Matrekta haya ni kwa ajili ya nini? Mbona msimu huu wa kilimo nayo yananyeshewa na mvua bila kazi!

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Awali wakati matrekta haya yakiletwa kwa mbwembwe tuliambiwa ni kwa ajili ya KILIMO KWANZA. Tukategemea msimu huu wa kilimo wakulima watanufaika kwa kukopeshwa zana hizo muhimu kwa ajili ya kujikwamua ki uchumi. Sasa cha ajabu, mpaka sasa matrekta haya yamekuwa mfano wa maonyesho huria, mwishowe naona nyuki wanaweza kuyageuza mizinga na kufanya maskani yao. Manaake kila nikisafiri kuja Dodoma kwa kipindi cha zaidi ya miezi mitano nayakuta yako pale pale. Tena kando kando ya barabara iendayo Dar. Kwa yeyote anayefahamu kazi ya haya matrekta hebu atufumbue macho. Kwani msimu wa kilimo ndiyo huu sasa nayo yanazidi kunyeshewa na mvua bila ya kazi. Au yameletwa kwa ajili ya kazi nyingine badala ya kilimo?
 
Biashara ya watu hiyo mkuu. Hakuna cha "kilimo kwanza". Kilimo kwanza ilikuwa ni daganya toto. Yachungulie vizuri hayo matrekta KUTU inayashambula kishenzi sna.
 
wanunuaji kila leo wananyang'anywa ardhi,watayatumia kulimia kwenye lami?tanzania ni zaidi ya uijuavyo.
 
awali wakati matrekta haya yakiletwa kwa mbwembwe tuliambiwa ni kwa ajili ya kilimo kwanza. Tukategemea msimu huu wa kilimo wakulima watanufaika kwa kukopeshwa zana hizo muhimu kwa ajili ya kujikwamua ki uchumi. Sasa cha ajabu, mpaka sasa matrekta haya yamekuwa mfano wa maonyesho huria, mwishowe naona nyuki wanaweza kuyageuza mizinga na kufanya maskani yao. Manaake kila nikisafiri kuja dodoma kwa kipindi cha zaidi ya miezi mitano nayakuta yako pale pale. Tena kando kando ya barabara iendayo dar. Kwa yeyote anayefahamu kazi ya haya matrekta hebu atufumbue macho. Kwani msimu wa kilimo ndiyo huu sasa nayo yanazidi kunyeshewa na mvua bila ya kazi. Au yameletwa kwa ajili ya kazi nyingine badala ya kilimo?

miradi ya wakubwa, siku zote haina hasara kwani fedha za ununuzi wake zimetoka ktk mfuko wa pembejeo, na moja ya masharti ya kukopa lazima upeleke hati ya nyumba + deposit ya 12m/ + andiko mradi + udhaminiwe na bibi/babu mzaa bibi/babu yako. Mimi nimehitaji kupata trecta hilo, na nimefuatilia kwa karibu sana lakini baada ya kuangalia terms zake nimeona haziendi sambasamba na kauli mbiu ya kilimo kwanza, haswa ukizingatia sharti la mwisho la mzamini, na uwe na shamba la ekari 50. Na huyo bibi ni kama mzamini ni rushwa.
 
yako show room yanasubiri yapelekwe kwenye maonyesho ya nane nane
 
Biashara ya watu hiyo mkuu. Hakuna cha "kilimo kwanza". Kilimo kwanza ilikuwa ni daganya toto. Yachungulie vizuri hayo matrekta KUTU inayashambula kishenzi sna.

Pia ikiiwezekana kama kuna tajiri yeyote ambae utajiri wake umetokana na kilimo hapa tz embu ajitokeze pls kwani mpaka sasasiamini na sidhani kama itajatokea
 
Back
Top Bottom