Mbowe atangaza maandamano nchi nzima

Hayo ameyasema ktk mkutano uliofanyika viwanja vya barafu mkoani Dodoma wakati akiwatambulisha wabunge wapya watakaoapishwa kesho. Akitoa kauli hiyo iliyoungwa mkono na maelfu ya wakazi wa Dom waliohudhuria mkutano huo amesema maandamano yataanzia Shinyanga, mwanza, Tabora, Dodoma, Arusha na mikoa mingine. Amesema nanukuu "hii mijamaa bila maandamano haisikii". Amesema tutafanya uasi kwasababu tunazo sababu za kufanya uasi.

ataandamana na mkewe, watu tuna kazi za kufanya. Yeye si anauza bar? Halafu anataka kuandamana ili auze na magazeti, mimi je?
 
Naunga mkono uasi kwa asilimia mia. Ikiwa serikali kupitia dola yaani polisi wameamua kuwaweka wabunge kati na kuamuru wacharangwe mapanga, huo ndio msingi wa kuondoka rasmi kwenye utawala wa sheria. Hivyo kwa kuwa hakuna tena chombo cha kusimamia utekelezaji wa sheria ni budi kila mtu au kundi kufanya lile wanaloona linafaa kujilinda bila kutegemea tena muongozo wa serikali, maana imejidhihirisha kupoteza uhalali wa kutuongoza. Polisi sasa kageuka kuwa adui namba moja wa haki za uhai wetu na mali yetu. Mahakama nayo imekuwa chombo cha kutumiwa na watawala kudhulumu haki ya raia zake. Serikali imetufikisha katika kona ambayo haina pa kutokea ila kuasi.
.

acha bangi, jaribu mirungi kichwa itakua sawa
 
Nyie mnaojifanya wasomi hamtaki maandamano ya Amani mmewahi kufanya nini na huo usom wenu "wakisenge" msipende kukandamiza mawazo ya watu kama unaona haifai funga mdomo wako kaa na ajanja wako waache watu na ujinga wao.

Mmmh!!! Hayo majibu vp!! ni siasa tu au kuna jingine. Matusi, hasira vya nini?
 
What the hell is this. Kumpeleka mwanao shule ni jambo zuri sana. Hizi vurugu za maandamano kila siku zinatokana na watu kukosa shule ya kutosha. Mbowe, tunakuheshimu sana, usiwe chanzo cha kuleta machafuko hapa nchini.
Naona umerudi baada ya kile kichapo cha Arumeru.
 
What the hell is this. Kumpeleka mwanao shule ni jambo zuri sana. Hizi vurugu za maandamano kila siku zinatokana na watu kukosa shule ya kutosha. Mbowe, tunakuheshimu sana, usiwe chanzo cha kuleta machafuko hapa nchini.
Wewe unayekosoa shule za wengine umesoma mpaka? hata post zako hapa JF zinadhihirisha kiwango chako cha elimu!!
 
Ninavyo elewa maandamano haya nchi nzima ni kwa ajili ya wabunge waliocharazwa mapanga mbele ya polisi. Kama ni kwa ajili hiyo sawa kabisa na hakuna uhaini katika hilo.
 
Mbowe anataka maandamano kutokana na kauli ya mkwewe? kuwa eti waislaam wengi tume ya katiba.
 
[/B].
Kufanya uasi tena,mbona sijaelewa hapo? maana uasi ninao ujua mimi ni wa ama wa kujitenga na kutaka kuanzisha eneo la utawala na ama kutaka kuipundua serikali na kujitwalia madaraka kwa njia ya mapambano/vita.Sasa labda mdau utusaidie kufafanua ni uasi gani huo aliouzungumzia mh.Mbowe? kama ni suala la kuandamana nchi nzima kwangu huo sio uasi, bali ni utaraibu wa kawaida tu katika nchi zinazojali demokrasia ili wahusika waweze kufikisha ujumbe wanoataka kuufikisha kwa jamii husika.Ufafanuzi tafadhali!!!
Mbowe hakuchanganya maandamano na uasi,ila katika kuongea alisema lazima tufanye uasi mpaka kieleweke,na akazid kusema tutafanya uasi kwa sbbu sababu tunazo na hayo aliyasema kwa uchungu bada ya mbunge machemli kumaliza kutoa ushuhuda wake wa kukatwa mapanga.

Hayo maandamano alisema hawa jamaa bila maandamano hawafany lolote akatoa mfano waliandamana kudai katiba mikoa michache akaitaja Kagera,mwanza,mbeya,arusha,moshi,tabora,dodoma kidogo wakatoa katiba ila hakutangaza kama jamaa anavyosema.
 
Ninavyo elewa maandamano haya nchi nzima ni kwa ajili ya wabunge waliocharazwa mapanga mbele ya polisi. Kama ni kwa ajili hiyo sawa kabisa na hakuna uhaini katika hilo.
Wabunge wote wataenda mwanza bada ya bunge kuisha,wataenda kuandamana huko mwanza kushinikiza hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi ya waliohusika na kuwakata mapanga wabunge wawili.
 
Hayo ameyasema ktk mkutano uliofanyika viwanja vya barafu mkoani Dodoma wakati akiwatambulisha wabunge wapya watakaoapishwa kesho. Akitoa kauli hiyo iliyoungwa mkono na maelfu ya wakazi wa Dom waliohudhuria mkutano huo amesema maandamano yataanzia Shinyanga, mwanza, Tabora, Dodoma, Arusha na mikoa mingine. Amesema nanukuu "hii mijamaa bila maandamano haisikii". Amesema tutafanya uasi kwasababu tunazo sababu za kufanya uasi.
Kaka ulichokinukuu si kweli,hakutangaza mgomo bali alitaja hyo mikoa ambyo walifanya maandamano kudai katiba mpya.Naomba uedit thread yako.
 
Mbowe anapenda sana sifa,yeye akiona watu wengi,anadhan watamsapot kw pumba zake,anasema hadharani kuwa yeye atakuwa mtu wa kwanza kuongoza UASI hapa nchini,hapa kuna tatizo,siamini kama huo ndio msimamo wa chadema,au ndio zidumu fikra za mwenyekiti..polisi fanyeni kazi yenu.
 
What the hell is this. Kumpeleka mwanao shule ni jambo zuri sana. Hizi vurugu za maandamano kila siku zinatokana na watu kukosa shule ya kutosha. Mbowe, tunakuheshimu sana, usiwe chanzo cha kuleta machafuko hapa nchini.
Kwahiyo tushabikie wizi wenu wa kodi na rasilimali zetu?
 
Sababu hasa alizotoa hadi watu kuandamana nchi nzima ni zipi maana hawezi kutangaza tu kuwa kuwe na maandamano nchi nzima,jaribu kuwapa wadau nini hasa wananchi waunge maandamano maana kama ni uongozi mbaya w taifa hili upo na hakuna namna ya kuubadlisha hadi 2015 watanzania wakielewa zaidi watabaki kuwa wa hivhivi.
 
Back
Top Bottom