Mbowe: Hatukubali matokeo EALA na tutakwenda mahakamani

Paskali unataka kutuambia kile ambacho ulishauri kwenye bandiko lako jana kina reflect kilichotokea kwenye uchaguzi? How? Katika hoja yako jana ulikuwa ukiwashauri na kuwabeza CDM kwamba wasiende kortini baada ya kutolewa taarifa kwamba CDM hawakutimiza matakwa ya kikanuni ikiwemo suala la gender balance. Lakini kabla CDM hawajaenda kortini wakawa wameruhusiwa kushiriki uchaguzi na kura zikapigwa kwa maana ya kwamba hoja ile ya kutofuatwa kwa kanuni haikuwa na mashiko kwa mujibu wa taratibu na sheria za uchaguzi wa EALA. Hii maana yake ni kwamba hata ushauri na kubeza kwako hakukuwa na mashiko!

Sasa CDM wanasema wanataka waende kortini kupinga kilichofanyika kwenye uchaguzi naona umeibuka tena ukitumia andiko hilo hilo la jana kama reference. Kinachonishangaza ni kwamba badala ya wewe uwaunge mkono CDM kwenda kortini (hata kama madai yao na yako yatakuwa tofauti kidogo) lakini bado unaendelea kuwaponda na kuwabeza!

Kama jana uliandika andishi refu ukiunga mkono uamuzi wa CDM kuwekewa ngumu kushiriki uchaguzi huo hadi wakidhi kilichodaiwa kuwa ni matakwa ya kikanuni, lakini baadaye wakaruhusiwa huoni kwamba uchaguzi ule ulifanyika pasipo kuzingatia taratibu za kikanuni zinazosimamia uchaguzi huo?
Mkuu
chabusalu hoja yangu ya jana, hapa CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA! ilihusu Chadema kutishia kwenda mahakamani kuusimamisha uchaguzi wa EALA, kisa ni kuzuiliwa kwa ukosefu wa gender balance, nikasema hiki ni chama cha ajabu sana, katiba imevunjwa ambayo ndio wangepswa kwenda mahakamani, badala yake walihamasisha maandamano ya UKUTA, nikawaandikia kuwauliza hivi uvunjaji wa katiba unapingwa kwa maandamano?.

Issue ya EALA ni ndogo na very simple, ilihitaji tuu, gender mainstreaming na inclusion, kama wabunge wanatakiwa kuwa na 1/3 ya wanawake, then kila chama lazima kilete 1/3 ya wanawake hata kama sio lazima wachaguliwe!. Hili ni hitaji la kikanuni, halina mjadala, hivyo kama kweli jana wangekwenda kuusimamisha uchaguzi mahakamani, wangekuwa ni watu wa ajabu sana!. Nikasema tatizo kubwa kabisa la Chadema, hawana ma strategists, kama nafasi zao ni mbili, na walijijua wanamtaka Wenje na Masha, then wangepeleka watu 6, wakiwemo wanawake wawili, hao wanne wangepeleka maboya, ili Masha na Wenje ndio wawe the best!. Kitendo cha nafasi zao mbili kisha wakapeleka watu hao hao wawili, ni kulilazimisha bunge kuwa a rumber stamp ya Chadema, na kwa vile wabunge had no choice to choose from, wakaamua kupiga kura za ndio na hapana!.

Kiukweli kilichofanyika kwenye selection ya Chadema ni madudu!, sasa kama wapenzi wa dhati wa Chadema mnaogopa kukiambia chama chenu, kuwa it got to do things right, hamkisaidii, nani anajua hao Masha na Wenje wamepatikanaje?, sasa kwenye issues ndogo ndogo kama hizi wanashindwa, wangekabidhiwa ikulu si ingekuwa chaos?. Kila nikilisoma bandiko hili la mwaka 2014 CHADEMA Ikipewa Nchi, October 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!
nimejikuta niko right, sasa watu kama hawa kwenye issue ndogo kama hii, wanashindwa, halafu ndio watujie ile 2020 kuwaomba Watanzania wawakabidhi nchi?!.

Hoja ambayo ni valid na ina hold water ni double standard ya CUF A na B!. NB, viti wiwili vya Chadema bado vipo, wanatakiwa kuleta watu wengine wakiwemo wanawake, then bunge litawachagua hao wawili na sii lazima achaguliwe mwanamke. Wampeleke Salum Mwalimu na Kafulila, wawatafutie maboya 4 ya kuwasindikiza, hili jambo liishe, kama ni kesi, wakamshitaki mvunja katiba.

