Mapinduzi ya Zanzibar yako hatarini.. Wazanzibari wamelala...

Unajuwa siku zote adui yako muombee njaa. Lakin vile vile dua la kuku haliwezi kumpata mwewe.

Mimi nimeishi sana Tanganyika na kubahatika kusomea huko kuanzia skuli darasa la sita Mchikichini, Tambaza Boys sec, Ilboru boys Sec na UDSM na nikapita JKT ruvu na kumalizia Mgulani. Hivyo nimeona mngi sana ya kasumba kwutoka kwa wabara dhidi ya waZnz.

Nakumbuka hata darasani walikuwa na dharau sana lakin kichwani wengi walikuwa hamna kitu. Wao na kwa jinsi ya mafunzo walopewa huko sunday school ni kuona kila Mznz ni goi goi na hawezi kuwa na akili darasani na hawezi uongozi. Kitu hicho kwa watu wa Bara ni chuki walizopandikiziwa na makovu ya UKOLONI wa mwingireza mbao ulitukuza sana dini yao na kujenga skuli nyingi za madh'hebu yao ukilinganisha na zile za waislam. sasa wamezoea kuona wao ni wasomi na wana uwezo wa kila kitu kuliko wengine.

Kumbuka kwa hilo ndilo liliweza kupelekea hata muasisi wa Chadema na waziri wa fedha mstahafu Mzee Mtei kuona kwanini kuna waislam wengi katika Tume ya kukusanya maoni ya kuundwa kwa katiba mpya. Kwani wanaamini waZnz hawawezi chochote.

Sasa ndio jua linawachwe na kuleta ghilba na fitna kama hizo.

Kwa mwenye akili timamu nafikiri atajiulize.
1. Iweje jiichi lenye watu zaidi ya milioni 12 lilazimishe kuungana na nchi yenye watu chini ya laki moja na nusu. tena kwa uwiano ulio sawa kwa kila kura?
2. Tena baya zaidi jiinchi hilo likubwa likubali kupoteza utaifa wake na jina lake na kukumbatia jina la muungano.
3. Cha aibu zaidi jiichi hilo kukubali lisiwe na serikali yake na kukumbatia ile ya muungano wakti kiichi kidogo kinakuwa na Serikali yake.

Kwa mwenye akili atagundua kuna jambo hapo limefichwa ambalo mpaka leo wenzenu wa upande wa pili hawalioni wala kuligundua si kwa sababu JKN ni saint bali ni uzuzu wa mawazo na kutegemea kutafuniwa kila kitu.

Kwani mtu mzima unaweza kumtishia nyau?


Barubaru (na wengine wote wenye mawazo kama yako kwenye RED);
Hebu niambieni, kama Watanganyika wanalazimisha muungano Wanzazibari wanalazimika kukubaliana na huko kulazimishwa muungano wasioutaka? Kama ulivyosema, kwenye muungano Zanzibar ime-retain identity yake, ina baraza lake la kutunga sheria na ina rais wake, sasa kinachowashinda kujitoa kwenye muungano ni kipi?? Au mnataka Watanganyika waseme "Muungano basi!" ndio nanyi "muamue kujitoa"? Kuna Mtanganyika aliewazuia kuitisha kura ya maoni? Mbona mliunda serikali ya muungano wa kitaifa, Mtanganyika gani aliewazuia kwa hilo?

Barubaru, ulishaingia darasa lolote la Sunday School? Kam jibu ndio, ni la dhehebu gani na wapi? Kama jibu sio, umejuaje kuwa Sunday School kunafundishwa mambo ya Uzanzibari na Utanganyika (achilia mbali mambo ya kiasiasa)?
 
Mamy punguza jazba japo inauma lakin ukweli ni ukweli japo umekujeruhi.

Umsome kwa utulivu sana na kwa uzuri sana between lines kwa NIA ya kuelewa na insh'Allah utaelewa na kama kutakuwa na mush'kira au pahala hapakukujilia vizuri basi mlango upo wazi kuuliza.

Pole sana mamy.

Hapana Barubaru,mie nimeshindwa kumuelewa pointi aliyotaka kuadress,maana kutoka kujadili mapinduzi mpaka Ukatoliki,mala Nyerereism camp,naona kama anapanga panga maneno katika mistari tu na sioni pointi.Haya turudi kwenye mada,mnataka JAMUHURI ya watu wa Zanzibar au Serikali ya MAPINDUZI Zanzibar?
 
Ndahani,

Kumbuka dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana hususan ubaguzi wa kidini ambao Tanganyika imerithi kutoka kwa wakoloni wa Kizungu wa kujiona iimani moja no bora zaidi kuliko nyengine. Imani hiyo ndio inayostahili kila kitu kuliko ingine na kujiona wao first citizen ship na wengine kuona ni second citizenship.

labda nikuulize.
Je unajuwa kwanini waTanganyika walidai uhuru wao toka kwa wazungu?
Hilo ndilo sasa litatokea kwa watu wa imani inayodhulumiwa haki zao na stahiki zao huko Tanganyika kama mtakuwa nje a muungano.

Kumbuka kuwa hakuna marafu ...


Mwanzoni sikuelewa...kumbe suala ni udini? Kila la kheri nyinyi we dini. Maana hata Somalia, Iraq, Iran, Syria na sehemu nyingine zote pia kuna dini tena dini safi. Ila watu si wasafi kabisaa. wanachofanya ni kuvaa joho la udini wakati unafiki na uchafu wao vinawaumbua. Kila kukicha kazi ni kuuana tu.
Barubaru, tell me something that will make sense...hilo la udini halina ukweli. Linasimamiwa na kufuatwa na watu wenye inferiority complex...watu wasiotaka kujifunza ili wapambane vema na challenge za maisha...watu wenye kuona karibu na wasiojua uhalisi wa mambo yanayoendesha ulimwengu wetu huu no matter we live where...Udini kama ndio tool ya kuhangaisha wengine wasio na imani yenu itawaumbua...wengi watakaochukua madaraka ya kuongoza kwa njia hiyo watakuwa watu wenye mashaka mashaka tu...time will tell
 
Last edited by a moderator:
Mbona ninyi "counter-revolutionists" mnapinga bila hoja kama ambavyo "revolutionists" wanajibu kwa hoja? Nobody has given us a reason why Zanzibar will be better-off outside the Union. Au mnataka tuanze kuwachambua kuwa sura na rangi zenu zinawasuta? Sijaona mzanzibari mweusi (mwenye zanzibar) akipiga domo kudai muungano uvunjike. Wote ninyi TV na video zinawaumbua kuwa mna asili ya waarabu.

Mtauvunja Muungano lakini mapinduzi yatalindwa kwa damu ya wabara. Harudi tena Muarabu katika pwani ya Afrika
Mashariki!

unasema nini wewe! hata huelewi unachokisema, fanya uchunguzi kwanza ndio uje na pumba zako kama hizi! "no research no right to speak" ijapokuwa rangi ya mtu sio issue kwetu, usituletee ubaguzi hapa!! sijui hata mkuu 'mzee mwanakijiji' kama atai like hii post yako s#$%^*(#!!!
 
Mwanakijiji,

Ni wajibu wa Bara kuwasaidia Zanzibar kuondoka? Hivi wao wenyewe hawana ubavu, kupitia vyombo vyao, kusema sasa basi? Ni lazima kuwe na hiyo referendum? Kwani Mapinduzi yalihitaji referendum? They could it the way they like mradi wameweza kufanya mengine madogo mpaka sasa ambyao ni prelude ya departure...ndio mtazamo wangu.
 
tanganyika ilipata uhuru 1961 ambapo nyerere alikuwa waziri mkuu na malkia alikuwa bado ndio 'mkuu'

zanzibar ilipata uhuru 1963 ampabo shamte alikuwa ni 'waziri mkuu' na sultani alikuwa bado ndio 'mkuu'

kwa nini mapinduzi yalifanyika zanzibar tu 1964 kumuondoa sultani na sio na tanganyika pia 1962 kumuondoa malkia?
 
unasema nini wewe! hata huelewi unachokisema, fanya uchunguzi kwanza ndio uje na pumba zako kama hizi! "no research no right to speak" ijapokuwa rangi ya mtu sio issue kwetu, usituletee ubaguzi hapa!! sijui hata mkuu 'mzee mwanakijiji' kama atai like hii post yako s#$%^*(#!!!

Rangi na asili ya mtu sio issue, ila uzalendo. Kwa nini watu wa rangi fulani wawe na maoni na msimamo sawa kuhusu muungano ndiyo issue hapa. Statistically, this is a risk factor that explains attitude.

Mimi siandiki post ili watu wabonyeze "like" kama wewe. Siogopi kusema ushoga ni dhambi na siutaki kwa kuwa naogopa kuambiwa ni mbaguzi wa jinsia. Likewise, siogopi kusema wenye asili ya kiarabu wana usongo na mapinduzi kwa hiyo wanauchukia muungano ili nisionekane ni mbaguzi wa rangi.

Siombi radhi kwa hili.
 
Nimesoma taarifa hii kwa mapana Gazetini nimefarijika na kunufaika sana nayo kimoja cha msingi hapa ni Tahadhari kwa viongozi na wananchi wote hasa Zanzibar ambao kila siku wanaota kujitoa kwenye muungano nadhani ni hoja ya watu wa mrengo wa kushoto na wazanzibari wenyewe wote tuwe makini naamini tanzania ni moja bila zanziba hakuna Tanzania bila tanganyika hakuna zanzibar tafakarini na mchukue hatua badala ya malumbano yasio na msingi...
 
Nimesoma taarifa hii kwa mapana Gazetini nimefarijika na kunufaika sana nayo kimoja cha msingi hapa ni Tahadhari kwa viongozi na wananchi wote hasa Zanzibar ambao kila siku wanaota kujitoa kwenye muungano nadhani ni hoja ya watu wa mrengo wa kushoto na wazanzibari wenyewe wote tuwe makini naamini tanzania ni moja bila zanziba hakuna Tanzania bila tanganyika hakuna zanzibar tafakarini na mchukue hatua badala ya malumbano yasio na msingi...
 
Barubaru (na wengine wote wenye mawazo kama yako kwenye RED);
Hebu niambieni, kama Watanganyika wanalazimisha muungano Wanzazibari wanalazimika kukubaliana na huko kulazimishwa muungano wasioutaka? Kama ulivyosema, kwenye muungano Zanzibar ime-retain identity yake, ina baraza lake la kutunga sheria na ina rais wake, sasa kinachowashinda kujitoa kwenye muungano ni kipi?? Au mnataka Watanganyika waseme "Muungano basi!" ndio nanyi "muamue kujitoa"? Kuna Mtanganyika aliewazuia kuitisha kura ya maoni? Mbona mliunda serikali ya muungano wa kitaifa, Mtanganyika gani aliewazuia kwa hilo?

Barubaru, ulishaingia darasa lolote la Sunday School? Kam jibu ndio, ni la dhehebu gani na wapi? Kama jibu sio, umejuaje kuwa Sunday School kunafundishwa mambo ya Uzanzibari na Utanganyika (achilia mbali mambo ya kiasiasa)?

tatizo hapa mnazungumza yatokanayo na mapinduzi lakini siri kubwa hamuijui,na kama mnaijua basi mwajitia ujuha hebu niambieni uchaguzi huru wa haki na wa vyama vingi zanzibar ulifanyika kabla ya muungano au baada ya muungano wa 1964
 


Nakumbuka hata darasani walikuwa na dharau sana lakin kichwani wengi walikuwa hamna kitu. Wao na kwa jinsi ya mafunzo walopewa huko sunday school ni kuona kila Mznz ni goi goi na hawezi kuwa na akili darasani na hawezi uongozi. Kitu hicho kwa watu wa Bara ni chuki walizopandikiziwa na makovu ya UKOLONI wa mwingireza mbao ulitukuza sana dini yao na kujenga skuli nyingi za madh'hebu yao ukilinganisha na zile za waislam. sasa wamezoea kuona wao ni wasomi na wana uwezo wa kila kitu kuliko wengine
Kwa mwenye akili timamu nafikiri atajiulize.
1. Iweje jiichi lenye watu zaidi ya milioni 12 lilazimishe kuungana na nchi yenye watu chini ya laki moja na nusu. tena kwa uwiano ulio sawa kwa kila kura?
2. Tena baya zaidi jiinchi hilo likubwa likubali kupoteza utaifa wake na jina lake na kukumbatia jina la muungano.
3. Cha aibu zaidi jiichi hilo kukubali lisiwe na serikali yake na kukumbatia ile ya muungano wakti kiichi kidogo kinakuwa na Serikali yake.

