia kiasi fulani kulipia kodi za pango la nyumba.
Walimweleza kuwa hali hiyo ni miongoni mwa mambo ambayo yanachangia kuzorota kwa kiwango cha elimu katika Jimbo la Songwe.
Dk. Sigonda alisema wakati serikali kwa kushirikiana na wananchi wa vijiji husika, inafanya mipango ya kujenga nyumba za kuishi kwa ajili ya walimu, yeye atawalipia kodi ya nyumba kila mwezi hadi hapo zitakapojengwa na kuwaagiza viongozi wa kata kumpelekea idadi ya walimu wanaoishi kwenye nyumba za kupanga.
Tatizo la nyumba za kuishi watumishi ni la nchi nzima, hata hivyo, mimi kama mbunge wenu, natangaza kuanzia sasa kwamba nitaanza kuwalipia kodi ya nyumba hadi hapo serikali itakapowajengea nyumba za kuishi, alisema Dk. Sigonda.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria waliichukulia ahadi hiyo kuwa huenda ni kampeni za uchaguzi mkuu ujao kwa kuwa kukosekana kwa nyumba za walimu ni tatizo la muda mrefu.
Mmoja wa wakazi wa kata hiyo ambaye hakutaka kutajwa, alihoji inakuwaje mbunge huyo awaonee huruma walimu hao kwa kuwalipia kodi za nyumba wakati hakufanya hivyo miaka mitano iliyopita.
Dk. Sigonda alitoa ahadi hiyo huku baadhi ya wananchi nchini wakiwalalamikia wanasiasa, wakiwemo wabunge wanaotoa misaada katika maeneo yao hivi sasa wakati uchaguzi mkuu ukikaribia.
Wananchi hao wanasema inakuwaje wanasiasa hao hawakutoa misaada hiyo kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne tangu waliposhika nafasi hizo.
Katika maeneo mengi nchini, ukiwemo Mkoa wa Mbeya, wanasiasa hususan wabunge, wamekuwa wakitoa misaada ya fedha taslim, vyombo vya usafiri kama pikipiki na misaada mingine kwa wapigakura wao wakidai kuwa wanatimiza ahadi walizozitoa kwao katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.
Jana mchana, Nipashe ilipowasiliana na Dk. Sigonda ili kutoa ufafanuzi wa ahadi yake kwa walimu na kampeni za uchaguzi, alisema kuwa alikuwa kwenye kikao.
Hata hivyo, alipotafutwa baadaye, mara zote simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.
Katika hatua nyingine, Dk. Sigonda alisema serikali imekubali kuwalipa wakulima fedha za pamba na kwamba zimeshapelekwa wilayani na utaratibu wa kulipa unaandaliwa.
Alisema madeni hayo yatakayolipwa ni yale ambayo yamelimbikizwa toka mwaka 1995 hadi 1996 na kuwataka wakulima ambao majina yao hayatajitokeza katika malipo hayo wawasilishe nyaraka ili walipwe.
Mbunge huyo pia alitoa Sh. 400,000 kwa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Watumishi wa Kata ya Galula ili kusaidia kutunisha mfuko wa chama kiweze kuwakopesha wanachama wake.