Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM



Thanks Jasusi, elimu ni pana na wala tuizungumzayo hatumaanishi ya vitabuni tu na wewe unafahamu fika juu ya niongeleacho. Mfano makamanda wa Chadema wanavyozunguka nchi nzima kutoa somo la uraia kwa wananchi na jinsi wananchi wanavyowaelewa na kuitikia kiasi cha kubadili kabisa wimbi la mtazamo wa kisiasa za mageuzi nchini mwetu. Hii ni moja wapo ya elimu ambayo wananchi wameikosa na CCM imefanya kila jitihada kuwanyima kwa ajili ya wachache wabaki kuwa katika nafasi wanazotaka bila kunyoshewa vidole na wananchi.

Serikali haijawa na mfumo wa kuwafunda watu namna ya kutoa elimu ya kujitegemea kama enzi za awamu ya kwanza ambapo vijijini kulikuwa na msukumo wa kujitegemea na watu baada ya kuhitimu shule walikuwa na mwelekeo wa uzalishaji vijijini. Leo elimu hiyo imekosekana, vijana toka vijijini baada ya kuhitimu shule wanakimbilia mijini. Ukiona vijana walivyojaa mijini huwezi kuamini wanakula nini na wanaajiriwa wapi na ndio maana wako waitikiaji wazuri sana kwenye mihadhara kwa kuwa hawana cha kufanya. Nenda vijiji wamebaki vijana wachache wana ambao nao wengi wanatafuta nafasi ya kwenda mijini na vijiji vimebaki makazi ya wazee tu.

Amini nisemayo kwani nimefanya utafiti na kushuhudia hali ilivyo vijijni na mijini. Shule za kata zimesaidia kuwashika walio mashuleni kubaki huko, na wakishahitimu wanatimkia mijini, ni dalili ya kukosa somo la elimu ya kujitegemea ambalo nio muhimu kwa mazingira ya kujiajiri vijijini ingawa nako kuna changamoto nyingi zinazotokana na kukosekana kwa miundo mbinu mbalimbali na kukosekana kwa utility.

..asante,kwa mwerevu atakuwa amekuelewa vema.na hapa ndo kuna shida!
 
Mshahara wangu umesomesha watoto ??? Ni lazima uwe Mbunge kufanya hili? Hivi kazi ya Ubunge ni ipi? This is too cheap, kwani kwa biashara zako tu ungeweza kusomesha watoto wengi zaidi ya hao Mr. Masha, well kubali kuwa ulishindwa kuzikonga nyoyo za wakazi wa Mwanza, next time if there will be next time kuwa karibu na wananchi waliokuchagua
 
kilikua cheo cha maana kwasbabu ya siasa za chama kimoja

u-DC ni sawa na u-CD tu kisiasa.... hasa kutokana na matendo ya baadhi ya ma DC kudhani kazi yao ni kusimamia interest za chama badala ya interest za wilaya

...kwanza hiki cheo kifutwe,hakina maadili yyte,matumizi mabaya ya rasilimali za taifa!...
 
hapana, umemiss his point

anazungumia knowledge... wakiwa na knowledge watafanya better decisions
Umemiss point tena
Masha yuko very clear, anazungumzia Historia ya Viongozi wetu hata sio Jamii yetu. VIONGOZI WETU, Kwamba tukijua Historical Background ya Ben Mkapa tutaipenda CCM. Kama Historia hii ni Knowledge inayoweza kunisaidia kurudi na mkate nyumbani jioni basi uko sawa.
 
Mkuu, avatar yako ile tuliizoea sana irudishe kamanda, mpaka nimejiuliza huyu ni Mungi yupi but siyo issue kanyaga twende,

Mkuu avatar ni ya yule yule we sema hapo nimepo kwenye suti kwa mapunziko, mapambano yakianza natinga tena!
 
Huyu Masha anavuta shuka kumekucha leo ndio analifaham hilo?
 
Sasa hizo shule za kata mliwajengea kina nani kama nyie watoto wenu wanasoma nje?

Mwenye nafasi ya kwenda kulima shamba ng'ambo ya pili hana kosa kwa vile nafasi inamruhusu, kwani ninayelalamika labda uwezo wa kufikia sina, laiti ningekuwa nao huenda ningeenda mbali ya hapo.
 
