Mauaji ya CCM Igunga:Scotland yard na OCAMPO wafanye uchunguzi

makoye2009

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
2,638
1,218
Ndugu wana JF,
Ndugu wana CHADEMA,
Ndugu Viongozi Waandamizi wa CHADEMA, Mabibi na Mabwana,

Kwanza hebu tusimame kimya kwa dk.1 kuwakumbuka marehemu wote waliouwawa kikatili kwa maelekezo ya Chama Cha MAUAJI-CCM kule Igunga. Amen.

Kwanza kabisa napenda nianze kwa kusema kuwa nina huzuni sana moyoni kutokana na yale yaliyojitokeza katika kinyang'anyiro cha kugombea Ubunge jimbo la Igunga. Kwamba Chama Tawala al-maarufu kwa majina ya Chama Cha Magamba,Chama Cha Mafisadi,Chama Cha Majambazi,na sasa baada ya IGUNGA kimepata jina jingine la CHAMA CHA MAUAJI-CCM!!!!

Kila Mtanzania mpenda haki,amani na mshikamano ameweza kupata picha kamili ya aina ya Watawala tulio nao ndani ya CCM kwa sasa. Kwamba wako tayari KUMWAGA DAMU YA WATANZANIA WENZAO ILI TU WAPATE UBUNGE AU KUINGIA IKULU!!!Hii imeonyesha UDHAIFU mkubwa sana wa CCM ya sasa. Kwamba chama hiki sasa kimebakia kama DUBWASHA kubwa lisilo na faida yoyote kwa mstakabali wa nchi yetu Tanzania.

Hapana shaka wala tashwishi kuwa MAUJI yaliyotokea wakti wa kampeni na siku ya Uchaguzi kule Igunga yalitekelezwa na CCM yenyewe kwa maelekezo maalumu. Kitendo cha Serikali yote ya CCM kuhamia Igunga kuanzia Rais mstahafu,Katibu Mkuu mstahafu wa CCM,Mawaziri na Makada mbalimbali kwenda Igunga ilikuwa kutekeleza MPANGO MAALUMU WA MAUAJI ULIOANDALIWA ILI KUWATISHA WATANZANIA NA HASA WANA CHADEMA kuwa hata kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 NDIVYO ITAKAVYOKUWA!!!

Kwa vile mauaji haya yana SURA YA KISIASA, napenda kwa heshima na taadhima niwaombe viongozi CHADEMA kitaifa kuingilia kati katika Uchunguzi wa mauaji haya ili kuweza kuwapata WAUAJI hawa kutoka ndani ya CCM ambao walitekeleza mpango huu.

Tunajua CCM na Vikaragosi vyao: Jeshi la Polisi,Usalama wa Taifa,JWTZ na wengineo hawawezi kufanya uchunguzi huu na kuweka wazi kile kilichotokea Igunga hatimaye haki kutendeka Kwa mazingira kama haya basi MSAADA WA JESHI LA POLISI WA SCOTLAND YARD kutoka Uingereza unahitajika.Scotland Yard wanatakiwa waitwe kufanya Uchunguzi wa kina na hatimaye waweze kuwabaini na kuwakamata WAUAJI WA CCM ili wapelekwe Mahakama ya Kimataifa-ICC kwa Bwana Moreno Ocampo na sheria ichukue mkondo.

Kama jambo hili litaachwa hivi hivi tu,basi Uchaguzi Mkuu wa 2015 tutegemee MAAFA ambayo YATAGHARIMU MAISHA MENGI SANA YA WATANZANIA wasio na hatia.

Nawasilisha.
 
Inasikitisha! Inauma!!!!!!!!!!! lakini wataua wahgapi???? sasa tumeshaelewa wakitakacho.Surely mwisho wao umeshafika wamekwisha!!!!!!!!! Damu ya mwanadamu haipotei bure!!!! Amini usiamini waliouwawa wote watajulikana tu!!!!!! hakuna green gurad wala green magamba siku ikifika !!!!!!!!!! naomba uchaguzi mdogo mwingine utokee kulidhihirisha hili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom