GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Tujuzane matukio au vitu tulivyoona au kukutana navyo kwa waganga wa jadi au Kienyeji vya kutisha na kuchekesha, Na hii itawafunza Wengine ambao wanategemea kwenda au ambao hawajui kinachoendelea huko
Mimi kama mwana siasa na mfanyabiashara haya mambo kuna wakati unataka kuyakwepa lakini kundi au crue inayokuzunguka kwa ushauri inakulazimu uisikilize
Tukio namba moja
Mwaka 2004 Katika harakati za kujiandaa na uchaguzi wa ubunge utakaofanyika 2005 washauri wangu wakaniambia Bwana mkubwa inabidi twende tukaangalie kama kutakuwa na kikwazo mbele yetu
Tukaamka asubuhi tukaelekea kwa Mzee wa makamo( Huyu ni Mganga ana wake wengi sana na pia anafuga mbuzi wa kutosha hapo nyumbani kwake, Ana mbuzi zaidi ya mia moja hapo kwake. Mzee anavalia barakashee na kanzu yake yenye Rangi ya kijivu fulani, Kufika tu pale kwake tulikuwa watu watatu mlangoni akatuambia nilijua mnakuja toka mbali sana, Na sasa mnatakiwa kuelezea ukweli bila kuficha kitu, Nikambonyeza mwezangu kwa kumkonyeza kuwa tusiongee bali yeye ndio atuambie tumefuata nini pale kwake kutokana na uzoefu wetu wa maeneo mengine, Mzee akachukua kitabu chake akawa kama anakisoma hivi huku anaandika lugha ambayo sisi tulikuwa hatuifahamu, Baadae akasema Nyie ni wanasiasa na mpo hapa kujua nini kitatokea mwakani kwenye kura za maoni, Kusikia hivyo tu nikasema moyoni oooho Yes that I need it,
Sasa ngoma ikaanza, Mganga akasema ili kuweza kuona vikwazo vyetu anahitaji mbuzi beberu kubwa lililoshiba na lenye nguvu na lazima beberu awe na Rangi nyeupe ambalo saa tisa usiku itabidi tuelekee Yeye na sisi baharini na mtubwi katikati ya Bahari tukamchinje huyo mbuzi beberu, Beberu atakapochinjwa inabidi asitikisike wala kupiga kelele, Akitikisika na kupiga kelele maana yake zoezi letu itabidi tuanze upya tena kutafuta beberu mwingine mweupe.
Nikafikiria Beberu natoa wapi, Nikamuuliza Mganga sasa Beberu namtoa wapi akasema ni wewe mwenyewe ukatafute au ununue hapa kwangu kwa wakati huo akataja beberu shilingi TZS 120,000.Nikamwambia nitakupa Jibu, Nikaenda soko la mbuzi nikakuta mbuzi wanauzwa TZS 50,000 mpaka TZS 70,000.Nikasema moyoni nanunua hapa mbuzi wawili wa TZS 60,000 @ mmoja wa mganga na mungine nachinja kwa ajili ya nyumbani kwangu kama kitoweo
Nikapeleka beberu nililonunua elfu 60,000 mweupe badala ya yule wa Mganga wa Tzs 120,000.
