Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

Masha alikuwa mbuge makini sana,sisi wana nyamagana tunakuhitaji tena, kwa sasa tuna chizi hajui alifanyalo ***** sana,wenje hufai
 
It is not correct to say, as Masha does, that there is a complete dearth of books about contemporary Tanzania. It is my ardent hope that Masha will find time to read the following three books, in the order given:
1. The Making of Tanganyika, Judith Listowel, London, Chattto & Widus, 1965.

2. From Goatherd to Governor: The Autobiography of Edwin Mtei, Edwin Mtei, Mkuki and Nyota
Publishers, 2009.
3. Tanzania in Transition From Nyerere to Mkapa, Kjeli Havnevik and Aika Isinika (eds.), Mkuki and
Nyota Publishers, 2010.


hawana hulka ya kusoma vitabu. ila waulize kuwa Dsm kuna night club ngapi
 
ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana, Lawrence Masha, amesema vijana wengi nchini hawataki CCM kwa sababu hawaoni kilichofanyika tangu kilipoanzishwa.

Masha alisema wananchi wanahitaji kuona mabadiliko na kwamba, hali hiyo inatokana na kutosoma vizuri historia ya Tanzania. Akizungumza kwenye kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha EATV, alisema hatua ya kutopenda chama hicho imetokana na vijana kutosoma historia.
“Vijana wengi hawaipendi CCM, wengi wanataka mabadiliko… siyo kosa lao, hawakufundishwa. Kuna wakati nilikuwa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza nazungumza, kijana mmoja akasimama akasema nyie, wazee ndiyo wanarudisha nyuma nchi. Nikaangalia nyuma nikajiuliza huyo mzee yuko wapi... Nikagundua kumbe na mimi ambaye nilikuwa najiona kijana kniko kwenye kundi la wazee” alisema Masha.

Masha ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini, Dk Fortunatus Masha, alisema vijana wengi wanapenda mabadiliko ya haraka jambo ambalo hawalioni ndani ya CCM na kuongeza kuwa, hali hiyo inasababishwa na kutokuwapo kwa mkakati wa kuwafundisha historia ya mafanikio ya Serikali na viongozi wake. “Leo hii ukienda Nairobi ukitaka kitabu kuhusu maisha ya Raila Odinga utaipata, ukitaka historia ya (Daniel) Moi .. Kenyatta utaipata. Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili nijue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna,” alisema Masha na kuongeza:

“Sasa kama mtoto ambaye anataka kujua nchi yake, anakosa hata pa kuipata, nchi yake ikoje, marais waliotawala, tumefikaje hapa? Lazima waseme tumekuwa maskini kwa sababu ya chama ambacho kiko madarakani.”

Kuhusu kushindwa kwake ubunge mwaka 2010, Masha alisema amekubali kushindwa na anaendelea na kazi zake nyingine. “Ukiingia kwenye uchaguzi ni sawa tu na kuingia kwenye mpira, kuna kushinda na kushindwa, kikubwa ukishashindwa kubali matokeo endelea na maisha. Tatizo watu wengi na hasa wanasiasa wenzangu hawana kazi nyingine za kufanya,” alisema Masha.

Alipinga madai kuwa kipindi chake cha ubunge na uwaziri hakufanya lolote katika jimbo lake, badala yake alitoa mifano ya kazi alizofanya na kwamba, wanaoeneza hayo ni watu wenye fitina. “Sidhani kama ni kweli, unajua kwenye siasa kuna fitina imani yangu ni kwamba kazi yangu nilifanya na kazi yangu ya uwaziri niliifanya. Of course (bila shaka) kutokana na mfumo tulionao, mwenzako lazima akumalize ili akushinde,” alisema Masha na kuongeza:

“Leo hii tunapoongelea Nyamagana kuna chuo cha polisi kimejengwa, kuna Sekondari ya Mkolani imejengwa nje ya bajeti ya Serikali… ni kutoka kwa wafadhili na marafiki, there’s a lot of works (kuna kazi nyingi).” Alisema alikuwa akisomesha watoto 236 kwa mshahara wake wa ubunge na kwamba, tangu alipoingia bungeni mshahara wake ulikuwa ukipelekwa jimboni kusaidia wasiokuwa na uwezo.

“Leo hii ndiyo watu wanakumbuka, ndiyo nasema leo hii hata mke wangu na watoto wangu nao wafurahi kidogo kile ninachokipata, nipeleke kwenye maendeleo ya familia,” alisema. Hata hivyo, Masha alisema kazi za siasa zinahitaji uvumilivu hivyo alijitahidi kuvumilia changamoto hizo kipindi chote cha uongozi wake.


