Mbinu chafu za serikali kuficha ukweli juu ya Dr. Ulimboka

kuna mbinu chafu zinapangwa katika kuficha ukweli wa kile kilichotokea kwa dr. Ulimboka. Mbinu hizi zinalenga kuficha maovu yaliyofanywa na serikali kwa dr ulimboka na hivyo kuisafisha serikali ili ionekane kuwa haihusiki na unyama huu.

Mtu aliyekuwa anajitambulsha kwa dr. Ulimboka na kuwa na mawasilinao nae kwa mda mrefu akitumia jina la abduel (si jina lake halisi na wengine humuita abedi) alikabidhiwa kazi ya kumfatilia dr ulimboka siku mbili baada ya waziri mkuu pinda kwenda kuonana na madaktari pale muhimbili. Kitu cha kwanza alichofanya ni kujiweka karibu na ulimboka katika kuzungumzia matatizo yao lakini pia huyu jamaa alikuwa link kati ya ulimboka na serikali. Katika kipindi chote hicho mwanausalama huyu likuwa akimfatilia ulimboka ili kumjua kwa undani zaidi.

Baada ya kuona msimamo wa dr ulimboka juu ya swala hili la madaktari hautetereki na habadiri msimamo wake maana walishataka kumpatia pesa ili anyamaze ; ndipo sasa maandalizi ya kumnyamazisha kwa kutumia formula ya ’’ maiti haisemi’’ yalianza. Lengo lilikuwa ni kumuua kabisa na hiyo juzi walidhani wamemuua.wazo la kumnyamazisha jumla ulimboka halikutoka kwa huyo mwana usalama bali nae alipokea maelezo toka juu kwa watawala. Mpango wa kutekwa ulimboka ulipangwa na kitengo anachofanyia kazi mwana usalama huyo na kutekelezwa na maafisa wapolisi waliokabidhiwa jukumu hilo.

Mbinu chafu
baada ya kufanikiwa kumteka na kumpiga vibaya dr ulimboka na hatimae kumtupa huko msitu wa pande huku wakidhani tayari adhma imetimia ya kumtoa uhai sasa serikali dhaifu imepanga mipango michafu ili kujisafisha ili isionekane kuwa imehusika na unyama huu.

1. Abduel amesafirishwa na kuondolewa nchini tanzania usiku wa tarehe 27 kwa kupita nairobi na baadae ataelekea kwenye ubalozi wa afrika ya kusini atakapopangiwa majukumu mengine. Hii yote ni katika kuficha ukweli . Hao maafisa wa polisi watano waliomteka ulimboka wapo nchini na mmoja amewekwa kwenye tume ya kuchunguza utekwaji nyara wake iliyoundwa na kova nahii imefanywa makusudi kwa malengo flani; wanne waliobaki wamesambazwa kwenda mikoan na hawapo dar.

2. Kamanda wa polisi kova ameelekezwa kuhakikisha anailinda serikali katika jambo hili na afanye awezalo kuonyesha umma wawatanzia kuwa serikali haihusiki na jambo hili.katika kuficha na kuilinda serikali kova, mwema na maafisa wa wajuu wa usalama wa taifa walishauliana ili kuilinda serikali na kadhia hii mahabusu 5 wenye makosa ya ujambazi wanahitajika kutoka katika magereza yaliyopo mwanza, songea, tabora, tanga na kigoma waletwe dar ili hao waweze kuonyeshwa kwenye vyombo ya habari kuwa ni majambazi yaliyomteka ulimboka na kumpiga. Wakishapatikana wataonyeshwa kwenye vyombo vya habari na umma wa watanzania utaambiwa kuwa wale ndio walifanya unyama huo wako chini ya ulinzi na kuwa maohojiano yanaelendelea na uchunguzi ukikamilika watapelekwa mahakamani na hapo ndipo utakuwa mwisho wa mchezo.
3. Mbinu nyingine ni kuwa mahabusu hao wasafirishwe hadi pwani na wauwawe wote na taarifa itoke kuwa ndio waliomteka dr ulimboka na wamekamatwa wakiwa mkoa wa pwani katika msako mkali wa jeshi la polisi. Na katika kujibizana risasi polis ilifanikiwa kuwaua majambazi hayo. Na hapo ndo itakuwa mwisho wa swala hili na serikali itakuwa imenawa mikono na kujisafisha

kwa sasa kinachofanyika ni kuwasiliana na magereza husika ili kila gereza litoe mtu mmoja (mahabusu) atakayesafirishwa hadi dar/pwani na wataunganishwa kisha kuonyeshwa kwenye vyombo vya habari wakiwa hai au maiti ili kuuaminisha umma kuwa wao ndio walimvamia dr.ulimboka
upelelezi na uchunguzi unaofanyika sasa ni changa la macho kwa watanznai na hiyo tume aliyoiunda kova nayo ni changa la macho ,na kama ulimboka alifanikiwa kuwaona vizuri na kuzishika sura zao ,mmoja wao yupo katika kamati hiyo. Hakuna uchunguzi wowote utakaofanyika wenye tija kwa taifa juu ya kilichotokea.kamanda kova anasimamia operation hii na ameambiwa hakikisha serikali inasafishika.

Mazingira yote yanayoihusisha serikali kwa watu wake kufanya ushenzi kuna jitihada kubwa inafanyika ili kufuta dhana hiyo. Si maraya kwanza kwa serikali kuua watu inaowaona ni mwiba kwake. Wapo wengi na wengi wamezikwa kwenye msitu huo wa pande, kuna msitu uko kibaha(kama uamzi wa kuwaua mahabusu utakubaliwa basi watauliwa kwenye msitu huo) na wengine hutupwa baharini .
Kusamilika kwa ulimboka ni kuwa mungu ana mpango nae na serikali inafanya kila linalowezekana kujinasua. Si wote serikalini wamefurahishwa na kilichotokea wengine wamechukia tena sana
tafakari!!!!!

acha kutengeneza habari wewe.. Na usitake potosha wananchi kwa habari zako za kutunga... Ukweli wewe unaujua au unatangu tu hapa. Wananchi hatudanganyiki na habari zenu za kutunga.
 
Nimewasiliana na rafiki zangu huko Africa ya kusini nimewaeleza hali halisi ya huyo jamaa aliyehusika kwenye unyama huo. Nikawauliza tufanye nini maana nina uhakika wanaweza kuhamasisha watz wote walioko huko Africa ya kusini.

Wakemee na ikiwezekana waanze maandamano hadi ubalozi watz huko Africa ya kusini kupinga kupelekwa huyu aliyefanya mauaji. Tunatakiwa tuungane wote ulimwenguni watz popote walipo waelezeni hawa watu wa magharibi anayoyafanya kikwete na serikali yake.

Mimi nimeshaanza mchakato nataka hata ikiwezekana niandike maombi ya kusaidia harakati nchini tz hii ni hali ya hatari imetangazwa kuanzi siku iliyomfika mpenwa wetu Dr Uli hatuwezi kuvumilia haya. Leo yeye kesho wewe hadi lini tuhamasishane jamani kila kona ya dunia

wewe ndugu ni mzalendo.MUNGU AKUBARIKI
 
Tanzania zaidi ya uijuavyo! Vituko ni vingi serikalini na viongozi (majority) ni wachawi, wezi, wauaji, wala rushwa wa kutupwa, wazinzi, akili hakuna (ni kama wanafikiri kwa kutumia makalio) na in short wanatembea katika laana na wamempa shetani kumbato (wamemkumbatia) na kuiweka nchi shidani.... Sasa tukiiombea kwa Mungu hawa wadudu wataondoka, serikali itapona na itakuwa na hofu ya Mungu. Otherwise tutaendelea kulalama tu hapa na mauzauza yao serikalini yanaendelea. Tuiombee nchi yetu ipone na vituko vyote vitaisha na tusitawaliwe kishetani shetani kwani hatutakuwa na viongozi waliochoka na wanaofanya maovu bali viongozi wanaoitakia mema nchi hii tajiri ilio na watu masikini...
 
Kuna watu wako so bitter na Dr. Ulimboka mpaka inatia mashaka nani hasa ni muhusika wa matendo hayo yasiyokubalika. That is how the weak think they get their strength and compensate their weakness
 
Hii serikali inataka kupendwa na watu wake. But how kama mambo yanaenda kihuni huni hivi?
 
kwa mtu asiyeijua serikali hii ya ccm anaweza kubisha lakini kwa waliofunguka hilo linawezekana kabisa kwa jinsi tukio lenyewe lilivyotokea watazima lakini wengi hatutawaamini bse of circumstantial eviidence.
 
nahisi watammaliza huko india anakotaka kwenda kweli sijui ulimboka angesema vyote then aondoke jamani mi nashindwa kuelewa kabisa its so sad to be slave on your own mothers land jamani inaniuma sana

bado zamu yako, wewe si unajifanya unajua kutongoza waume za watu kupitia jf? tutaona mwisho wake. wewe ni ngiriba wa kike na figganigga si saize yako. bora uwende facebook.
 
Last edited by a moderator:
Asije akawa ameisha kufa tayari na hasiweze kutoa ushaidi..nakumbuka kesi ya Mh. Zombe shaidi mahususi alifariki pale OCI na yawezekana kile kifo hakikuwa ni mapenzi ya Mungu bali ya sirikari...
 
Asije akawa ameisha kufa tayari na hasiweze kutoa ushaidi..nakumbuka kesi ya Mh. Zombe shaidi mahususi alifariki pale OCI na yawezekana kile kifo hakikuwa ni mapenzi ya Mungu bali ya sirikari...
Ulimboka is well and sound, ishu ya kwenda nje kimatibabu ni kumuondoa katika mazingira ya MOI ambapo serikali ilikuwa na mpango wa kufukuza madaktari wote ili wadhibiti hospitali na kuwa na total control na maisha ya Ulimboka.
Japo hata huko wanaweza fika but they need a serious homework, given the mentality ya government yetu.
Waishindwa akiwa peke yake msituni mikono na miguu imefungwa, at least he stand a bigger chance in another soil.
Of course he is en route to another sterile location
 
Naungana na watu na taasisi zote kupinga unyanyasaji na ukatili wa mwisho kabisa duniani dhidi ya Mpigania haki Dr.Stephen Ulimboka.Pamoja na huzuni kubwa niliyonayo naomba nami nishiriki mjadala huu.Naomba mnisaidie kufikiri.Maelezo mengi yaliyokusanywa mpaka sasa(sio na polisi) ni kuwa walioko nyuma ya hili tukio ni serikali kwa kutumia vyombo vyake vya uuaji(sio usalama) hasa polisi.Sasa kama hili ni kweli na kama kwa sasa wanapanga na kufanya mikakati hii ambayo imewasilishwa na mtoa mada kwa ajili tu ya kupoteza ushahidi.Kama ndivyo basi kwa nini polisi hawakumuua Dr. ile alfajiri alipopelekwa kwao na wasamaria?
Kwa nini polisi waliwapigia simu watu wa haki za binadamu kuwapa taarifa za kupatikana kwa Dr.akiwa mzima huku wakijua kuwa uhai wake sio salama kwao?
Kwa nini hawakumuua pale kituoni na kutoa maelezo rahisi tu kuwa aliletwa akiwa mahututi sana na kabla waliopigiwa simu hawajaja akawa kakata roho?Hivi ilikuwa vigumu kufanya hivyo kuliko kupanga mauaji ya watu zaidi sasa na kuwahamisha wengine huku baadhi ya majina ya polisi yakiwa yameshaanza kutajwa kwenye mpango huu?
Naomba mnisaidie kufikiria wanajamvi.

Get well soon Dr.Ulimboka.

Kwa mujibu wa msamaria mwema aliyemuokota Dr..Ulimboka..mara baada ya kumkuta pale bara barani msitu wa mambwe pande ambapo alipokuwa akihojiwa na Wapo Radio Fm...alisema kuwa Dr alisaidiwa na mpita njia ambaye alikuwa anapita hiyo njia kwa miguu ambaye alisikia sauti ya mtu anaomba msaada kutoka porini huyu mpita njia kwa ujasiri akaingia msituni na kumkuta Dr na kuja nae barabarani...lakini hata hapo barabarani magari yalikuwa yanawapita tuu wenye magari wakihofia kutekwa kuwa inawezekana wakawa majambazi lakini ndio wakatokea hawa vijana ambao wao walikuwa na gari na kujitolea kusimama kumsaidia Dr Ulimboka hiyo ilikuwa ni saa moja asubuhi hawa vijana wakamuhoji Dr ndio akawaeleza kuwa yeye ni Dr alitekwa na watu na kumtesa na kumtupa porini...wakamuuliza kama anakumbuka namba ya Dr au rafiki yake yoyote ndio akawatajia namba ya Dr wa Muhimbili hawa vijana wakampigia huyo Dr wakamweleza wamemwokota Dr kwahiyo wao wanampeleka kituo cha Police Bunju kwahiyo wakutane nao huko kituoni...kwahiyo waliowapigia haki za binadamu simu sio police ni Ma Dr wenzake...hii ni Kauli ya Bi Helen Kijo Bi Simba..

Mungu wa Mbinguni mponye Dr Stephen Ulimboka na umlinde na kila hila na uwalaaani wote waliohusika kwa kitendo hiki wao na vizazi vyao na mapigo yaje juu yao...tunajua Mungu wewe ni Mungu wa kisasi kama ilivyoandikwa kisasi ni chako wewe Mungu..mkono wako wenye uweza usimwache salama hata mmoja mshiriki wa unyama huu.iwe kwa Cancer,Ukimwi,Presha,Kisukari,Tauni,Tb,Kupooza,majukumu yote wanayofanya washindwe kuyatimiza na hatakuwaziba pumzi zao kwa mapepo wanayoyatumaini.

...Amen
 
Is there a theory or hypothesis without facts?

It depends on which type of theory you are talking about--scientific or non-scientific one. Certainly, in the context of science realm, all theories must be tested with scientific researchs before they're made publicly available. In contrast, non-scientific theories merely represent people's cursory views on certain issues, and therefore they don't necessary call for an intensive investigation prior to their releasing.
 
Kwa mujibu wa msamaria mwema aliyemuokota Dr..Ulimboka..mara baada ya kumkuta pale bara barani msitu wa mambwe pande ambapo alipokuwa akihojiwa na Wapo Radio Fm...alisema kuwa Dr alisaidiwa na mpita njia ambaye alikuwa anapita hiyo njia kwa miguu ambaye alisikia sauti ya mtu anaomba msaada kutoka porini huyu mpita njia kwa ujasiri akaingia msituni na kumkuta Dr na kuja nae barabarani...

...Amen
Kapindisha kidogo stori.
Alipigwa hadi kuzimia
Kafungwa mikono kwa nyuma
Na miguu kafungwa,
Katumbukizwa kwenye shimo na kuwekwa miti na majni juu yake.
Muda ukapita ndo nguvu na faham zikaanza kumrudia,
Akajaribu kumanipulate miguu na mikono na kamba za miguu zikaachia.
Za mikono were bony tight.
Akaanza kutembea bila kujua anaenda wapi msituni.
Kwa mabli akasikia magari yakipita barabara ya vumbi akafuata.
Magari yalimpita japo alijitahidi kusimamisha.
Akakutana na jamaa anatembea kwa miguu na sigara yake akamweleza story ndo huyo jamaa akavua pensi yake akamvalisha kwa sababu alikuwa na shati lililowa damu tu huku chini ya kiuno hana hata kipande cha nguo.
 
Kuna haja ya kutafuta muarobaini wa kumaliza huu ujinga unaofanywa na serikali ya CCM!
Hii kitu hakika haikubaliki hata kidogo.Lazima Watanzania wachukue hatua za haraka na za maksudi kuliokoa taifa hili ambalo linaenda kuangamia!
 
Back
Top Bottom