Paskali
 
Nashindwa kuelewa kiini na sababu ya msingi ya kura waliopigiwa wagombea wa chadema. Msema kweli mpenzi wa Mungu, tunajua, nanafahamu na tumeona si mara moja au mbili bali mara nyingi kwenye uchaguzi wowote nafasi inayogombaniwa inapo baki na mgombea mmoja hupita bila kupingwa.

Je, kama wagombea sita wa CCM wangejitoa kisha wakabaki 6 wangepigiwa kura wakati waliokuwa wanahitajika walikuwa 6?

Kilichofanyika ni kuwanyima haki watanzania kuwakilishwa na mawazo mbadala kutokana chadema.
 
Hapana unakosea

CCM walijua kabisa wana nafasi sita

Ila kwa kutambua Demokrasia wamepeleka watu zaidi ili bunge lipate nafasi ya kuchagua....

Kujitoa ni tofauti na kutokupeleka kabisa mgombea

Tusitetee ujinga uliokubuhu wa Mbowe
 
Hapana unakosea

CCM walijua kabisa wana nafasi sita

Ila kwa kutambua Demokrasia wamepeleka watu zaidi ili bunge lipate nafasi ya kuchagua....

Kujitoa ni tofauti na kutokupeleka kabisa mgombea

Tusitetee ujinga uliokubuhu wa Mbowe

Kanuni na sheria hazijawalazimisha kaka yangu. kwa nini tunapenda kulazimisha mawazo yetu badala ya kufuata sheria?
 
WATANZANIA TUSIPOONGEA ILI BUNGE LA AFRICA MASHARIKI LIKASIKIA NA KUWAWEKEA PINGAMIZI CCM WASIVURUGE TARATIBU ZA UCHAGUZI ZA BUNGE HILO, HASA SISI TUNAOATHIRIKA NA MAGOLI YA MKONO TUTAKUWA HATUJALITENDEA TAIFA LETU HAKI.

KWA LEO NAPENDA KUPINGA NA KULAANI KITENDO CHA KUKIUKWA TARATIBU ZA UCHAGUZI WA BUNNE HILO ZILIZOFANYWA NA CCM BUNGENI ....HAKUNA UTARATIBU WA KUPIGA KURA ZA NDIO AU HAPANA MAHALI POPOTE KATIKA BUNGE LA A.MASHARIKI NA IMETOKEA KUWA NI WABUNGE WETU TU WA CDM WAMEKUWA WAKIPIGIWA KURA KWA MTINDO HUO.....IKUMBUKWE KUWA KILA MBUNGE ALITAKIWA KUPIGA KURA TISA LAA SIVYO KURA ITAKUWA IMEHARIBIKA....KWA KUINGIZA TARATIBU BATILI YA KURA ZA NDIO/HAPANA WAMEWEZA KUJIONESHA KUWA WAMEPIGA KURA TISA WAKATI ILITAKIWA KIUHALISIA PASIWEPO HIYO OPTION YA HAPANA NA SISI CDM TUNGEPATA HAKI ZETU BILA PINGAMIZI.

WATANZANIA TUNALITAKA BUNGE LA AFRICA MASHARIKI LITAKAPOKUTANA LILAANI NA KUPINGA UTARATIBU HUU NA TURUDISHIWA WABUNGE WOTE TUWAPIGIE KURA UPYA KWA UTARATIBU UNAOSTAHILI!!
Hivi kwa hakili yako unajua nn maana ya uchaguzi? Hivi hamuoni kosa mlilofanya mpaka mtokwe povu hivyo. Vyama vingine vilikuwa na wagombea wengi kuliko idadi inayotakiwa ili wabunge wachague kati ya hao yupi wanataka akawawakilishe kwenye bunge la E.Afrika.

Ila nyie kwa ufinyu wa akili zenu mkajua upoyoyo mnaofanyiwa na na mwenyekiti wenu wa kuletewa majina mfukoni ndo utakubaliwa na spika msahau.
Au kama ww kwa hakili yako nafasi zilikuwa zinatakiwa wachaguliwe watu wawili halafu na nyie mmeleta watu 2 mfumi gani ungetumika zidi ya huo wa kula za ndio au hapana?


Kuweni na hakili za ziada ndo maana wamekataliwa wote mkalete majina ya kupigiwa kula wabunge wenyewe wachague sio ninyi kuwapangia kwamba wenje na masha ndo wapite.
 
