Ndugu wanaJF, nimesafiri kikazi nipo eneo la Mbulu mjini,top story hapa mjini ni kuhusu kuzomwea na kuitwa mwizi waziri Marmo.
Habari zinasema alifika kijijini kwao katika harakati zake za kampeni kwa mbwembwe za magari yaliyopambwa picha zake na za JK na mziki mkubwa wa kwaya yao ya TOT,wanakijiji waliposikia walijikusanya na kuanza kupiga yowe la mwizi wa kura! Mwizi wa kura kwani wanamshutumu kuwa huwa anashinda ubunge kwa kuiba kura kwa miaka yote na kibaya zaidi katika kura za maoni za ndani ya CCM NEC haikurudisha jina la mgombea aliyekuwa chaguo lao.
Watu wamemchoka Marmo kupita kiasi kwani wanadai amejaa kibri na majivuno, katika mkutano wake mmoja wa kampeni eneo linaitwa Haydom alishawaambia wakazi wa eneo hilo hata kama wasipompigia kura atashinda kwa kura za watu wanaovaa mashuka wasio na elimu huko vijijini. Kilichotokea hawa watu wa Hydom wakawasimulia hao wanaoitwa hawana elimu, alipoenda kifanya kampeni wakamtimua kwamba wameishapata habari jinsi anavyowadharau, kazi anayo mwaka huu.
Habari zinasema alifika kijijini kwao katika harakati zake za kampeni kwa mbwembwe za magari yaliyopambwa picha zake na za JK na mziki mkubwa wa kwaya yao ya TOT,wanakijiji waliposikia walijikusanya na kuanza kupiga yowe la mwizi wa kura! Mwizi wa kura kwani wanamshutumu kuwa huwa anashinda ubunge kwa kuiba kura kwa miaka yote na kibaya zaidi katika kura za maoni za ndani ya CCM NEC haikurudisha jina la mgombea aliyekuwa chaguo lao.
Watu wamemchoka Marmo kupita kiasi kwani wanadai amejaa kibri na majivuno, katika mkutano wake mmoja wa kampeni eneo linaitwa Haydom alishawaambia wakazi wa eneo hilo hata kama wasipompigia kura atashinda kwa kura za watu wanaovaa mashuka wasio na elimu huko vijijini. Kilichotokea hawa watu wa Hydom wakawasimulia hao wanaoitwa hawana elimu, alipoenda kifanya kampeni wakamtimua kwamba wameishapata habari jinsi anavyowadharau, kazi anayo mwaka huu.