Mbowe amvaa Kikwete

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,013
Mbowe amvaa Kikwete

• Ambeza kutangaza kufunga mjadala wa Dowans

na Edward Kinabo
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amemtaka Rais Jakaya Kikwete, kutofunga mjadala wa suala la mitambo ya kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura, Dowans, bila kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu wamiliki wake na mahala walipo.

Mbowe aliyasema hayo jana katika mahojiano maalum na Tanzania Daima, akitoa maoni yake kuhusu baadhi ya masuala aliyoyazungumza Rais Kikwete juzi usiku, wakati akilihutubia taifa kwa njia ya redio na televisheni.

Alisema hatua ya Rais Kikwete kutangaza kufunga mjadala wa Dowans ni ya kuungwa mkono kwa kuwa mjadala huo si jibu la matatizo ya umeme nchini, lakini alimtaka kwanza awaeleze Watanzania ukweli wote kuhusu Kampuni ya Dowans, ndipo aufunge mjadala huo vizuri.

“Tunakubaliana na ushauri wake wa kutaka mjadala wa Dowans uishe. Tunakubaliana naye kwa sababu Dowans si jibu la matatizo ya msingi ya sekta ya nishati nchini. Hata hivyo, Kikwete asikimbilie kufunga mjadala bila kuwaeleza wananchi, Dowans ni nani. Watoe tamko, waueleze umma wa Watanzania, wamiliki wa Dowans ni nani, wako wapi, wanafanya nini, wataje watu wote wanaonufaika na Dowans, kisha ndipo atufungie mjadala huo vizuri. Kikwete anataka kuficha ukweli,” alisema Mbowe.


Akizungumzia tatizo la uhaba wa umeme nchini, alisema si mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kuahidi kumaliza tatizo la umeme, kwani wakati wa sakata la kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, alishaahidi kuwa tatizo la umeme lingekuwa historia.

“Si mara ya kwanza rais kuahidi kwamba nchi haitakuwa gizani. Ameshaahidi hivyo wakati wa vuta nikuvute ya Richmond, ameshasema hivyo karibu mara tatu. Alishasema kwamba matatizo ya umeme yatakuwa historia, lakini hadi leo nchi haina umeme wa uhakika. Rais anaendelea kutoa maneno matamu, hatuwezi kupata umeme kwa maneno yake….”

“Asitazame tu uchaguzi wa 2010, na kuwapa watu maneno matamu, atazame mbele. Tunahitaji mkakati wa muda mrefu na mfupi. Na si mkakati tu, tunahitaji mpango wa utekelezaji, maana sera ya nishati imeainisha yote hayo, lakini tatizo utekelezaji. Serikali inapaswa kuwa na uhakika wa kulipatia taifa umeme hata kwa miaka zaidi ya 50 ijayo,” alisema Mbowe.


Alisema kwa kiasi kikubwa sekta ya umeme nchini inaathiriwa na wafanyabiashara wakubwa ambao ni maswahiba wa Rais Kikwete na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaoigeuza sekta hiyo kuwa chanzo chao cha mapato, kwa kuanzisha kampuni za kufua umeme wa dharura na kuiuzia TANESCO kwa gharama kubwa.

Alisisitiza kuwa, msingi wa tatizo la nishati ya umeme nchini ni kutokuwapo kwa sera endelevu na mikakati yakinifu na inayotekelezeka, ya muda mrefu na mfupi, ya kuzalisha na kusambaza umeme.

Alisema pamoja na uhaba wa umeme unaozalishwa, bado sehemu kubwa ya umeme huo imekuwa ikiibwa na kusababisha wananchi wengi kukosa haki ya kupata umeme.

“Na tatizo hapa si uhaba wa umeme unaozalishwa tu. Bado kuna umeme mwingi sana unaibwa, lakini serikali halizungumzii hili,” alisema Mbowe.

Alisema tatizo jingine ni umeme unaozalishwa kuwa wa gharama kubwa kiasi cha wananchi wengi kushindwa kuupata na kuutumia.

“Tuna network (mtandao) kubwa sana ya umeme. Maeneo mengi nyaya za umeme zinapita jirani na nyumba za watu, lakini wenye uwezo wa kuunganisha umeme huo kwenye nyumba zao ni wachache sana. Gharama za kufunga umeme majumbani ni kubwa mno kwa Mtanzania maskini kumudu. Gharama za kuutumia, kulipa ankara pia ni kubwa.

“Kwa hiyo Rais Kikwete na serikali yake, wasiishie tu kuzungumzia uzalishaji, lakini pia lazima waeleze ni jinsi gani watapunguza gharama za umeme ili Watanzania maskini nao waweze kuutumia,” alisema Mbowe.


Akizungumzia tahadhari ya Rais Kikwete, kwamba kwenye baadhi ya mikoa kuna uwezekano wa kutokea tatizo la chakula kwa sababu ya kuchelewa kwa mvua za masika, Mbowe alisema ni aibu na fedheha kubwa kwa nchi yenye maji mengi yanayotiririka kama Tanzania, kutangaza njaa ndani ya msimu mmoja wa matatizo ya mvua.

“Sikio la kufa halisikii dawa. Tatizo la chakula ni tatizo la kujitakia. Kukosa mvua msimu mmoja, halafu rais anatangaza njaa, ni jambo la kutia aibu sana. Tuna maji mengi sana yanatiririka, tuna mito na maziwa, ardhi yenye rutuba nzuri sana. Tuna kila kitu, tatizo ni ukosefu wa sera nzuri na uongozi bora,” alisema Mbowe.

Alisema Rais Kikwete anapaswa kumfukuza mara moja Waziri wake wa Kilimo na Chakula kwa kushindwa kusimamia programu za kilimo cha uwagiliaji nchini.

“Walipoingia madarakani walikutana na tatizo la chakula. Kikwete na Lowassa waligawa chakula na kuahidi kwamba njaa ile isingetokea tena, sasa leo wanatuambia nini? Wamefanya nini? Na hii ndiyo kawaida yake, anaahidi halafu anasahau. Nchi hii ikipata viongozi wazuri serikalini, kilimo cha umwagiliaji kinaweza kabisa kumaliza tatizo la njaa za mara kwa mara,” alisema Mbowe.

Alisema serikali inapaswa kuwa na mpango wa makusudi wa muda mrefu wa kuzalisha na kuhifadhi chakula kwa wingi, ili kiwe kinaingia katika mtandao wa matumizi ya wananchi, pindi kunapokuwa na uhaba wa chakula.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi uliopita, Rais Kikwete pamoja na mambo mengine, alitaka mjadala wa kununua au kutonunua mitambo ya Dowans, ufungwe baada ya wahusika (TANESCO), kutangaza kuachana na uamuzi wa kutaka kuinunua.

Alisema anashangazwa na malumbano ya baadhi ya viongozi wa siasa kuhusu jambo hilo.

Mjadala wa Dowans, hivi karibuni uliwaingiza katika malumbano makali, Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wote wa CCM.
 
Si kazi ya Rais kutangaza kampuni ya nani! huyu mbowe ana nini, BRELA hapajui?
 
Si kazi ya Rais kutangaza kampuni ya nani! huyu mbowe ana nini, BRELA hapajui?

Ila ni kazi yake kufunga mjadala pamoja na kuwa bado kuna maswali chungu nzima ambayo hayajajibiwa likiwemo la wewe fisadi RA kurudisha bilioni 23 ambazo ulikabidhiwa na serikali ili kukusaidia kuleta ile mitambo michakavu!!!! We kweli ni fisadi wa hali ya juu lakini hapa JF tutakula nawe sahani moja
 
Advise your boss that we need to know more regarding this Dowans fiasco before the matter can be laid to rest..
 
Hata kama si kazi ya raisi kwanini anaufunga mjadala hayamuhusu pia kufunga mjadala huo auche mpaka uishe

wacha na Dr Slaa ajisemee ukweli wake tunataka watu kama hawa wataikomboa nchi yetu

JF Kama kawaida
 
Ila ni kazi yake kufunga mjadala pamoja na kuwa bado kuna maswali chungu nzima ambayo hayajajibiwa likiwemo la wewe fisadi RA kurudisha bilioni 23 ambazo ulikabidhiwa na serikali ili kukusaidia kuleta ile mitambo michakavu!!!! We kweli ni fisadi wa hali ya juu lakini hapa JF tutakula nawe sahani moja

- Mkuu acha name calling, kata ishu tu maana ninajua kua unaweza tena big time, nia na madhumuni ni kuwa na mawazo mbadala badala ya wote kufuata bendera, only through malumbano ndio tutajua ukweli,

- Lakini haipendezi kuwemo na name calling, tunachojaribu hapa ni kupata the truth na nothing but the whole truth, through malumbano na tumekubaliana sana kwamba hatujuani, ni suala dogo tu la kuheshimu mawazo tofauti na yako lakini kusimamia unachoamini kwamba ni ukweli on the ishu kwa kupanga hoja, kwa sababu mimi siamini for a minute kwamba unatumwa na rais wangu Dr. Slaa, na sina sababu yoyote ya kuamini kwamba Mkulu Dar, anatumwa na mafisadi, kwa kweli it is unfair na his name calling.

- Haiwezekani wote hapa tukawa na mawazo sawa, na ikitokea hii tabia ikataliwe kwa nguvu zote kwa sababu ndio imetufikisha hapa as a nation, yaani pabaya!

Respect!

FMES
 
Nimekubali maneno ya Mbowe ni ukweli kabsa

SASA WANA JF MNASEMAJE?

Thanks BABU
 
Ila ni kazi yake kufunga mjadala pamoja na kuwa bado kuna maswali chungu nzima ambayo hayajajibiwa likiwemo la wewe fisadi RA kurudisha bilioni 23 ambazo ulikabidhiwa na serikali ili kukusaidia kuleta ile mitambo michakavu!!!! We kweli ni fisadi wa hali ya juu lakini hapa JF tutakula nawe sahani moja

Ningekuwa na fedha hiyo ungeniona humu, hiyo minoti ningeitengeneza godoro, mito, makochi, badala ya kutumia sponchi na pamba. Duhh, dua yako iwe ya kweri nami nikumbane na minoti japo 1% ya hiyo.

RA anawashinda ujanja hasira zako umtolee Mzee Dar. Duhhh, wewe una agenda ya siri nini?

Mie nashangaa, leo hii Mbowe wacha ya yeye kwenda BRELA hata akikuagiza wewe tu, si utampa hiyo information.

Yes, JMK as President of Tanzania and as Chairman of CCM ana haki ya kutowa wazo la kufunga huo mjadala, na anaetaka kuuendeleza pia ana haki ya uhuru wa maoni na mawazo.

Sasa basi hili la kupatiwa jibu na BRELA anamtaka Rais amsaidie, sasa huu kama si upunguwani ni nini?
 
Last edited by a moderator:
- Mkuu acha name calling, kata ishu tu maana ninajua kua unaweza tena big time, nia na madhumuni ni kuwa na mawazo mbadala badala ya wote kufuata bendera, only through malumbano ndio tutajua ukweli,

- Lakini haipendezi kuwemo na name calling, tunachojaribu hapa ni kupata the truth na nothing but the whole truth, through malumbano na tumekubaliana sana kwamba hatujuani, ni suala dogo tu la kuheshimu mawazo tofauti na yako lakini kusimamia unachoamini kwamba ni ukweli on the ishu kwa kupanga hoja, kwa sababu mimi siamini for a minute kwamba unatumwa na rais wangu Dr. Slaa, na sina sababu yoyote ya kuamini kwamba Mkulu Dar, anatumwa na mafisadi, kwa kweli it is unfair na his name calling.

- Haiwezekani wote hapa tukawa na mawazo sawa, na ikitokea hii tabia ikataliwe kwa nguvu zote kwa sababu ndio imetufikisha hapa as a nation, yaani pabaya!

Respect!

FMES


Yes Dat is True malumbano na hoja za kweli ndio zitatupa jibu kamili
 
Si kazi ya Rais kutangaza kampuni ya nani! huyu mbowe ana nini, BRELA hapajui?

Former Presendent Mkapa, ndie mwanzilishi wa hotuba za mwisho wa mwezi. Lengo likiwa ni pamoja na kutoa updates ya critical issues zilizojili pamoja na kuclear doubts fulani miongoni mwa wananchi. Katika vitu and mhimu alivyorithi JK kwa Mkapa japo kashindwa kutimiza ipasavyo ni swala hili la hotuba za mwisho wa mwezi. Mkuu, issue inayo husu grand corruption no way rais asikizungumzie. Hatakama watu wengine watakizungumzia anatakiwa pia japo kuhighligh kuonyesha yupo pamoja nao. Hivyo ni wajibu wake.
 
Former Presendent Mkapa, ndie mwanzilishi wa hotuba za mwisho wa mwezi. Lengo likiwa ni pamoja na kutoa updates ya critical issues zilizojili pamoja na kuclear doubts fulani miongoni mwa wananchi. Katika vitu and mhimu alivyorithi JK kwa Mkapa japo kashindwa kutimiza ipasavyo ni swala hili la hotuba za mwisho wa mwezi. Mkuu, issue inayo husu grand corruption no way rais asikizungumzie. Hatakama watu wengine watakizungumzia anatakiwa pia japo kuhighligh kuonyesha yupo pamoja nao. Hivyo ni wajibu wake.

Yote uliyosema ni swadakta kabisa wala sina ubishi nayo ila naomba na wewe nielewe, japo kidogo. Nnachosema mimi ni, ''BRELA'' si ndio kuna data za usajili wa makampuni? sasa vipi mtu kama Mbowe amuulize Rais? kitu ambacho kipo wazi kabisa, si aende BRELA tu.
 
Ningekuwa na fedha hiyo ungeniona humu, hiyo minoti ningeitengeneza godoro, mito, makochi, badala ya kutumia sponchi na pamba. Duhh, dua yako iwe ya kweri nami nikumbane na minoti japo 1% ya hiyo.

RA anawashinda ujanja hasira zako umtolee Mzee Dar. Duhhh, wewe una agenda ya siri nini?

Mie nashangaa, leo hii Mbowe wacha ya yeye kwenda BRELA hata akikuagiza wewe tu, si utampa hiyo information.

Yes, JMK as President of Tanzania and as Chairman of CCM ana haki ya kutowa wazo la kufunga huo mjadala, na anaetaka kuuendeleza pia ana haki ya uhuru wa maoni na mawazo.

Sasa basi hili la kupatiwa jibu na BRELA anamtaka Rais amsaidie, sasa huu kama si upunguwani ni nini?

Kwa nini twenda Brela wakati raisi ana majibu yote? nina haja gani ya kufunga safari wakati naweza kupata kwa mwenye jibu?
Raisi ana majibu ya dowans ni nani bwana Dar!
 
Yote uliyosema ni swadakta kabisa wala sina ubishi nayo ila naomba na wewe nielewe, japo kidogo. Nnachosema mimi ni, ''BRELA'' si ndio kuna data za usajili wa makampuni? sasa vipi mtu kama Mbowe amuulize Rais? kitu ambacho kipo wazi kabisa, si aende BRELA tu.

Ukienda BRELA kuangalia wamiliki wa New Habari Corporation hutamkuta Rostam Aziz. Lakini ukimuuliza swahiba wake Kikwete nani ni mmiliki wa hiyo kampuni atakwambia ni Rostam. Sasa Mbowe anamuuliza nani ni mmiliki wa Dowans iliyorithi mkataba toka Richmond, kwa kuwa ni maswahiba wa Kikwete-atoe jibu badala ya Mbowe kwenda Brela ambapo hatapata wamiliki wenyewe!

Ukienda BRELA utakuta wamiliki tofauti wa Kagoda, lakini imeelezwa wazi kuwa Rostam ndio mmiliki ya fedha zilikuwa ni za kampeni za swahiba wake Kikwete. Sasa kwanini Kikwete asiulizwe?

Asha
 
Ukienda BRELA kuangalia wamiliki wa New Habari Corporation hutamkuta Rostam Aziz. Lakini ukimuuliza swahiba wake Kikwete nani ni mmiliki wa hiyo kampuni atakwambia ni Rostam. Sasa Mbowe anamuuliza nani ni mmiliki wa Dowans iliyorithi mkataba toka Richmond, kwa kuwa ni maswahiba wa Kikwete-atoe jibu badala ya Mbowe kwenda Brela ambapo hatapata wamiliki wenyewe!

Ukienda BRELA utakuta wamiliki tofauti wa Kagoda, lakini imeelezwa wazi kuwa Rostam ndio mmiliki ya fedha zilikuwa ni za kampeni za swahiba wake Kikwete. Sasa kwanini Kikwete asiulizwe?

Asha

BRELA unaweza ukakuta miliki ni ya kampuni kumiliki kampuni na ukifatilia mwisho wake utajuwa ni nani mmiliki wa kweli, kwani hata kama mmiliki wa kampuni fulani ni kampuni zingine lazima kuna signatories, lazima kuna uwezekano wa kujuwa ni kampuni ya nani, na kama unanambia BRELA hawana uwezo wa kujuwa kampuni zinazosajiliwa kwao, basi ya nini kuwa na chombo kama hicho?

Hicho cha kuelezwa wazi bila kuwa na ushahidi wowote, aaah, ni mengi tu yanaelezwa lakini hakuna cha kuweza kumtia hatiani mpaka sasa, kama kipo tunangija nini? offer nimeshatowa, nitafutieni proof mimi ntakwenda kushitaki!

Hili la kuulizwa JMK siafikiani nalo hata kidogo wala haliingii akilini, hizo zitakuwa ni chuki binafsi au kutafuta umaarufu kwa kutumia jina la JMK! mnanishangaza sana mnapomtaka Rais aanze kazi ya BRELA. Na huyo aliyetowa rai hiyo (Mbowe) naona hajafanya homework yake, amekurupuka tu na kutaka ajipatie umaarufu kwa kutumia njia ya mkato.

Sasa ukikuta wamiliki tofauti wa Kagoda ndio imeshakuwa ya RA? mbona sikuelewi?
 
Kwa nini twenda Brela wakati raisi ana majibu yote? nina haja gani ya kufunga safari wakati naweza kupata kwa mwenye jibu?
Raisi ana majibu ya dowans ni nani bwana Dar!

Kuna thread humu JF inaonyesha wamiliki wa Dowans, sasa ikiwa hata wana JF wanaweza kulipata hilo na katika hiyo thread kuna scanned documents zilizobandikwa, naomba zitafute (humu humu JF) na utuambie ni kina nani wamiliki wa Dowans kwa mujibu wa hizo documents? na kama mpaka JF zimo kuna umuhimu wa kutaka Rais aulizwe? si upunguani huu jamani! Kuzithibitisha si unaenda BRELA tu au kama hutaki kwenda si unawaandikia tu! hivi kwa akili yako haswa, JMK ana time ya kukujibu BRELA ni ya nani? na hata kwa mfano atakujibu si wasaidizi wake watakuletea data hizo hizo za BRELA. Au?

Hivi nyinyi hamjaona kuwa alichofanya Mbowe ni kutaka kujipatia umaarufu tukielekea 2010 kupitia JMK kwa kuuliza hilo? halina mantiki wala maana. Lakini namsifu (Mbowe) kwa kuwa mbunifu na kujuwa kuwa hapa kuna njia ya mkato (JMK) ya kujipatia umaarufu tukielekea 2010, kwa hiyo anajaribu kutumia vyema ubunifu wake, na nnashangaa wengi hatulioni hilo! kwa Mbowe kuwa sharp na kuliona hilo anastahili sifa.
 
Back
Top Bottom