Kwa mwenye akili atagundua kuna jambo hapo limefichwa ambalo mpaka leo wenzenu wa upande wa pili hawalioni wala kuligundua si kwa sababu JKN ni saint bali ni uzuzu wa mawazo na kutegemea kutafuniwa kila kitu.
Kwani mtu mzima unaweza kumtishia nyau?
Ahlan, Baru baru unapojenga hoja ukajawa na jwazba basi unapoteza mwelekeo. Umesoma Tanaganyika na watu wa dini na makabila mbali mbali, sasa ukisema wanaokudharau ni sunday school tayari umeonyesha kuwa shida si muungano bali ni sunday school. Hii ndiyo hoja ya UAMSHO na inasikitisha kuona mtu wa kiwango chako umeingia katika huo mtego. Inasikitisha.

Lakini pia lazima utambue adui wa mzanzibar si mkristo ni Mtanganyika. Wanapochoma makanisa wanawaadhibu wakristo, na wakitaka kuwaadhibu waislam wanawaita machogo kwa vile hawawezi kuchoma misikiti.
Adui ni mtanganyika ndiyo maana neno kafir wa bara hutumika

Kwa kuelewa uzuzu wetu na liinchi letu likubwa kama ulivyosema, sasa tunasema basi, muungano ufe ili mpate nchi yenu yenye neema na hapa kauli mbiu ni LET ZNZ GO!

Nadhani mada haipo katika udini zaidi na tusijaribu kui 'adulterate'. Tujikite katika mada ya kulinda mapinduzi na kama lipo liwalo basi lianzishiwe nyuzi yake. Hii itatusaidia tubaki 'composed' and not just shoot any moving object
 
Barubaru (na wengine wote wenye mawazo kama yako kwenye RED);
Hebu niambieni, kama Watanganyika wanalazimisha muungano Wanzazibari wanalazimika kukubaliana na huko kulazimishwa muungano wasioutaka? Kama ulivyosema, kwenye muungano Zanzibar ime-retain identity yake, ina baraza lake la kutunga sheria na ina rais wake, sasa kinachowashinda kujitoa kwenye muungano ni kipi?? Au mnataka Watanganyika waseme "Muungano basi!" ndio nanyi "muamue kujitoa"? Kuna Mtanganyika aliewazuia kuitisha kura ya maoni? Mbona mliunda serikali ya muungano wa kitaifa, Mtanganyika gani aliewazuia kwa hilo?

Barubaru, ulishaingia darasa lolote la Sunday School? Kam jibu ndio, ni la dhehebu gani na wapi? Kama jibu sio, umejuaje kuwa Sunday School kunafundishwa mambo ya Uzanzibari na Utanganyika (achilia mbali mambo ya kiasiasa)?

nasikia wanataka kwanza kutoa Majeshi wote na polisi wenye asili ya Tanganyika halafu wajenge upya jeshi lao la Zanzibar Military force kuweka vizuri ulinzi wa nchi yao pamoja na mipaka yao iwe kwenye Control yao baadae ndio watakuwa tayari kutangaza kama Muungano basi Zanzibar iko kivyake kuanzia hapo...wanaenda step by step nasikia wamekataa kuanzishwa kwa ligi ya Muungano wa TZ:focus:
 
nasikia wanataka kwanza kutoa Majeshi wote na polisi wenye asili ya Tanganyika halafu wajenge upya jeshi lao la Zanzibar Military force kuweka vizuri ulinzi wa nchi yao pamoja na mipaka yao iwe kwenye Control yao baadae ndio watakuwa tayari kutangaza kama Muungano basi Zanzibar iko kivyake kuanzia hapo...wanaenda step by step nasikia wamekataa kuanzishwa kwa ligi ya Muungano wa TZ:focus:


Historia inatabia ya kujirudia rudia
 
Ahlan, Baru baru unapojenga hoja ukajawa na jwazba basi unapoteza mwelekeo. Umesoma Tanaganyika na watu wa dini na makabila mbali mbali, sasa ukisema wanaokudharau ni sunday school tayari umeonyesha kuwa shida si muungano bali ni sunday school. Hii ndiyo hoja ya UAMSHO na inasikitisha kuona mtu wa kiwango chako umeingia katika huo mtego. Inasikitisha.