Mkuu
chabusalu hoja yangu ya jana, hapa CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA! ilihusu Chadema kutishia kwenda mahakamani kuusimamisha uchaguzi wa EALA, kisa ni kuzuiliwa kwa ukosefu wa gender balance, nikasema hiki ni chama cha ajabu sana, katiba imevunjwa ambayo ndio wangepswa kwenda mahakamani, badala yake walihamasisha maandamano ya UKUTA, nikawaandikia kuwauliza hivi uvunjaji wa katiba unapingwa kwa maandamano?.

Issue ya EALA ni ndogo na very simple, ilihitaji tuu, gender mainstreaming na inclusion, kama wabunge wanatakiwa kuwa na 1/3 ya wanawake, then kila chama lazima kilete 1/3 ya wanawake hata kama sio lazima wachaguliwe!. Hili ni hitaji la kikanuni, halina mjadala, hivyo kama kweli jana wangekwenda kuusimamisha uchaguzi mahakamani, wangekuwa ni watu wa ajabu sana!. Nikasema tatizo kubwa kabisa la Chadema, hawana ma strategists, kama nafasi zao ni mbili, na walijijua wanamtaka Wenje na Masha, then wangepeleka watu 6, wakiwemo wanawake wawili, hao wanne wangepeleka maboya, ili Masha na Wenje ndio wawe the best!. Kitendo cha nafasi zao mbili kisha wakapeleka watu hao hao wawili, ni kulilazimisha bunge kuwa a rumber stamp ya Chadema, na kwa vile wabunge had no choice to choose from, wakaamua kupiga kura za ndio na hapana!.

Kiukweli kilichofanyika kwenye selection ya Chadema ni madudu!, sasa kama wapenzi wa dhati wa Chadema mnaogopa kukiambia chama chenu, kuwa it got to do things right, hamkisaidii, nani anajua hao Masha na Wenje wamepatikanaje?, sasa kwenye issues ndogo ndogo kama hizi wanashindwa, wangekabidhiwa ikulu si ingekuwa chaos?. Kila nikilisoma bandiko hili la mwaka 2014 CHADEMA Ikipewa Nchi, October 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!
nimejikuta niko right, sasa watu kama hawa kwenye issue ndogo kama hii, wanashindwa, halafu ndio watujie ile 2020 kuwaomba Watanzania wawakabidhi nchi?!.

Hoja ambayo ni valid na ina hold water ni double standard ya CUF A na B!. NB, viti wiwili vya Chadema bado vipo, wanatakiwa kuleta watu wengine wakiwemo wanawake, then bunge litawachagua hao wawili na sii lazima achaguliwe mwanamke. Wampeleke Salum Mwalimu na Kafulila, wawatafutie maboya 4 ya kuwasindikiza, hili jambo liishe, kama ni kesi, wakamshitaki mvunja katiba.

Paskali
Mkuu Paskali, unaweza usikubaliane na mimi lakini ukweli ni kwamba hiki ulichokiandika hapa kinaonyesha unakubaliana moja kwa moja na mkakati wa CDM na wala kumbe huna sababu hata kiduchu ya kuwabeza. CDM wanajaribu kuukwepa mtego wa CCM wa kuwachagulia hayo maboya unayoyasema. Strategy nzuri ni hii waliyoitumia kuliko ile ya kwako ambayo ingewaingiza choo cha kike asubuhi mapema. Kuwaweka Masha, Wenje pamoja na maboya ingewasaidia CCM kupigia kura maboya. Umeona kwa CUF walichokifanya-CCM wameamua "kumchagua Lipumba" kwa makusudi ili kunogesha mgogoro ndani ya chama hicho, na kwa CDM ambacho wangekifanya ni kuchagua maboya.

Tuwaache CDM wapambane na mkakati ovu wa CCM kutaka taifa lipeleke EALA maboya. Hizo kanuni za uchaguzi zinaelekeza wabunge kupiga kura za hapana? Zianzie kwa Masha na Wenje? Kwamba Masha na Wenje hawawezi kutoa uwakilishi mzuri wa Tanzania EALA tukilinganisha na wale waliopitishwa na CCM?

Unahoji Masha na Wenje wamepatikanaje lakini CDM wenyewe wameeleza kuwa walikuwa na wagombea 17 na mchakato ukawapa nafasi hao wawili. Lakini inashangaza pia mtu wa aina yako kulipa uzito suala la Masha na Wenje (ambao ni wanachama halali wa CDM) kuwa wamepatikanaje ndani ya chama badala ya uwezo wao kama wawakilishi wa nchi katika EALA! Hili jingine unalowataka CDM washughulike nalo-"kumshtaki mvunja nchi"/suala la katiba. Hili sio la CDM peke yake bali ni pamoja na wewe kama mwananchi. Labda utuambie wewe umefanya nini katika hili ukiacha kumuuliza swali Rais ambaye aliishia kukuambia jina la ubini wako maana yake ni njaa?
 
