Matibabu ya viongozi nje ya nchi - Aibu kwa Tanzania!

Huwa natatizika sana naposikia viongozi wetu wanasafiri all the way kutoka Tanzania mpaka Marekani au nchi nyingine yoyote ya Ulaya kwa ajili tu ya kuchunguzwa afya. Huwa najiuliza hivi madaktari wetu wa waliosomea hapahapa nchini hawawezi kufanya hiyo kazi? Kama hawawezi basi kwa maoni yangu ni wakati muhimu wa kuwawezesha ili waweze kuifanya hiyo kazi na ili kupunguza gharama za kwenda nje ya nchi.

Wala usisikitike kwanza ngoja nikutoe tongotongo kwanza unajua ni nani aliziuwa zile shule za vipaji maalumu?
Na nisababu zipi wakati wale viongozi na maprofesa, ma dr , mainjinia wa enzi hizo sio hawa wa dot.com ndio hizo shule ziliwatoa?

Pili unajua kuanzishwa kwa hizi shule binafsi ambazo kwa asilimia kubwa hakuna kiongozi wa sasa awaye yeyote mtoto ama mjukuu au kitukuu ndio wanaosoma shule hizo?
Na hizi za hali ya chini ukiunganisha za kata na hizi za serikali ambazo hazina tena nuru ile iliyokuwako miaka ya 90 kushuka chini ndizo wanazosoma watoto wa makabwela? Sasa hapo unataka kuniambia kuna kiongozi gani anayeweza kuzithamini hizi shule zetu makabwela wakati hapa kati pameshawekwa tabaka jibu unalo.

Tatu twende mahospitalini asilimia kubwa ya viongozi tuliokuwa nao sasa wengi wanatibiwa nje na familia zao , atakuwaje na uchungu au kizithamini hizi zetu huku makabwela tunazo lala kitanda kimoja wagonjwa wawili ?
Hapo jibu unalo sasa wapendwa nanukuu kwenye maandiko Matakatifu imeandikwa unapoona mmoja wenu anawakwaza ni heri kumfunga jiwe kubwa shingoni na kumtosa baharini ,
Na jiwe lenyewe ni hili kwa wale ambao hamjajiandikisha kwenye daftari la kudumu la kupiga kura siku ikifika shime tuende wote kuhakiki na kujiandikisha kwenye hilo daftari,
Ili ifikapo october tuweze kwa umoja tuweze kuwafunga jiwe kubwa hawa waliotukwaza mpaka tukawa kama yatima na kuishi kama wakimbizi kwenye nchi yetu wenyewe , yenye kila neema na baraka za Mungu tuwatupe baharini nayo ni kura yako ndio mkombozi wako na kizazi kijacho leo tupo kesho hatupo,
Shime wapendwa hakuna linaloshindikana chini ya jua na kwa pamoka twaweza Mungu ibariki Tanzania.
 
Watibiwe hapa nchini?hawa viongozi walivyo wabinafsi wenye majivuno wanaojiona wako tafauti na mtanzania wa kawaida asie na uwezo, hawa ambao wanataka gari ya milioni 200 wakati watoto wanakaa chini kwa kukosa madawati? Hawa wanaolipana posho kubwa kuliko mshahara wa kima cha chini na cha kati cha mfanyakazi wa serikali hiyohiyo?Hawa wanao safiri na SMG, bastola, shilingi na dola wakiwa ndani ya nchi, wakati albino wanauwawa kwa kukosa ulinzi, watu wanakufa kwa kukosa dawa? Ndugu yangu hwa viongozi wa nchi hii ni zaidi ya wafalme wa zama za kale waliobebwa mabegani na watumwa wangekuwa na uwezo hata chakula chao kingeagizwa kutoka nje ya nchi hii. Ni janga kubwa uwepo wao madarakani.
 
Vitendea kazi hakuna, Dawa na vifaa tiba hakuna, MSD inakopwa..... RIP Huduma za Afya TZ. Bora hata Kenya.
 
Wenye kuwapima ndiyo haohao wa kuwapigia kura kipindi cha uchaguzi kikifika kwa hiyo wanajua matokeo ya vipimo vyao yatawakwamisha kupata kura,

Jiulize ni nani anayepima chakula wanachokula viongozi wetu wakiwa ziarani ughaibuni.

Wakati mwingine magonjwa wanayachukua hukohuko ughaibuni, wametegwa, hawajitambui, hawachukui tahadhari, wanabweteka na ukarimu wanaopata wakienda ziarani kumbe wenzao wamekusudia kuwapunguza ili mikataba fake waliyo saini nao iendelee kuzineemesha nchi zao pindi walafi wetu watakapotoweka duniani
 
Ukitibiwa hapa hata transport allowance inakuwa ni kidogo, pia kujikweza kunachangia!
 
Huwa natatizika sana naposikia viongozi wetu wanasafiri all the way kutoka Tanzania mpaka Marekani au nchi nyingine yoyote ya Ulaya kwa ajili tu ya kuchunguzwa afya. Huwa najiuliza hivi madaktari wetu wa waliosomea hapahapa nchini hawawezi kufanya hiyo kazi? Kama hawawezi basi kwa maoni yangu ni wakati muhimu wa kuwawezesha ili waweze kuifanya hiyo kazi na ili kupunguza gharama za kwenda nje ya nchi.

Hili jambo asubuhi ya leo kama saa 11:30am nilikuwa naperuzi mahali nikaona wamesema Prof. Jakaya Kikwete, ameenda Marekani kwaajili ya kuchunguzwa afya sasa najiuliza kwanini asingeunganisha juzi kati alivyokuwa kwenye safari zake za kikazi hadi amekuja huku ndio aanze safari upya?
 
Nchi kama India unapata matibabu ya hali ya juu kwa gharama nafuu, tatizo kubwa kwa wagonjwa wengi ni nauli ya ndege ya kwenda India, lakini kwa gharama ya matibabu, Tanzania ( kama nchi nyingine ) matibabu yanayohitaji utaalam wa hali ya juu na vyombo vya kisasa ni ghali sana kufananisha na India kama huamini kamlaze mgonjwa wako Agha Khan Hospital au TMJ kwa wiki mbili au tatu halafu usikie habari yake ...
 
Ni jambo la aibu sana kwa viongozi wa afrika, yaani wao ndio wanaosababisha bara la afrika tuendelee kuteseka na kudharaurika kwa nchi za mangaribi, yaani kila kitu imekuwa ni ulaya tu, msaada, kutibiwa,.

hapo ndio utagundua chazo kikuu cha kuibiwa rasilimali zetu.

akili waafrika tunazo, wasomi wapo, rasimali za kutuwezesha kujenga hata hospitali ya rais pekee huo uwezo tunao.


kwa nini usiboreshe nyumbani kwako kwanza.

kwa akili ya harakara yaani raisi yuko tiyari kuua wakinamama wajawazito pamoja na wototo mia moja lakn yeye apone kwa garama yoyote.

kama umeshidwa kuboresha hospitali zako kwa nini na wewe usiende kutibiwa pale kama wanainchi waliokupa madaraka ya uraisi wanavyofanya?
 
Mimi naamini kabisa ya kwamba viongozi wetu kwenda kutibiwa nje ya nchi siyo kwa sababu ya Ubovu wa Muhimbili bali tatizo liko kwingine kabisa, na hapa nina ,,thought experiment" ambayo inasema hivi kwa mfano leo hii tuichukulie Hospitali ya rufaa Muhimbili kama ilivyo bila kubadilisha chombo chochote kile isipokuwa Madaktari, badala ya Madakatri wetu Waafrika wenzetu weusi waje Madaktari Wazungu ktk Ulaya na Marekani, au hata Wachina na Korea na Wajapani Je unafikiri Viongozi wetu hawataenda kutibiwa hapo Muhimbili?

Mimi nafikiri wengi sana wataenda kutibiwa hapo (Muhimbili), Mifano iko mingi hospitali za Wahindi zinaaminiwa klk za Wafrika weusi hata Mandela alitibiwa AK kwa sababu madaktari walikuwa ni Wazungu lkn kama kungekuwa hakuna daktari Mzungu basi wangempeleka Ulaya, angalia Mugabe naye anatibiwa Singapore kwa Wachina hivyo nafikiri tatizo siyo Muhimbili bali taizo ni kwamba Mwafrika mweusi hamuamini Mwafrika mweusi!
 
Back
Top Bottom