Mugo"The Great"
JF-Expert Member
- Oct 7, 2007
- 262
- 25
"CCM wanasafisha Chama chao na sisi tusafishe chetu, tusibweteke na umaarufu binafsi wa baadhi ya viongozi wetu''.
CCM hawasafishi Chama bali wanakipaka rangi kwa nje kwa kutumia umaskini wa Wadanganyika wengi . Wangekuwa wanasafisha Chama ubadhirifu uliofanyika NSSF, Mikataba mibovu ya IPTL, CITY Water na Uanzishwaji wa makampuni ya kuchota fedha za wadanganyika ungekwisha na waliohusika wangefukuzwa uanachama na kuozea segerea.
''Mwenyekiti ana historia chafu ya ufuska na uasherati . Hili ni tatizo kwa maadili lakini ni tatizo zaidi kwa Mwenyekiti Mbowe kwasababu analeta hizi tabia kwenye kazi na kuleta mifarakano''.
Kwani mjomba yeye msafi??
Ninachojua sasa hivi ni suala la wakati tu lakini nguvu ya Sisiemu inapungua na hata kule vijinini kama Sitalike, Chankabwimba, Vudee, Kazaroho(Urb) wadanganyika wameanza kuamka kwenye usingizi mzito.