BAK Matusi ya nini sasa? Tumia hoja, kama umeshindwa futa uzi wako. Usikimbilie kuanzisha mada tuuu wakati hata kuitetea huwezi... :D:D:D
Nakuunga mkono Gragoon,
Hapa hatutakiwi kurushiana matusi na ndio maana likaitwa jukwaa la GTs, uko sawa kabisa kuwa tulete hoja na tuzichambue na yote iwe kwa mstakabari wa nchi yetu.
Dragoon, nisaidie tu kuelewa au tufanye wewe ni mmoja wa wapiga kura wa jana. Lengo ilikuwa kutafuta nini pale?
Naomba mie nitoe uelewa wangu then na wewe utakuja na udadavuzi wako katika hili,
Nilifikiria walikuwa wanatafutwa wawakili wa Tanzania ndani ya bunge la Afrika Mashariki na wawakilishi wa CCM ndani ya bunge la Afrika Mashariki.
Sasa,hebu tuwe wawazi, yes kura ni utashi wa mpiga kura hilo halipingiki na ni sawa kumpigia umtakaye

Unaweza kukubariana na mimi kuwa rafiki zetu wabunge wa CCM halikuwa kimkakati wa kuwa CDM na CUF- Maalimu Seif waambulie patupu?
Hata kama uliwasikiliza hoja zilizokuwa zikitolewa wakati wa mabishano ya kikanuni za upigwaji wa kura mtu unakata tamaa ya kuwa tuna wawakilishi wa namna hiyo kweli tutegemee taifa kusonga mbele!!!
 
Mambo yaliyofanyika kwenye uchaguzi wa wabunge wa EALA ni ushahidi kwamba wanaccm wote wanaburuzwa na mtu mmoja tu.

Wabunge wa chama hiki si wa kushirikiana nao katika jambo lolote , iwe la heri au la shari , kwao siasa ni uadui na ni vita kamili , hakuna haja yoyote ya ushirikiano .

Hata kwenye kamati za bunge , kuweni makini sana na wabunge wa ccm na mamluki wao , hakuna sababu yoyote ile ya kushirikiana na wabunge ambao maamuzi yao yanatoka Lumumba .

CCM inafanya siasa za kishamba sana .
 
Mambo yaliyofanyika kwenye uchaguzi wa wabunge wa EALA ni ushahidi kwamba wanaccm wote wanaburuzwa na mtu mmoja tu.

Wabunge wa chama hiki si wa kushirikiana nao katika jambo lolote , iwe la heri au la shari , kwao siasa ni uadui na ni vita kamili , hakuna haja yoyote ya ushirikiano .


Nilifikiri walikuwa (chadema) wamepanga kupiga kura ya kutokuwa na Imani na Raisi wetu, vipi yamekuwa hayo tena? Kwa maana kura zao 30 chadema hazitoshi, bado wanahitaji na za CCM!
 
Nilifikiri walikuwa (chadema) wamepanga kupiga kura ya kutokuwa na Imani na Raisi wetu, vipi yamekuwa hayo tena? Kwa maana kura zao 30 chadema hazitoshi, bado wanahitaji na za CCM!
Tutatumia njia mbadala , kuna lundo la njia za kutumia .
 
We jamaakweli Toilet paper ya DJ. Yaani upuuzi anao ufanya DJ una thubutu kuunga mkono?
 
Mkuu Paskali, unaweza usikubaliane na mimi lakini ukweli ni kwamba hiki ulichokiandika hapa kinaonyesha unakubaliana moja kwa moja na mkakati wa CDM na wala kumbe huna sababu hata kiduchu ya kuwabeza. CDM wanajaribu kuukwepa mtego wa CCM wa kuwachagulia hayo maboya unayoyasema. Strategy nzuri ni hii waliyoitumia kuliko ile ya kwako ambayo ingewaingiza choo cha kike asubuhi mapema. Kuwaweka Masha, Wenje pamoja na maboya ingewasaidia CCM kupigia kura maboya. Umeona kwa CUF walichokifanya-CCM wameamua "kumchagua Lipumba" kwa makusudi ili kunogesha mgogoro ndani ya chama hicho, na kwa CDM ambacho wangekifanya ni kuchagua maboya.

Tuwaache CDM wapambane na mkakati ovu wa CCM kutaka taifa lipeleke EALA maboya. Hizo kanuni za uchaguzi zinaelekeza wabunge kupiga kura za hapana? Zianzie kwa Masha na Wenje? Kwamba Masha na Wenje hawawezi kutoa uwakilishi mzuri wa Tanzania EALA tukilinganisha na wale waliopitishwa na CCM?