Lakini pia lazima utambue adui wa mzanzibar si mkristo ni Mtanganyika. Wanapochoma makanisa wanawaadhibu wakristo, na wakitaka kuwaadhibu waislam wanawaita machogo kwa vile hawawezi kuchoma misikiti.
Adui ni mtanganyika ndiyo maana neno kafir wa bara hutumika

Kwa kuelewa uzuzu wetu na liinchi letu likubwa kama ulivyosema, sasa tunasema basi, muungano ufe ili mpate nchi yenu yenye neema na hapa kauli mbiu ni LET ZNZ GO!

Nadhani mada haipo katika udini zaidi na tusijaribu kui 'adulterate'. Tujikite katika mada ya kulinda mapinduzi na kama lipo liwalo basi lianzishiwe nyuzi yake. Hii itatusaidia tubaki 'composed' and not just shoot any moving object


Ahlan wa sahalan Nguruvi3,

Nafikiri watu mnaanza kupotosha maana nzima ya hoja zangu kama mnavyoweza kubatilisha na kuweka propaganda kuhusu jumuiya ya UAMSHO na kujaribu kujenga hoja kuwa ni kama ya kigaidi kitu ambacho ni uongo na uzandiki mkubwa.

Siku zote ukiwa Tanganyika mnajaribu sana kuficha makucha yenu na kujiona kuwa ni superior sana kuliko Znz na waZnz. Kitu hicho nimebainisha wazi kuwa mnajiona ni wasomi zaidi, mnajua kila kitu sana na mna uwezo mkubwa sana wa akila kitu kuliko Znz. Kwa mantiki hiyo mnalazimisha na kujenga hoja kuwa Znz haiwezi kabisa kujitawala yenyewe bila Tanganyika. Kitu ambacho ni kujidanganya na kuleta fitna kwa waZnz na Znz kijumla.

Mimi point zangu nafikiri nimezijenga kwa kuangalia Tanganyika nje ya Muungano wenu. Nimebainisha bila kuficha KOVU mliloachiwa na utawala wa mkoloni la UDINI kwa Tanganyika (kitu ambacho japo mnakijua lakin hamtaki kabisa kukikubali) kama ilivyo ukabila kwa kenya na Uganda. Tahadhari yangu kwa Tanganyika ni kuwa kwa kuwa waiskam nao sasa wameshasoma (sio kama mlivyokuwa mnawadharau hapo kale) pasi na shaka yoyote mtaingia kwa mgogoro mkubwa nao. Kwani nao watakuwa na mtazamo kama wa Mzee wangu Mtei pale alipoitazama tume ya kukusanya maoni kuhusu katiba mpa na kusema ameona WAISLAM NI WENGI.

Lakin pia kama uliisikiliza vizuri ile hotna a nyerere aliposema Dhambi ya Ubaguzi. Mwisho alisema yeye aliwabembeleza Kuunda EAC kwa sababu alitaka kuwasaidia nchi za kenya na Uganda kuunguza Ukabila. Kwani aliamini ndani ya EAC watu wote watazungumzia kuhusu maslah ya nchi zao na sio makabila yao. Hii ina maana aligundua kuwa Ukabila ilikuwa ni athari za ukoloni kwa nchi hizo za Kenya na Uganda. Je Tanganyika walipata Athari gani kutokana na ukoloni huo ukizingatia kuwa Mkoloni hiyo alitumia divide and rule?

Suala hilo nafikiri wengi wenu mnakataa kulijibu lakin ukiendelea na kuona Nchi kubwa inaungana na nchi ndogo kwa 50/50 % nalo pia utaona Nyerere alificha nini ndanimwe.