Na aliucheza bahati mbaya Mpinzani wake alikuwa Makini Ukamshinda; Wakumbuka alijitangaza yeye na Ngeleja wamepita bila kupingwa? Anasubiri kuapishwa tu na Rais? Alimsingizia Mpinzani wake Vidudu Vya Ajabu; Leo hii anaongea haongelei hayo baada ya zaidi ya Nusu Mwaka anapanga Interview akiwa anajua ana Jambo Jipya kila Mtu atafurahia na Masikini kama Sisi tutalipenda, anajitokeza anatunusisha alivyofanya Mazuri... Woote tunalala chini na kumpigia Makofi...

Wakati wa kutafuta kuingia mjengoni ye yote aatatumia kila upenyo unaowezekana kumpitisha kwa urahisi, lakini hilo si la kuzuia kutoa ya moyoni ambayo yana manufaa kwa nchi na mageuzi kwa nchi yetu.
 
sikubaliani na analysis ya kuwa vijana wakielimishwa/wakielimika wataona mazuri ya CCM na kukikubali. In fact ni kinyume chake. kwa yeyote mwenye knowledge na asiye beneficiary wa moja kwa moja wa CCM, hawezi katu kukishabikia CCM. kwa sababu ndogo tu. Kwa mwenye knowledge ataona madudu makubwa yafanywayo na CCM na hatokubali.

lakini kwa upande mwingine pia, tumeona jinsi CCM inavyo manipulate watu wenye elimu ndogo na uelewa mdogo hususan vijijini na hasa maeneo ya kusini mwa nchi. na kwa kutumia huo uelewa wao mdogo wamekuwa wakijipatia kura zao kwa wingi. so hii hypothesis ya Masha sio sahihi
 
Wakati wa kutafuta kuingia mjengoni ye yote aatatumia kila upenyo unaowezekana kumpitisha kwa urahisi, lakini hilo si la kuzuia kutoa ya moyoni ambayo yana manufaa kwa nchi na mageuzi kwa nchi yetu.

LOL... Angalia familia inayomzunguka ameisaidiaje? Au Amesaidia hao wanafunzi kujitangaza? Hizo ndio siasa za Sasa
Nimesomesha hawa, Nimejenga hiki, Anaweza kufanya hivyo, kama ana Nyumba South Africa...

Angalia Amesaidia Ndugu Wangapi halafu uje uniambia kweli huyu ni mtu swafi, ni hivyo alivyo pleasing public for his own advantages, angalia sasa alivyopata hawa Mashabiki wa ajabu

Mnadhani alipokuwa waziri nani angefika ofisini kwake? mlisha wahi kuuliza watu waliomjua jinsi walivyonyanyasika?
 
LOL... Angalia familia inayomzunguka ameisaidiaje? Au Amesaidia hao wanafunzi kujitangaza? Hizo ndio siasa za Sasa
Nimesomesha hawa, Nimejenga hiki, Anaweza kufanya hivyo, kama ana Nyumba South Africa...

Angalia Amesaidia Ndugu Wangapi halafu uje uniambia kweli huyu ni mtu swafi, ni hivyo alivyo pleasing public for his own advantages, angalia sasa alivyopata hawa Mashabiki wa ajabu

Mnadhani alipokuwa waziri nani angefika ofisini kwake? mlisha wahi kuuliza watu waliomjua jinsi walivyonyanyasika?

Naona tumetoka nje ya uringo kwani mada haikulewa kumjadili Masha, ila kauli yake ndiyo tunayoijadili. Kauli na uchambuzi wa Masha una maana gani kwa umma. Kuhusu kukosekana kwa elimu kwa vijana ambao awali elimu ilikuwa inafundishwa hasa vijijini kujitetemea, leo kwa nini vijana karibu wote wanakimbilia mijini badala ya kufanya uzalishaji vijijini? Kuna tatizo la uelimishaji umma hapa. Elimu ni pana si kusoma vitabu tu.

Masha ni sawa na mchezaji wa basketi, mambo yakimzidi uwanjani huenda kupumzika kwenye benchi na kutafakari yaliyojilia hadi kuzidiwa kete. Kutafakari huko ni muhimu na ndio maana tunamwona ameamua kuchukua mkondo wake ambao anaona unamlindia heshima yake kuliko hizi nafasi za utwa na utwana na kuvuana nguo mbele ya wakwe.

