tukio ni kubwa. msaada wa interpol ni lazima ili kama wauaji wamekimbilia nje wadakwe.
Bwana ametoa na Bwana Ametwaa!
Kumbe polisi wa Tanzania hawana intelijensia yoyote hadi waombe msaada interpol!!!!!
Ujinga mtupu, inaonekana hata hao Interpol hawana kazi ndio maana wanaweza kujishughurisha na mambo ya kijinga kama haya. Kamanda Barlow ndio Mtanzania wa kwanza kuuwawa kwa risasi?
Labda polisi ndio ana thamani zaidi anapokufa kuliko Mwangosi na wale wahanga wengine waliouawa na polisi, wamwache apunzike kwa amani.
Labda na hao interpol wakachunguze pia mauaji ya Mwangosi ntawaelewewa na sio kutumia kodi zetu kwa maslahi ya wachache
Nilijiuliza swali hilo baada ya kusikia kwamba ni mmojawapo wa watu wanaoshikilia,sasa kipengele hicho hapo juu ndicho kinaonyesha wazi kwanini wanamshikilia kwa mahojiano zaidi,nadhani wanataka kujuwa kama ni nani mwingine aliyekuwa akijuwa kuwa kamanda atampeleka nyumbani,kwasababu inaonekana kama vile alikuwa akisubiriwa na hao watu.Hata mimi nilidhani waliondoka naye kutoka kwenye hicho kikao cha harusi.
Kuna vitu vingi sana havi add up,kwa mfano kuna habari iliyokuwa ikisema kwamba haikuwa mara ya kwanza kwa kamanda huyo kumpeleka nyumbani,however kuna habari nyingine inayodai tena kwamba alimpelekea nyumbani ili apajue anapoishi.Sasa imeshageuka tena kuwa aliombwa lifti wakati akielekea nyumbani kwake Pasiansi.
Wanataka waandishi wawasaidie kwenye uchunguzi na huku wanatoa habari zisizo add up.
CCM ilivyoishiwa support kutoka kwa wananchi, hiyo interpol feki itasema ni Chadema wamehusika!!!
Mmmhhh, tarifa za awali zilitueleza kuwa walitoka wote kwenye kikao na mwalimu Doroth, mara mambo yamegeuzwa walikutana njiani (usiku saa 8 huyo mama alikuwa anatembea peke yake, makubwa!!).
Moyo wangu unakataa kuamini hii new twist. Nyie badilisheni na kunyumbulua tu, time will tell.