Matrafiki wameanza tena kamata kamata

Verily Verily

Senior Member
Jan 4, 2007
188
143
Miezi michache baada ya rai ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Comredi Adulrahaman Kinana kwa jeshi la polisi kupunguza bugudha kwa magari na hasa maeneo ya mijini, hali imebadilika na taratibu inaanza kujirudia kama ilivyokuwa awali.

Ule unafuu uliokuwa umeanza kupatikana sasa unapotea kwa haraka. Mfano, jijini Dar Es Salaam barabara ya Morogoro utawakuta wanabugudhi madereva pale Urafiki, Kimara Baruti, Kimara Temboni, Kibanda cha Mkaa, kwa Yusufu na maeneo hayo hayana umbali hata wa kilometema 3-5 katikati yake. Na ukiendelea mpaka Maili Moja Kibaha ndipo wamejaa kila umabali wa wastani wa kilometer mbili Luguruni, Kibamba, Kilivya, Maili Moja nk.

Haya ni matumizi mabaya ya pesa za walipakodi kulipa mishahara wafanyakazi wasio na tija au mzigo kwa jamii.

Mdau hebu na wewe ongezea kero unazokutana nazo za hawa watu pamoja na kutakiwa kupunguza bugudha zao.

Mwisho, Je polisi na hasa hawa wa barabarini wako juu ya sheria?
 
mshahara wa 520,000 take home unaweza toboa mkuu, mke na watoto 3 ??
 
Ngoja tusikilize Seminar elekezi aliyoandaa mama huko Moshi!! Ni kero kubwa kuruhusu kada nyingine ya ajira kupokea rushwa hadharani
 
tumerudi wakuu, tumegundua bila nyie maisha hayaendi kabisa, buku buku zenu tumezimiss sana makoo yanawasha vikoba haviendi.
#kwani mlijua haturudi?
 
Matrafiki kukaa barabarani ni sehemu yao ya Kazi lakini kwa Hawa trafiki wetu kwao sehemu ya kuijiingizia KIPATO.

Too bad viongozi wao wamewapata target ya kiasi Cha kukusanya pesa per day ukimpa 5,000 hawataki wanataka 10,000

Shortly wapo barabarani kujipatia riziki na sio kulinda Usalama wa raia.

Ajali za barabarani zinazuiliwa na Trafiki au Dereva makini? Hili kundi Lina mbingu yao
 
Only in Tozonia mnajenga mabarabara makuuubwa mnaita sijui njia nane huku mnajaza vibaka barabarani wachuke na wao tozo zao aibu sana sana hii, ndio maana mliambiwa majitu kama mwigulu etal ni majanga kabisaaaa hamkuelewa, sasa kama kila baada ya mita mia unakuta wabrashi viatu, hayo maendeleo mtayatoa wapi? majitu yamekalia rushwa tu wala hayapunguzi ajali yoyote ile yamejaza matumbo tu.
 
Matrafiki kukaa barabarani ni sehemu yao ya Kazi lakini kwa Hawa trafiki wetu kwao sehemu ya kuijiingizia KIPATO.
Too bad viongozi wao wamewapata target ya kiasi Cha kukusanya pesa per day ukimpa 5,000 hawataki wanataka 10,000
Shortly wapo barabarani kujipatia riziki na sio kulinda Usalama wa raia.
Ajali za barabarani zinazuiliwa na Trafiki au Dereva makini? Hili kundi Lina mbingu yao
Halaf mpaka wakubwa wao wanajua kama wanachukua rushwa ila wanalindana tu
 
Vyombo vya habari TZ vibadiishe kazi zao na waweke mziki na tamthilia tuu wao ndio wana wajibu wa kufanya habari za uchunguzi na kujua hasara na faida ya trafik kusimamisha kusumbua na kutisha watu barabarani hivi ni hasara ngapi inapatikana, usafiri unarahisisha kazi na maendeleo kwa ujumla ndio maana nchi ziizoendelea unanunua gari hata kwa $500 na unatembea nayo bila ya kusumbuliwa wanajua umuhimu wa usafiri kwa wananchi na wanajua wanapata kodi kwenye mafuta na mengine,
 
Back
Top Bottom