Binafsi nachukia sana mauaji ya raia yanayofanywa na jeshi la polisi wa Tanzania. Hawa polisi tatizo lao kubwa ni kuwa hawajui hasa kazi zao ni zipi na pia wanatumiwa na wenye mamlaka kuudhoofisha upinzani jambo ambalo huligharimu taifa na kusababisha amani ya nchi kutoweka. Chonde!chonde! polisi tendeni haki katika kazi zenu na kulinda amani na mali za raia.