Unahoji Masha na Wenje wamepatikanaje lakini CDM wenyewe wameeleza kuwa walikuwa na wagombea 17 na mchakato ukawapa nafasi hao wawili. Lakini inashangaza pia mtu wa aina yako kulipa uzito suala la Masha na Wenje (ambao ni wanachama halali wa CDM) kuwa wamepatikanaje ndani ya chama badala ya uwezo wao kama wawakilishi wa nchi katika EALA! Hili jingine unalowataka CDM washughulike nalo-"kumshtaki mvunja nchi"/suala la katiba. Hili sio la CDM peke yake bali ni pamoja na wewe kama mwananchi. Labda utuambie wewe umefanya nini katika hili ukiacha kumuuliza swali Rais ambaye aliishia kukuambia jina la ubini wako maana yake ni njaa?
Mkuu Chabusalu, kwanza nimependa ujengaji hoja wako la logic na objectivity ya bandiko post yako.

Naamini Chadema ingefuata kanuni na taratibu, CCM wangewachagua hao hao.

Utekelezaji wa kanuni unataka maandishi na sio kauli. Hili la kuambiwa kwa kauli tuu halina mashiko.

Kesi ya mvunja katiba ninachofanya mimi ni kile tuu kilicho ndani ya uwezo wangu, kama mwandishi kazi yangu ni kuuliza tuu na kuandika, na inawezekana kabisa mimi nikawa ni miongoni wa watu wa mwanzo kabisa humu jf kutoa angalizo la udikiteta wa mvunja katiba. Nimeandika nyuzi zaidi yards 20 kuhusu huu udikiteta. That is the best I can do.

My surprise ni concentration ya non issues na kuachana na issues.
Paskali
 
Mkuu Chabusalu, kwanza nimependa ujengaji hoja wako la logic na objectivity ya bandiko post yako.

Naamini Chadema ingefuata kanuni na taratibu, CCM wangewachagua hao hao.

Utekelezaji wa kanuni unataka maandishi na sio kauli. Hili la kuambiwa kwa kauli tuu halina mashiko.

Kesi ya mvunja katiba ninachofanya mimi ni kile tuu kilicho ndani ya uwezo wangu, kama mwandishi kazi yangu ni kuuliza tuu na kuandika, na inawezekana kabisa mimi nikawa ni miongoni wa watu wa mwanzo kabisa humu jf kutoa angalizo la udikiteta wa mvunja katiba. Nimeandika nyuzi zaidi yards 20 kuhusu huu udikiteta. That is the best I can do.

My surprise ni concentration ya non issues na kuachana na issues.
Paskali
Nikubaliane na wewe kwamba suprise yako ni concentration ya non issues na kuachana na issues , nikuombe na wewe ukubaliane na mimi kwamba wakati mwingine kwa CDM kama taasisi yenye malengo zile ambazo kwako ni non issues zinaweza kuwa ni nazo ni issues! Na kama utakubaliana na mimi katika hili, bila shaka utaunga mkono mpango wa CDM kwenda kortini.
 
Mimi naona kuna baadhi ya mambo yanafanyika kana kwamba chama kina lengo la kujenga taasisi ya kisheria zaidi badala ya kisiasa. Na kikiendelea hivi bila ya kuwa tunarejea tunapokosea huenda kweli tukafanikiwa sana upande wa kisheria (kwa kutangaza wanasheria wetu na kuwapa uwanja wa kuapply taaluma yao) hali ya kuwa tukisahau upande wa pili ambao ndio lengo letu. Tujijenge kisiasa zaidi na taratibu za maamuzi ya chama zijikite katika falsafa ya chama (Demokrasia na maendeleo).

Political strategy ya chama iangaliwe vema! Kuna ambao hawatanielewa, lkn tujisahihishe ili kujikita zaidi ktk mambo ya siasa bila ya kudharau sharia; na siyo kinyume chake.
 
Hii chuki inayowasumbua CCM dhidi ya CDM ni ya nini hata kwa kitu cha halali?! CCM wanadai kukomaa kisiasa lakini naona wanasumbuliwa wivu wa kike usiokuwa na faida. Si mara ya kwanza wana CCM kuifanyia CDM visa dhidi ya wajumbe wake ili wasiende EALA !!! Ni kama vile wanaona ni haramu CDM kwenda ktk taasisi za kimataifa hata kama ni haki ya ki katiba !! Hii ni zaidi ya wivu wa kike na haina faida
Kidogo umenena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom