Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,923
- 12,198
Mchanganuo wa takwimu hizo ndani ya kipindi hicho, Makosa ya Ubakaji; Mbeya Jiji ni 70, Mbalizi (37), Chunya (77), Rungwe (33), Kyera (34) na Mbarali (33).
Makosa ya Ulawiti, Mbeya Jiji (20), Mbalizi (7), Chunya (0), Rungwe (4), Kyera (3), Mbarali (3).
Wizi wa Watoto; Mbeya Mjini (2), Mbalizi, Chunya, Rungwe, Kyera na Mbarali kote (0)
Makosa ya Kutupa Watoto; Mbeya Jiji (5), Kyera (2) kwingine kote hakukuwa na kesi hizo.
Mkuu wa Dawati la Jinsia Mkoa wa Mbeya, Loveness Mtemi amesema “Fikiria makosa yote hayo na hapo ni kesi zilizoripotiwa Polisi, kuna wengine hawajafika Polisi kuripoti, je, jamii yetu ipoje?
"Watoto wanabakwa, wanalawitiwa, mimi na wewe tusimame, tuone hili ni tatizo."