Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,003
- 964
MBUNGE MHE. MARTHA GWAU AWAFUNDA WAKINAMAMA NA MABINTI WA SHULE SIKU YA WANAWAKE DUNIANI
Mhe. Martha Gwau, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Singida alikuwa ni miongoni mwa viongozi waliofika shule ya Sekondari Ilongero kuzungumza na kusikiliza midahalo miwili ya mabinti wa shule pamoja mdahalo wa wazazi, midahalo yote ililenga kukomboa kizazi chetu kutoka kwenye makuzi yasiyofaa na ukatili kwa watoto wetu.
Mbunge huyo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni ramsi katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa Ilongero Singida vijijini.
Mbunge huyo aliwasihi sana wazazi kutokuwa sehemu ya kuficha watu wanaoharibu watoto wetu vilevile kuwa askari namba moja wa kuwalinda watoto na kuwapa malezi mema yatakayowaandaa kuwa raia wema kwa taifa, vilevile aliwataka wakina mama wachangamkie fursa mbalimbali za serikali lakini wajitahidi sana kutunza uaminifu
Mwisho, aliishukuru na kuipongeza halmashauri chini ya mkurugenzi wao Bi. Esther Chaula kwa maandalizi mazuri ya maadhimisho hayo.
Imetolewa na;
Ofisi ya Mbunge Viti Maalum Mkoa Singida
#MarthaGwauKazini
#KaziIendelee
Mhe. Martha Gwau, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Singida alikuwa ni miongoni mwa viongozi waliofika shule ya Sekondari Ilongero kuzungumza na kusikiliza midahalo miwili ya mabinti wa shule pamoja mdahalo wa wazazi, midahalo yote ililenga kukomboa kizazi chetu kutoka kwenye makuzi yasiyofaa na ukatili kwa watoto wetu.
Mbunge huyo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni ramsi katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa Ilongero Singida vijijini.
Mbunge huyo aliwasihi sana wazazi kutokuwa sehemu ya kuficha watu wanaoharibu watoto wetu vilevile kuwa askari namba moja wa kuwalinda watoto na kuwapa malezi mema yatakayowaandaa kuwa raia wema kwa taifa, vilevile aliwataka wakina mama wachangamkie fursa mbalimbali za serikali lakini wajitahidi sana kutunza uaminifu
Mwisho, aliishukuru na kuipongeza halmashauri chini ya mkurugenzi wao Bi. Esther Chaula kwa maandalizi mazuri ya maadhimisho hayo.
Imetolewa na;
Ofisi ya Mbunge Viti Maalum Mkoa Singida
#MarthaGwauKazini
#KaziIendelee