Mwananchi

Mbona heading ya Thread yako haifanani na kilichosemwa na Masha? Ni uwezo mdogo wa kuelewa au una chuki binafsi na chama tawala?
 
Nimekubaliana na majibu ya Masha pamoja na mchepuo wa maisha yake baada ya kubwagwa ubunge. Kimsingi siasa ni mchezo mchafu, ukiamua kuuendeleza unaweza kushtukia hata umekufilisi kama kama hukufanikiwa nafasi uliyogombea. Na walioshinda ndio maana wanafanya jitihada kubwa na kutumia njia haramu kurudisha gharama walizotumia kupata nafasi hizo.

Kama nafasi inaruhusu bora kuamua kuendesha shughuli binafsi zinazokupatia lishe na kuyaendesha maisha kwa utulivu kuliko haya ya nafasi za kisiasa za kunyoosheana vidole kila kukicha bila kikomo.

Na aliucheza bahati mbaya Mpinzani wake alikuwa Makini Ukamshinda; Wakumbuka alijitangaza yeye na Ngeleja wamepita bila kupingwa? Anasubiri kuapishwa tu na Rais? Alimsingizia Mpinzani wake Vidudu Vya Ajabu; Leo hii anaongea haongelei hayo baada ya zaidi ya Nusu Mwaka anapanga Interview akiwa anajua ana Jambo Jipya kila Mtu atafurahia na Masikini kama Sisi tutalipenda, anajitokeza anatunusisha alivyofanya Mazuri... Woote tunalala chini na kumpigia Makofi...
 
MASHA ANA ufalme wa kumtosha, hahitaji JK... pia uelewe JK ana less than 50% influence kwenye serikali iliyo madarakani

wewe unaangalia juu, kazi zote zipo local government....

komaa-komaa ujue maisha,

inatia aibu sana mtu kama muhingo, a well seasoned journalist anakubali kuwa DC, what a waste!!

tubadilike, we can sustain our families bila hata political appointments

Jenerali Ulimwengu alishawahi kuwa mkuu wa wilaya?, je ilikuwa bahati mbaya au U-DC wa hivi sasa ni too dilute? najaribu kufikiria U-DC wa Muhingo na makala zake za nyuma hasa before uchaguzi
 
Kwa ilo la vitabu nakubaliana naye asilimia mia moja,watu badala ya kutunga vitabu vyenye manufa kwa taifa na vitakavodumu vizazi na vizazi wanatunga vya Rushwa kwa mujibu wa biblia na suna.I know Masha personally,he is a very nice guy,sincere and transparent.I beleive one day he will come back in politics with a very loud bang.I always play for him.
 
Kama ni kweli kwamba vijana hawaipendi ccm kwa sababu hawakufundishwa historia ya Tanzania, ni afadhali kwa faida ya ccm hawakufundishwa, maana wangefundishwa wangeshaipindua hii serikali ya kihuni zamani sana. Ametolea mfano kenya, kwamba walifundishwa historia. Ndiyo maana kanu haipo madarakani, ni kwa sababu waliijua historia ya kenya.
Mkuu, avatar yako ile tuliizoea sana irudishe kamanda, mpaka nimejiuliza huyu ni Mungi yupi but siyo issue kanyaga twende,
 
Masha: Vijana wengi hawaipendi CCM


ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana, Lawrence Masha, amesema ...... Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili ajue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna," alisema Masha ......Hata hivyo, Masha alisema kazi za siasa zinahitaji uvumilivu hivyo alijitahidi kuvumilia changamoto hizo kipindi chote cha uongozi wake.

Hapo kwenye redi : Tulisema Mafisadi wameanzisha shule za Kata kwa walala hoi ili hali Watoto wao wote wamewapeleka nje ya nchi kwa pesa za kifisadi ambazo zingepaswa kuweka vitabu na kuajiri walimu bora kwenye shule zetu hapa nyumbani. Mabadiliko Tanzania ni ya lazima. CDM jiandaeni kuchukua nchi 2015. Tumechoka na unafiki wa hawa CCM-Fisadi !!
 
Jenerali Ulimwengu alishawahi kuwa mkuu wa wilaya?, je ilikuwa bahati mbaya au U-DC wa hivi sasa ni too dilute? najaribu kufikiria U-DC wa Muhingo na makala zake za nyuma hasa before uchaguzi

Ni kama laaana vile. Upeo wa wa wengi wa wana JF ni wa kupandikizwa , wengi humu wanasema walizchokisikia na siyo walichokiona wala kukifanyia utafiti. Kinga kubwa ya mawazo yao imekuwa ni matusi kwa vile wantambua wazi kuwa mtu mwenye akili,elimu, busara na hekima hawezi kamwe kuwarudishia madudu waliochangia. Kuweni na fikra pevu humu Jf la sivyo ni picha chafu sana kama kweli tutajiita kioo cha jammii.

Lugha kama za shost nk. mara nyingi nazisikia kwenye tasnia ya muziki tena ule wa taarab na sifa za wamiliki wake kila mmoja anazijua, je nawe tukuweke kundi hilo?
 
Wakuu Ngoja nichomoke kwenye hii thread Mimi upande wangu nilikuwa simpendi Masha kabisa nawatakia hoja njema

Nakuunga mkono Mkuu. Kiongozi yeyote anayetumia Cheo chake kudharau watu simpendi. Huyu nilianza kumchukia tangu alipokoromea Mlinzi pale JMall na kumwuliza kama hajui yeye (Masha) ni nani ili aachwe aendelee kuongea na simu kwenye kibanda cha ATM. Halafu, inakuwaje ana mtoto wa umri wa miaka kumi na saba na bado anajiweka kwenye kundi la vijana ? Kwa nini atumie pesa yake kusomesha watoto 236 ? Kazi ya Mbunge sio kutumia pesa yake kuleta maendeleo, bali kuishawishi Serikali kuleta maendeleo. Kwa nini mtoto wake asome Africa Kusini, shule za Kata wanamjengea nani ? Alipokuwa Mbunge na Waziri alifanya nini ili haom vijana wafundishwe historia ya nchi yao !!! Sisitaki mbichi hizi !!!!!
 
Masha: Vijana wengi hawaipendi CCM


ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana, Lawrence Masha, amesema vijana wengi nchini hawataki CCM kwa sababu hawaoni kilichofanyika tangu kilipoanzishwa.

Masha alisema wananchi wanahitaji kuona mabadiliko na kwamba, hali hiyo inatokana na kutosoma vizuri historia ya Tanzania. Akizungumza kwenye kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha EATV, alisema hatua ya kutopenda chama hicho imetokana na vijana kutosoma historia.

“Vijana wengi hawaipendi CCM, wengi wanataka mabadiliko… siyo kosa lao, hawakufundishwa. Kuna wakati nilikuwa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza nazungumza, kijana mmoja akasimama akasema nyie, wazee ndiyo wanarudisha nyuma nchi. Nikaangalia nyuma nikajiuliza huyo mzee yuko wapi... Nikagundua kumbe na mimi ambaye nilikuwa najiona kijana kniko kwenye kundi la wazee” alisema Masha.

Masha ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini, Dk Fortunatus Masha, alisema vijana wengi wanapenda mabadiliko ya haraka jambo ambalo hawalioni ndani ya CCM na kuongeza kuwa, hali hiyo inasababishwa na kutokuwapo kwa mkakati wa kuwafundisha historia ya mafanikio ya Serikali na viongozi wake.

“Leo hii ukienda Nairobi ukitaka kitabu kuhusu maisha ya Raila Odinga utaipata, ukitaka historia ya (Daniel) Moi .. Kenyatta utaipata. Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili ajue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna,” alisema Masha na kuongeza:

“Sasa kama mtoto ambaye anataka kujua nchi yake, anakosa hata pa kuipata, nchi yake ikoje, marais waliotawala, tumefikaje hapa? Lazima waseme tumekuwa maskini kwa sababu ya chama ambacho kiko madarakani.”

Kuhusu kushindwa kwake ubunge mwaka 2010, Masha alisema amekubali kushindwa na anaendelea na kazi zake nyingine.

“Ukiingia kwenye uchaguzi ni sawa tu na kuingia kwenye mpira, kuna kushinda na kushindwa, kikubwa ukishashindwa kubali matokeo endelea na maisha. Tatizo watu wengi na hasa wanasiasa wenzangu hawana kazi nyingine za kufanya,” alisema Masha.

Alipinga madai kuwa kipindi chake cha ubunge na uwaziri hakufanya lolote katika jimbo lake, badala yake alitoa mifano ya kazi alizofanya na kwamba, wanaoeneza hayo ni watu wenye fitina.

“Sidhani kama ni kweli, unajua kwenye siasa kuna fitina imani yangu ni kwamba kazi yangu nilifanya na kazi yangu ya uwaziri niliifanya. Of course (bila shaka) kutokana na mfumo tulionao, mwenzako lazima akumalize ili akushinde,” alisema Masha na kuongeza:

“Leo hii tunapoongelea Nyamagana kuna chuo cha polisi kimejengwa, kuna Sekondari ya Mkolani imejengwa nje ya bajeti ya Serikali… ni kutoka kwa wafadhili na marafiki, there’s a lot of works (kuna kazi nyingi).”