Masha kajadili jambo zuri ambalo nimependezwa nalo. Wengi tatizo letu kujadili jambo tunamtazama nani kasema hayo badala ya kufikiria maudhui ya mada yana maana gani kwetu. Binadamu si kama jiwe. Tujifunze static na dynamic. Kwa vyo vyote binadamu hubadilika na mazingira yanayomzunguka ni darasa kubwa la maisha kwa wanofungua akili tofauti na jiwe ambalo lipo kama lilivyo miaka nenda rudi.

 
sikubaliani na analysis ya kuwa vijana wakielimishwa/wakielimika wataona mazuri ya CCM na kukikubali. In fact ni kinyume chake. kwa yeyote mwenye knowledge na asiye beneficiary wa moja kwa moja wa CCM, hawezi katu kukishabikia CCM. kwa sababu ndogo tu. Kwa mwenye knowledge ataona madudu makubwa yafanywayo na CCM na hatokubali.

lakini kwa upande mwingine pia, tumeona jinsi CCM inavyo manipulate watu wenye elimu ndogo na uelewa mdogo hususan vijijini na hasa maeneo ya kusini mwa nchi. na kwa kutumia huo uelewa wao mdogo wamekuwa wakijipatia kura zao kwa wingi. so hii hypothesis ya Masha sio sahihi

Kuelimika kwa vijana hakuna maana ya kuyaelewa ya Chama fulani, ila elimu ya maisha. Vijana wanachofuata Chadema si kupata ya Chadema ila kupata kiu ya elimu kwa ajili ya maisha yao.
 
Masha: Vijana wengi hawaipendi CCM


ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana, Lawrence Masha, amesema vijana wengi nchini hawataki CCM kwa sababu hawaoni kilichofanyika tangu kilipoanzishwa.

Masha alisema wananchi wanahitaji kuona mabadiliko na kwamba, hali hiyo inatokana na kutosoma vizuri historia ya Tanzania. Akizungumza kwenye kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha EATV, alisema hatua ya kutopenda chama hicho imetokana na vijana kutosoma historia.

“Vijana wengi hawaipendi CCM, wengi wanataka mabadiliko… siyo kosa lao, hawakufundishwa. Kuna wakati nilikuwa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza nazungumza, kijana mmoja akasimama akasema nyie, wazee ndiyo wanarudisha nyuma nchi. Nikaangalia nyuma nikajiuliza huyo mzee yuko wapi... Nikagundua kumbe na mimi ambaye nilikuwa najiona kijana kniko kwenye kundi la wazee” alisema Masha.

Masha ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini, Dk Fortunatus Masha, alisema vijana wengi wanapenda mabadiliko ya haraka jambo ambalo hawalioni ndani ya CCM na kuongeza kuwa, hali hiyo inasababishwa na kutokuwapo kwa mkakati wa kuwafundisha historia ya mafanikio ya Serikali na viongozi wake.

“Leo hii ukienda Nairobi ukitaka kitabu kuhusu maisha ya Raila Odinga utaipata, ukitaka historia ya (Daniel) Moi .. Kenyatta utaipata. Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili ajue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna,” alisema Masha na kuongeza:

“Sasa kama mtoto ambaye anataka kujua nchi yake, anakosa hata pa kuipata, nchi yake ikoje, marais waliotawala, tumefikaje hapa? Lazima waseme tumekuwa maskini kwa sababu ya chama ambacho kiko madarakani.”

Kuhusu kushindwa kwake ubunge mwaka 2010, Masha alisema amekubali kushindwa na anaendelea na kazi zake nyingine.

“Ukiingia kwenye uchaguzi ni sawa tu na kuingia kwenye mpira, kuna kushinda na kushindwa, kikubwa ukishashindwa kubali matokeo endelea na maisha. Tatizo watu wengi na hasa wanasiasa wenzangu hawana kazi nyingine za kufanya,” alisema Masha.

Alipinga madai kuwa kipindi chake cha ubunge na uwaziri hakufanya lolote katika jimbo lake, badala yake alitoa mifano ya kazi alizofanya na kwamba, wanaoeneza hayo ni watu wenye fitina.

“Sidhani kama ni kweli, unajua kwenye siasa kuna fitina imani yangu ni kwamba kazi yangu nilifanya na kazi yangu ya uwaziri niliifanya. Of course (bila shaka) kutokana na mfumo tulionao, mwenzako lazima akumalize ili akushinde,” alisema Masha na kuongeza:

“Leo hii tunapoongelea Nyamagana kuna chuo cha polisi kimejengwa, kuna Sekondari ya Mkolani imejengwa nje ya bajeti ya Serikali… ni kutoka kwa wafadhili na marafiki, there’s a lot of works (kuna kazi nyingi).”