Sasa kindumbwe ndumbe ni huko baharini saa tisa za usiku nani ataenda kati ya sisi, Sisi wote hatujawahi kanyaga saa tisa za usiku katikati ya Bahari Halafu na mtubwi, Kwa uwoga wangu nikasema Jamaa zangu waende huko na Mganga Bahari kuchinja mbuzi, Mbuzi alichinjwa huko cha kushangaza alitikisika na kupiga kelele hivyo zoezi la kwanza likafeli ikatakiwa warudi Halafu tujipange upya kwa mbuzi mwingine
Baada ya zoezi kufeli Nikamwambia Mganga sasa labda nijaribu kununua mbuzi wako kwa TZS 120,000 kama anavyouza, Nikachagua beberu mweupe na zoezi likafanikiwa huko katikati ya Baharini kwa kutumia mbuzi anafuga Mganga, Hivyo ni kapata hasara ya mbuzi mmoja, Hata nyama ya mbuzi wote hao wawili baada ya zoezi sikukabidhiwa na Mganga
Swali ambalo najiuliza mpaka Leo wale mbuzi kwa Mganga ni mbuzi wa kawaida au ni viini macho
Swali jingine ambalo najiuliza ile nyama ya mbuzi baada ya zoezi anakula na familia yake au anaitupa, Maana mimi hakunipatia hata kipande cha nyama wala damu
Mimi kama mwana siasa na mfanyabiashara haya mambo kuna wakati unataka kuyakwepa lakini kundi au crue inayokuzunguka kwa ushauri inakulazimu uisikilize
Tukio namba moja
Mwaka 2004 Katika harakati za kujiandaa na uchaguzi wa ubunge utakaofanyika 2005 washauri wangu wakaniambia Bwana mkubwa inabidi twende tukaangalie kama kutakuwa na kikwazo mbele yetu
Tukaamka asubuhi tukaelekea kwa Mzee wa makamo( Huyu ni Mganga ana wake wengi sana na pia anafuga mbuzi wa kutosha hapo nyumbani kwake, Ana mbuzi zaidi ya mia moja hapo kwake. Mzee anavalia barakashee na kanzu yake yenye Rangi ya kijivu fulani, Kufika tu pale kwake tulikuwa watu watatu mlangoni akatuambia nilijua mnakuja toka mbali sana, Na sasa mnatakiwa kuelezea ukweli bila kuficha kitu, Nikambonyeza mwezangu kwa kumkonyeza kuwa tusiongee bali yeye ndio atuambie tumefuata nini pale kwake kutokana na uzoefu wetu wa maeneo mengine, Mzee akachukua kitabu chake akawa kama anakisoma hivi huku anaandika lugha ambayo sisi tulikuwa hatuifahamu, Baadae akasema Nyie ni wanasiasa na mpo hapa kujua nini kitatokea mwakani kwenye kura za maoni, Kusikia hivyo tu nikasema moyoni oooho Yes that I need it,
Sasa ngoma ikaanza, Mganga akasema ili kuweza kuona vikwazo vyetu anahitaji mbuzi beberu kubwa lililoshiba na lenye nguvu na lazima beberu awe na Rangi nyeupe ambalo saa tisa usiku itabidi tuelekee Yeye na sisi baharini na mtubwi katikati ya Bahari tukamchinje huyo mbuzi beberu, Beberu atakapochinjwa inabidi asitikisike wala kupiga kelele, Akitikisika na kupiga kelele maana yake zoezi letu itabidi tuanze upya tena kutafuta beberu mwingine mweupe.
Nikafikiria Beberu natoa wapi, Nikamuuliza Mganga sasa Beberu namtoa wapi akasema ni wewe mwenyewe ukatafute au ununue hapa kwangu kwa wakati huo akataja beberu shilingi TZS 120,000.Nikamwambia nitakupa Jibu, Nikaenda soko la mbuzi nikakuta mbuzi wanauzwa TZS 50,000 mpaka TZS 70,000.Nikasema moyoni nanunua hapa mbuzi wawili wa TZS 60,000 @ mmoja wa mganga na mungine nachinja kwa ajili ya nyumbani kwangu kama kitoweo
Nikapeleka beberu nililonunua elfu 60,000 mweupe badala ya yule wa Mganga wa Tzs 120,000.
Sasa kindumbwe ndumbe ni huko baharini saa tisa za usiku nani ataenda kati ya sisi, Sisi wote hatujawahi kanyaga saa tisa za usiku katikati ya Bahari Halafu na mtubwi, Kwa uwoga wangu nikasema Jamaa zangu waende huko na Mganga Bahari kuchinja mbuzi, Mbuzi alichinjwa huko cha kushangaza alitikisika na kupiga kelele hivyo zoezi la kwanza likafeli ikatakiwa warudi Halafu tujipange upya kwa mbuzi mwingine
Baada ya zoezi kufeli Nikamwambia Mganga sasa labda nijaribu kununua mbuzi wako kwa TZS 120,000 kama anavyouza, Nikachagua beberu mweupe na zoezi likafanikiwa huko katikati ya Baharini kwa kutumia mbuzi anafuga Mganga, Hivyo ni kapata hasara ya mbuzi mmoja, Hata nyama ya mbuzi wote hao wawili baada ya zoezi sikukabidhiwa na Mganga
Swali ambalo najiuliza mpaka Leo wale mbuzi kwa Mganga ni mbuzi wa kawaida au ni viini macho
Swali jingine ambalo najiuliza ile nyama ya mbuzi baada ya zoezi anakula na familia yake au anaitupa, Maana mimi hakunipatia hata kipande cha nyama wala damu