Elections 2010 Matumaini ya kutokuibiwa kura yametokea - bado swali moja dogo

Mtaka Haki

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
492
149
HABARI ZILIZOANDIKWA KATIKA MAGAZETI MBALIMBALI LEO ZINAONYESHA KUWA KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU KITASAMBAZA WAANGALIZI HURU NA KUJUMLISHA MATOKEO. KILA MKOA KITAKUWA NA MWANGALIZI MMOJA. KULINGANA NA HABARI HII HAPA CHINI INAONEKANA WAANGALIZI NI 1744. Swali dogo je vituo vya kupiga kura mwaka huu ni vingapi kama idadi hiyo ni sawa na ya vituo vilivyoko basi matumaini yetu ni makubwa.
Hongereni sana.


HRC kusambaza waangalizi majimboni
NA RICHARD MAKORE
16th October 2010
B-pepe
Chapa
Maoni

Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa ndani wanatarajia kuanza kusambaza katika majimbo mbalimbali kunzia Jumatatu ijayo.
Kaimu Mkurugenzi wa Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Anna Katemana, alisema jana kuwa waangalizi hao wanafikia 1,744 na watakuwa katika mikoa, majimbo na kwenye vituo vya kupigia kura.
Waangalizi hao wameteuliwa na mtandao wa Asasi za Kiraia (TACCEO) unaoundwa na mashirika 17 ambapo watatumia kompyuta na simu za mkononi kufanya kazi hiyo.
Kadhalika, mtandao huo umeandaa utaratibu utakaowawezesha wananchi kutuma ujumbe mfupi wa simu (SMS) kwa waratibu wa kitaifa watakaokuwa Dar es Salaam kupitia namba 15540 kwa mitandao ya Vodacom, Tigo, Zain na Zantel ili kutoa taarifa kwao juu ya mambo mbalimbali yatakayotokea katika vituo vya kupigia kura.
Waangalizi hao watasambazwa katika mikoa yote ya Tanzania bara na Zanzibar kwenye majimbo na vituo vyote vya kupigia kura.
Katemana alisema waangalizi 270 watakuwa katika majimbo na kila mkoa utakuwa na mratatibu mmoja ambaye atakuwa anaratibu shughuliz zote za uangalizi na kutoa taarifa makao makuu ya mtandao huo yatakayokuwa jijini Dar es Salaam.
Asasi hizo za kiraia ni pamoja na Tamwa, SAHRINGON Tanzania, WLAC, TANLAP, WILDAF, ForDIA, Haki Madini, MPI, ACCORD, ZLSC, PF, Tahurifo, YPC, LEAT na LHRC.
Alisema TACCEO imepata kibali cha kufanya kazi hiyo kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kwamba lengo la uangalizi huo ni kuanisha mapungufu yatakayojitokeza wakati wa Uchaguzi Mkuu 2010.
Kwa mujibu wa Katemana taarifa zitakazokusanywa nchi nzima na kuchambuliwa ili kuweka kumbukumbu na rejea ili ziweze kusaidia kuboresha Uchaguzi Mkuu siku zijazo.
Maeneo mengine yatakayoangaliwa na waangalizi hao ni pamoja na kiwango cha wananchi kuelewa masuala ya uchaguzi, elimu ya uria kwa wananchi, ushiriki wao, ushiriki wa wadau mbalimbali kama Nec, vyomb o vya habari, vyombo vya usalama na Asasi za kiraia zinavyoelimisha jamii.
CHANZO: NIPASHE
0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
 
Je kuna mwenye idadi ya vituo vya kura nchi nzima? Tunaweza kuwashauri kama idadi ya vituo ni nyingi kuliko idadi ya watu.
 
vituo vya kupigia kura viko vingi kuliko hiyo idadi ya hao wasimamizi nadhani vituo viko 50,000 na zaidi kama sijakosea ila hata hivyo wamejitahidi sana
 
Kuna mwenye taarifa kamili. Tunaweza kuwaomba wakubali watu watakao vulunteer bila ya kulipwa. Wako watu waaminifu katika kila mkoa. Wako wanafunzi wa vyuo vikuu amabao hawapigi kura wengi wao
 
Mungu awajalie baraka. God Willing Tanzania itazaliwa upya! Mbona nitajivunia kuitwa Mtanzania na kutembea kifua mbele
 
nazidi kupata matumaini makubwa juu ya ushindi wa SLAA maana uchakachuaji ungetudhulumu ila kama wameamua kusaidia hivyo tumefurahi
 
vituo vya kupigia kura viko vingi kuliko hiyo idadi ya hao wasimamizi nadhani vituo viko 50,000 na zaidi kama sijakosea ila hata hivyo wamejitahidi sana

Sina hakika na idadi ila niliwahi kumsikia Kiravu akisema kila kituo kitakuwa na wapiga wasiozidi 500. Akasema kwa idadi hii siyo rahisi kuiba kura
 
Je kuna mwenye idadi ya vituo vya kura nchi nzima? Tunaweza kuwashauri kama idadi ya vituo ni nyingi kuliko idadi ya watu.
Eneo moja mfano shule moja inaweza kuwa na vituo hata 20 yaani kila darasa ni kituo A,B,C,D,E,F.......kwa hiyo mwangalizi mmoja anaweza kuzungukia vituo hivyo vyote bila shida.
 
vituuo vya kupigia kura vpo 57000
Dhahiri kama ndivyo itakavokuwa basi itasaidia lakini mi nina wazo moja kwa wenzangu wanaJF kuwa mara nyingi mambo mazuri hayapatikani kwa kujiweka kando,bali kujitoa kwa moyo mmoja,kuvumilia kashikashi na kuwa na imani kuwa lile tunalo amini linawezekana.
Binafsi ningependa mambo yafuatayo tuyafanye:-
a)kuhakikisha watu ambao tunadhani wanamsukumo wa mabadiliko wakapige kura
b)Tuwe wawazi kwa watanzania wenzetu juu ya hisia zetu juu ya mstakabali wa
nchi yetu kwa kulinganisha mahitaji na maisha tulonayo sasa.
c)Pia siku ya kupiga kura tukae mita 200 ili kulinda kura zetu na wale ambao ni
mawakala wetu(chadema) ikibidi tuwape motisha na kuwaeleza tuko nyuma yao,wasiwe
na mashaka hii pia itakuwa nafasi nzuri katika kuhakikisha kura zetu zinalindwa vizuri.
d)Kumshirikisha MWENYEZI MUNGU katika kile tunachoamini ni sahihi na kumwomba pia
asaidie kukilinda maana yeye hakuna limshindalo.
Ni imani yangu kuwa hili tutaliweka katika kumbukumbu zetu.
 
Lakini anayetangaza mshindi ni NEC kumbuka kuhesabu kura na kutangaza mshindi hapa kwetu ni vitu viwili tofauti.
 
Back
Top Bottom