Mauaji ya RPC yaibua mapya, kampeni za CCM zarindima msibani, 15 wakamatwa!

Kumbe polisi wa Tanzania hawana intelijensia yoyote hadi waombe msaada interpol!!!!!
 
CCM ilivyoishiwa support kutoka kwa wananchi, hiyo interpol feki itasema ni Chadema wamehusika!!!
 
kumbe polisi wanaweza fanyakazi bila msaada wa tume, RPC ameuwawa juzi, leo tunaambiwa watu 15 tayari wamekamatwa wala hawana haja ya kusubiri tume, mwangozi kauwawa na watu wanajulikana kwa majina na picha zipo wakati wakitekeleza unyama wao, eti aliekamatwa na mtu mmoja tu, kweli malipo ya mwovu ni hapa hapa duniani.
 
Watakamata ata na wasio husika ili waonekane wako serious kwa kutaja iadadi kubwa ya watu
 
Hao polisi wamedhalilika kweli,kwa sasa hakuna lolote wanalosema lisilo na kasoro zawazi kabisa!mabingwa wa kubambikiza kesi sembuse kutunga uongo!waseme kuwa kitu cha ncha kali kilifyatuka toka kwenye gari na kumpiga shingoni!maana ndio zao Senso yu wapi na hekaya zake?
 
Ujinga mtupu, inaonekana hata hao Interpol hawana kazi ndio maana wanaweza kujishughurisha na mambo ya kijinga kama haya. Kamanda Barlow ndio Mtanzania wa kwanza kuuwawa kwa risasi?

Hakuna cha Interpol hapo. Hizo ni propaganda tu. Interpol watahusishwa iwapo imebainika hao watuhumiwa wanatoka nje ya nchi
 
Hapana Lokissa vifo vyote viwili vinasikitisha. Hakuna mtu aliyepewa mamlaka ya kutoa uhai wa mtu. Inasikitisha sana kuona watu tunaona uhai kama kitu kidogo sana. Waliomuua Mwangosi hawakuwa na haki na hata hawa waliomuua RPC hawana na haki. Mbele za macho ya Mungu wote wanamakosa. Wafiwa poleni sana. Mungu atawape faraja.
Labda polisi ndio ana thamani zaidi anapokufa kuliko Mwangosi na wale wahanga wengine waliouawa na polisi, wamwache apunzike kwa amani.

Labda na hao interpol wakachunguze pia mauaji ya Mwangosi ntawaelewewa na sio kutumia kodi zetu kwa maslahi ya wachache
 
Nilijiuliza swali hilo baada ya kusikia kwamba ni mmojawapo wa watu wanaoshikilia,sasa kipengele hicho hapo juu ndicho kinaonyesha wazi kwanini wanamshikilia kwa mahojiano zaidi,nadhani wanataka kujuwa kama ni nani mwingine aliyekuwa akijuwa kuwa kamanda atampeleka nyumbani,kwasababu inaonekana kama vile alikuwa akisubiriwa na hao watu.Hata mimi nilidhani waliondoka naye kutoka kwenye hicho kikao cha harusi.

Kuna vitu vingi sana havi add up,kwa mfano kuna habari iliyokuwa ikisema kwamba haikuwa mara ya kwanza kwa kamanda huyo kumpeleka nyumbani,however kuna habari nyingine inayodai tena kwamba alimpelekea nyumbani ili apajue anapoishi.Sasa imeshageuka tena kuwa aliombwa lifti wakati akielekea nyumbani kwake Pasiansi.

Wanataka waandishi wawasaidie kwenye uchunguzi na huku wanatoa habari zisizo add up.

kumbuka aliekua amfungulie mlango huyo mdada alipigiwa simu na dorothy akimwambia nakuja na mgeni anataka kupajua kwangu.which means hakua akipajua kama alikua anapajua doroty asingemwambia hivo huyo kijana mfungua geti.vinginevo kijana nae yuko kwenye issue.
 
Kwa kweli inasikitisha sana kilichotokea kwa kamanda wa polisi kuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi sote hatuungi mkono tukio hilo ta tunalaani wale wote waliohusika kwa njia moja au nyingine wafikishwe kwenye vyombo husika ili liwe fundisho kwa wale wote wanaokusudia kuendesha uharifu wa namna hiyo.

Swali la kujiuliza ni kwa nini kamanda wa polisi atembee wakati huo wa usiku wa manane na hali anajua ya kuwa yeye ni koingozi wa serikali na matembezi yenyewe yalikuwa ya binafsi na wala siyo ziara ya kiserikali je huu sio uvunjifu wa sheria kwa kingozi kama barlow kutembea usiku wa manane?

Lakini pia ikumbukwe tu ya kuwa popote mwanadamu alipo anachukiwa na wanadamu wenzake pengine moja kwa moja kwa maana ya kuwa anaweza kuwa anafahamu ya kuwa anachukiwa au la. Pia yaweza kuwa siyo moja kwa moja kwa maana ya kuwa anaweza asijue ya kuwa anachukiwa lakini kubwa ambalo waliobaki wanapaswa kujua hasa hawa walinda amani ya nchi. Ni kwa kutokana na mazingira ya kazi zao wajue ya kuwa raia wanawachukia takribani muda wote kwani waweza kusimama kwenye haki kwa lengo la kunusuru maisha ya raia lakini kwa vile raia siku zote ni wabinafsi wanamchukulia tofauti.

Hivyo basi isifikie hatua ya wao kutembea kwa kujiamini kama anavyotembea mwalimu, daktari au mfanyabiashara kwani mazingira ya kazi yake siyo hatarishi sana kama ilivyo kwa wenzetu askari
 
Nilipoona tu IGP Mwema wa kwanza kulaani mauaji hayo nikajua tu amri ya kumuua kamanda Barlow haikutoka kwa mkulu.

Angalia polisi wanavyofanya kazi kila baada ya masaa machache lazima yawepo maendeleo ya upelelezi. Tumepewa hadi taarifa ya Bugando. Mbona hawakufanya hivyo kwa Dr. Ulimboka na marehemu Mwangosi? Mimi mpaka leo siamini bomu la machozi ndo lililosambaratisha mwili wa marehemu. Taarifa ya hospitali kuhusiana na kifo cha Mwangosi kwani inasemaje?
 
Huyu mwalimu nae atakuwa ni jambazi mbona hatupewi maelezo saa nane usiku huyo mama alitoka wapi na je pansiasi na kitangiri ni eneo moja coz lift mda huo mara nyingi utampa mtu lift kama anakwenda njia moja na wewe.Je sheria za jeshi zinamruhusu kiongozi wa ngazi za juu kama yeye mkumpa mtu yeyote lift na kumpeleka atakapo?
 
Mmmhhh, tarifa za awali zilitueleza kuwa walitoka wote kwenye kikao na mwalimu Doroth, mara mambo yamegeuzwa walikutana njiani (usiku saa 8 huyo mama alikuwa anatembea peke yake, makubwa!!).

Moyo wangu unakataa kuamini hii new twist. Nyie badilisheni na kunyumbulua tu, time will tell.

NAKUUNGA MKONO KWA ASILIMIA 100. Watu wanakurupuka tu.
 
huyo mwalimu doroth ambaye alipakiwa na marehemu kamanda walikuwa wanafahamiana kabla?na je ana mume huyo mama?mliopo mwanza nisaidieni maana naona pana kitu hapa.
 
Back
Top Bottom