Alisema alikuwa akisomesha watoto 236 kwa mshahara wake wa ubunge na kwamba, tangu alipoingia bungeni mshahara wake ulikuwa ukipelekwa jimboni kusaidia wasiokuwa na uwezo.

“Leo hii ndiyo watu wanakumbuka, ndiyo nasema leo hii hata mke wangu na watoto wangu nao wafurahi kidogo kile ninachokipata, nipeleke kwenye maendeleo ya familia,” alisema.

Hata hivyo, Masha alisema kazi za siasa zinahitaji uvumilivu hivyo alijitahidi kuvumilia changamoto hizo kipindi chote cha uongozi wake.

Ningalipata chanzo cha hii habari ningalichangia japo kidogo
 
yawezekana aliona na alizungumza, ila nijuavyo mimi si kila wanachozungumza kinaenda media

ukizungumzuza cha maana kazima kitokee kwenye media, labda kama alizungumza nyumbani kwake na nwanae, ansmd he was supposed to do not just talk.
 
Gamba ni gamba tu. Kama shule imejengwa kwa nini mtoto wake asisome hapo, badala yake anasoma South Agrica? Hiyo ni shule au majengo tu?
 
Observation ya Masha imekuja wakati mwafaka.
Asitake kutuaminisha kwamba historia ya maendeleo ya nchi hii haijaandikwa, hii si kweli. Kuna vitabu lukuki vimeandika hatua mbalimbali za maendeleo tangu enzi za mwali mpaka hapa tulipo, labda atuambie huwa havisomi vitabu hivyo. Namshauri asome kitabu cha Prof. Seithy Chachage cha 'MAKUWADI WA SOKO HURIA', ajua sisiem ilipotutoa na kututupa. Nadhani ktabu hiki kinaweza kumpa jibu la maswali aliyoulizwa na vijana 'Wasioona' chochote ilichofanya sisiem.
 
Mkuu, mapungufu aliyonayo mtu huonwa na jirani yake. It is almost impossible to identify your defects. He is out of system, where he is currently he can identify the defects.
 
Nakuunga mkono Mkuu. Kiongozi yeyote anayetumia Cheo chake kudharau watu simpendi. Huyu nilianza kumchukia tangu alipokoromea Mlinzi pale JMall na kumwuliza kama hajui yeye (Masha) ni nani ili aachwe aendelee kuongea na simu kwenye kibanda cha ATM. Halafu, inakuwaje ana mtoto wa umri wa miaka kumi na saba na bado anajiweka kwenye kundi la vijana ? Kwa nini atumie pesa yake kusomesha watoto 236 ? Kazi ya Mbunge sio kutumia pesa yake kuleta maendeleo, bali kuishawishi Serikali kuleta maendeleo. Kwa nini mtoto wake asome Africa Kusini, shule za Kata wanamjengea nani ?

Mkuu nilikuwa nimechomoka lakini imebidi nirudi huko kwenye red kumenifurahisha sana haoni aibu kutuambia sisi ambao watoto wetu wanasoma hizo shule za kata yeye wa kwake yupo Africa kusini. kama maendeleo yapo hapa mbona mtoto wake yupo nje mkuu ngoja nisindelee ban inaweza ikaja sasa hivi
 
CAndid Scope naona unamtetea sana huyu jamaa eti katoa ushauri mzuri. Mtoto wa masha ana miaka 17 yuko South Africa kwenye shule nzuri na bora. Kuna kijana kamwambia wewe mzee ndo muharibifu wa maisha yetu na yuko kwenye vyuo vyetu kapa nchini. lakini pia kaanzisha shule pale mkolani je ina walimu wenye vifaa vya kujitoshereza. Hiyo shule kwa nini asisome pia huyo mwanae wa miaka 17. Ameona tofauti ipi mpaka ampeleke SA. But, Cs shule hizi zilianzishwa kisiasa kama unavoona maduka ya NAtional Milling yalivyopukutika. Shule zazina walimu wa kutosha, maabara hakuna, na mambo mengine halafu leo unawaeleza mambo ya Historia. Maanake pia ni kuwa MAsha anajua kuwa tangia darasa la kwanza mpaka chuo kikuu asomacho huyo kijana wa St.Augustine hakuna vitabu vya Historia. Yeye kama mdau na Waziri mstaafu(mshindwa) hakuliona hilo??
 
Back
Top Bottom