Alisema alikuwa akisomesha watoto 236 kwa mshahara wake wa ubunge na kwamba, tangu alipoingia bungeni mshahara wake ulikuwa ukipelekwa jimboni kusaidia wasiokuwa na uwezo.

“Leo hii ndiyo watu wanakumbuka, ndiyo nasema leo hii hata mke wangu na watoto wangu nao wafurahi kidogo kile ninachokipata, nipeleke kwenye maendeleo ya familia,” alisema.

Hata hivyo, Masha alisema kazi za siasa zinahitaji uvumilivu hivyo alijitahidi kuvumilia changamoto hizo kipindi chote cha uongozi wake.
Kumbe njaa ikiuma unazinduka usingizini. Shibe ilimlevya wakati ule akashindwa kufanyia kazi anayoyasema.
 
Naona tumetoka nje ya uringo kwani mada haikulewa kumjadili Masha, ila kauli yake ndiyo tunayoijadili. Kauli na uchambuzi wa Masha una maana gani kwa umma. Kuhusu kukosekana kwa elimu kwa vijana ambao awali elimu ilikuwa inafundishwa hasa vijijini kujitetemea, leo kwa nini vijana karibu wote wanakimbilia mijini badala ya kufanya uzalishaji vijijini? Kuna tatizo la uelimishaji umma hapa. Elimu ni pana si kusoma vitabu tu.

Masha ni sawa na mchezaji wa basketi, mambo yakimzidi uwanjani huenda kupumzika kwenye benchi na kutafakari yaliyojilia hadi kuzidiwa kete. Kutafakari huko ni muhimu na ndio maana tunamwona ameamua kuchukua mkondo wake ambao anaona unamlindia heshima yake kuliko hizi nafasi za utwa na utwana na kuvuana nguo mbele ya wakwe.

Masha kajadili jambo zuri ambalo nimependezwa nalo. Wengi tatizo letu kujadili jambo tunamtazama nani kasema hayo badala ya kufikiria maudhui ya mada yana maana gani kwetu. Binadamu si kama jiwe. Tujifunze static na dynamic. Kwa vyo vyote binadamu hubadilika na mazingira yanayomzunguka ni darasa kubwa la maisha kwa wanofungua akili tofauti na jiwe ambalo lipo kama lilivyo miaka nenda rudi.


He was not on the same game with you from the start; Nadhani alikuwa na best opportunities than most of us from way back, na wengi wao kama yeye wana NGO's kusaidia Nchi zao; Sio kugombea Ubunge na Madini ili kuendeleza ulaji.

Sasa hivi angekuwa anafanya kwa Wananchi kwa Yeye na Baba yake walivyopata Nje na Hapa Nchini Wote Wamekuwa Wabunge Mmojwa wa East Africa na Mwingine wa Tanzania hapo ingekuwa bora; Kama kweli unaipenda nchi yako

Vijana sio hawaipendi CCM; Mimi ni wa Mwanza watu wengi walikuwa na Imani na Lau, lakini ukienda huko kila mtu ana Jambo la kukueleza kuhusu alivyotenda; kabla ya kusifia fanya Uchunguzi wako be fair; Usione Mtu kwenye TV na Maneno Mazuri ukanunuliwa. Hapo hatutaweza kuwa na Viongozi bora hata kidogo kila siku tutachagua Mafisadi.
 
Alichoongea Masha kina mashiko, suala la kwamba alikuwa waziri au mbunge si la msingi sana, binafsi naamini wengi walio CCM kama viongozi kuna wakati akili zao kama wanaziacha mahali wanabaki kama misukule tu, wakitoka ndiyo akili zao zinarudi wanaanza kuuona ukweli. Hongera Masha endelea na maisha yako ya ujasiriamali na siasa ikibidi achana nayo lakini usihame CCM.
Ni mtizamo wako tu!
 
Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili nijue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna,” alisema Masha na kuongeza:


Sasa hizo shule za kata mliwajengea kina nani kama nyie watoto wenu wanasoma nje?


Kwanza kwa aliyekuwa waziri kusema anaelimisha wanae nje bila hofu niishara kwamba hajali maslahi ya wananchi.
Out of touch.
CCM sio TANU
 
Vijana hawahitaji kufundishwa historia ya mafanikio, wanahitaji kuona mafanikio!!
 
Back
Top Bottom