Matonya alivunja katiba ya bongo flava, hakushitakiwa

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Masterplan ya Tanga kuitawala Bongo Flava, ilianza kwa kutambulisha silaha yao ya maangamizi "Matonya", ambaye kinyonge, alilia “Uaminifu” akimshirikisha Bwana Misosi.

Jamhuri yote ya Bongo Flava ilisaluti talanta ya Matonya. Halafu akapotea masikioni mwa watu. Tanga ikachekwa kuwa ilitambulisha silaha ya one hit wonder yani Ngoma moja, pumzi kwisha.

Hesabu 2004, nenda 2005, weka kituo 2006. Matonya akarudi kwa ujio ulioacha historia ya dude baada ya dude, mawe juu ya mawe.

“Siamini” ilikuwa chereko. Janki wa Kitanga aliopoa manzi mwenye mahaba ya kibaikoko na kidumbaki, hakuamini kuchukua mtoto mkali. Halafu huyo manzi, kawatosa matajiri wenye mzigo.

Ujio wa pili, Matonya hakutaka mazoea. Hapo bado "Siamini" haijapoa, akaifanya Afrika Mashariki ilie kwa “Dunia Mapito.” Zikafuata tambo za kumpata “Vailet”. Sijui nani alichonga Tonya asingempata Vai wake!

Ngoja nikusimulie mshikaji wangu, Vailet ni mkwaju uliokaa kileleni kitambo kirefu bila kushuka wala kuchoka. Taifa likashudia ma-Vailet wengi. Walijitokeza kwenye vyombo vya habari, wakisema ni wao walioimbwa. Ni Bongo Flava na drama zake.

Wanamuziki wanadumu na mapenzi basi? Ilipofika mwaka 2008, Matonya alikwenda mpaka kwa mganga kumsaka “Anita”. Kazi ya Ambrose Dunga. Mom In Chief wa Bongo Flava, Lady Jaydee, aliweka sauti.

Ni Matonya aliyemfanya Irene Uwoya aitwe “Taxi Bubu” kwa kolabo na Fid Q, halafu akampigia magoti Aunty Ezekiel, ili tu amkubalie kuwa “Spare Tyre” mbele ya njemba yake, Mpoki.

Katiba ya Bongo Flava inatambua muhula wa utawala kimuziki ni mwaka mmoja bila nyongeza. Mwaka 2006, Matonya alipokaa on top, alivunja Katiba, akabaki madarakani 2007, 2008 hadi 2009. Raia walichekelea Tonya kuvunja Katiba.

Wengi hamjui how good the good old days, Matonya akiitawala Bongo Flava kama mali yake binafsi. Mapromota waliteseka kumpata. Bookings zimefunga mwaka mzima. Hakuna upenyo. Kila siku ziarani.

Nini nyumba na magari? Matonya alijenga mpaka hoteli. Unashangaa? Kwani ule u-busy, mwaka mzima anapiga show bila kupumzika, alikuwa anaingiza mawe?

Respect kwa Tonya mbili
 
Kweli kila zama za fursa zake kwa namna zile nyimbo zilihit, kwa dunia ya sasa ya social media na pesa za mtandaoni, Matonya, Mr Nice, Rose Muhando, Ferouz na Saida Karoli wangekuwa mabilionea

Muziki wanaudai hela nyingi sana sema ndio hivyo tena,

zile zama unaiuta hela za kule wanakomba mapromota na za huku mdosi anachukua chake

Basi ndio hivyo tena
 
Tunda Man wa Manzese ndio alikuwa mwandishi wa nyimbo za Matonya na watu wote waliokuwa wanashinda mbele ya Kitega Uchumi kwenye ofisi za Clouds wanalijua hilo. Kilichomsukuma Tunda kushika microphone mwenyewe ni hicho. Alikuwa anampa mwana mistari yenye vina lakini hapewi credit yoyote na mambo ya mitonyo mchizi anamruka viunzi.
Magumashi ni sababu nyingine inayozorotesha nyanja nyingi za maendeleo Bongo yetu.
 
Back
Top Bottom