Kumbuka kuwa siku zote historia haifichiki na inajirudia kila wakti. UDINI kama athali za ukoloni huko Bara nafikiri sasa linaonekana dhahiri wa shahri. Binafsi sikuliona nilipokuwa skuli wala JKT bali kazini nililiona sana na kila tulipouliza tuliambiwa kuwa waislam bwaa wanendekeza Madrasa na hawataki skuli. Kwa mwenye akili timamu unajiuliza hivi bara na Znz wapi kuna madrasa nyingi na kila famili lazima ipeleke watoto madrasa. Utaona Znz. Nikija kwa waitimu wa UDSM kwa 5 wale kutoka Bara na Znz utaona Znz wapo mbali sana. Sasa vipi waislam wa Bara.

Hizi ni kasumba na kuziongopea jamii. Kumbuka vile vile siku zote anayedhulumiwa ndie anaeona machungu. hata ukipitia uhuru wenu wale waasisi wa Uhuru wenu wengi ni waislam, Je nalo hujui kwanini? kama utakuwa muwazi na mkweli na unaipenda sana jamii yako huwezi kujipendekeza kwa kupindisha ukweli kwani siku zote ukweli unasimama na uongo unajitenga.

Mimi pamoja na historia inatabiri. Nje ya muungano Znz itakwenda vizuri sana kwani kosa lao wamelitambua na wamelipatia dawa mujarab. Tanganyika lazima mtayumba sana kwa sababu ile ile ya kuficha ukweli na kukataa kuelezwa ukweli kama mnavyojidanganya kwa kusema Tanganyika ni Salama. Je kuna usalama kweli?

Nawashauri kama Tanganyika hamtaliangalia hilo kovu na urithi wenu wa mkoloni kama janga. Basi lazima siku moja litawamaliza. kwani mficha magonjwa ...


 
Mwanzoni sikuelewa...kumbe suala ni udini? Kila la kheri nyinyi we dini. Maana hata Somalia, Iraq, Iran, Syria na sehemu nyingine zote pia kuna dini tena dini safi. Ila watu si wasafi kabisaa. wanachofanya ni kuvaa joho la udini wakati unafiki na uchafu wao vinawaumbua. Kila kukicha kazi ni kuuana tu.
Barubaru
, tell me something that will make sense...hilo la udini halina ukweli. Linasimamiwa na kufuatwa na watu wenye inferiority complex...watu wasiotaka kujifunza ili wapambane vema na challenge za maisha...watu wenye kuona karibu na wasiojua uhalisi wa mambo yanayoendesha ulimwengu wetu huu no matter we live where...Udini kama ndio tool ya kuhangaisha wengine wasio na imani yenu itawaumbua...wengi watakaochukua madaraka ya kuongoza kwa njia hiyo watakuwa watu wenye mashaka mashaka tu...time will tell

Ndahani,

Kila wakti nabainisha HAKUNA KITU BORA DUNIYANI KULIKO SKULI, na raha ya kusoma ni kuelimika kwa maana kabla ujamua au kutenda chochote kwa unafikiri na kukifanyia udadisi kabla kutenda.

Nitakusaidia vizuri kuhusu nchi ulizo zitaja. Nchi hizo zote hakuna tatizo la DINI bali kuna matatizo ya kikabila na koo. Kama ilivyokuwa Mauaji ya kimabri kule Rwanda na hata machafuko ya Kenya baada ya uchaguzi wao uliopita. Ukitaka kujua machafuko ya dini yapo wapi fuatilia kadhia la Nigeria au Lebnon.

Lakin ningependa kumaliza kwa kukupa suala kidogo.
1. Nafikiri unakubali kabisa Kenya na Uganda kuna Ukabila? Na ukabila huo ni zao la urithi wa Mkoloni? Je Tanzania urithi wake kwa mkoloni au mkoloni alitumia njia gani kuwagawa waTanganyika ili awatawale?

2. Je unajuwa kwanini waanzilishi na waasisi wa uhuru w Tz wengi walikuwa wazee wa Pwani na wengi walikuwa waislam?

Kila la kheir na l'jumaa njema
 
Ndahani,

Kila wakti nabainisha HAKUNA KITU BORA DUNIYANI KULIKO SKULI, na raha ya kusoma ni kuelimika kwa maana kabla ujamua au kutenda chochote kwa unafikiri na kukifanyia udadisi kabla kutenda.

Nitakusaidia vizuri kuhusu nchi ulizo zitaja. Nchi hizo zote hakuna tatizo la DINI bali kuna matatizo ya kikabila na koo. Kama ilivyokuwa Mauaji ya kimabri kule Rwanda na hata machafuko ya Kenya baada ya uchaguzi wao uliopita. Ukitaka kujua machafuko ya dini yapo wapi fuatilia kadhia la Nigeria au Lebnon.

Lakin ningependa kumaliza kwa kukupa suala kidogo.
1. Nafikiri unakubali kabisa Kenya na Uganda kuna Ukabila? Na ukabila huo ni zao la urithi wa Mkoloni? Je Tanzania urithi wake kwa mkoloni au mkoloni alitumia njia gani kuwagawa waTanganyika ili awatawale?

2. Je unajuwa kwanini waanzilishi na waasisi wa uhuru w Tz wengi walikuwa wazee wa Pwani na wengi walikuwa waislam?

Kila la kheir na l'jumaa njema

Barubaru, pongezi kwa kukiri umuhimu wa shule kwenye maisha ya binadamu. Kama shule inatukomboa, kwanini isitukomboe kwenye urithi wa vitu vibaya vya wakoloni? Kwa bahati mbaya waafrika wengi tumesoma ila hatukuelimika...we did not develop educated mind. As a result we want to be recognized as learned people while our deeds go contractry to what education minds entails.
Matatizo ya nchi zote ulizozisema sio ya wakoloni...ni ya kwao wenyewe maana kwanini mtu unakubali kukumbatia kitu kinachokuletea madhara?
Mimi na wewe tuna dini na si lazima iwe dini moja....sikubaliani kabisa na hoja za udini mnazotaka kuzileta hapa. Hata leo hii muungano ukivunjika, kama dini ndiyo kigezo mnachotaka kitumike kutawala Zenj, mtafanya makosa makubwa....you will create a divided Zenj maana zipo hoja pia za watu kutofautiana kwa upemba na uunguja.
 
Barubaru, pongezi kwa kukiri umuhimu wa shule kwenye maisha ya binadamu. Kama shule inatukomboa, kwanini isitukomboe kwenye urithi wa vitu vibaya vya wakoloni? Kwa bahati mbaya waafrika wengi tumesoma ila hatukuelimika...we did not develop educated mind. As a result we want to be recognized as learned people while our deeds go contractry to what education minds entails.
Matatizo ya nchi zote ulizozisema sio ya wakoloni...ni ya kwao wenyewe maana kwanini mtu unakubali kukumbatia kitu kinachokuletea madhara?
Mimi na wewe tuna dini na si lazima iwe dini moja....sikubaliani kabisa na hoja za udini mnazotaka kuzileta hapa. Hata leo hii muungano ukivunjika, kama dini ndiyo kigezo mnachotaka kitumike kutawala Zenj, mtafanya makosa makubwa....you will create a divided Zenj maana zipo hoja pia za watu kutofautiana kwa upemba na uunguja.

Ndahani.

Ahali yangu nimezungumzia skuli sana kwa maana mtu anatakiwa kuwa mdadisi wa mambo na nimekupa masuala mawili naona hukuyaona. nakukumbusha hebu jibu hayo masuala.

Lakin pia nimekubainishi kuwa HUWEZI FICHA HISTORIA na siku zote HISTORIA HUWA INAJIRUDIA. Urithi wa madhara ya Ukoloni kutokana na mfumo wao wa gawanya utawale ilikuwa Ukabila kwa Kenya na Uganda. Na hilo sio siri huko Kenya na Uganda. Znz kuna yao ambayo kwa sasa SMZ imaliona na kulitatua kwa kuunda SUK.

Je Tanganyika kunani?

Kumbuka kuwa najenga hoja zangu kwa kutumia historia na wewe kama unataka nihukumu basi ujue unaihukumu Historia yenu.

Nasubiri majibu ya masuala yangu kwako.

 
Ndahani.

Ahali yangu nimezungumzia skuli sana kwa maana mtu anatakiwa kuwa mdadisi wa mambo na nimekupa masuala mawili naona hukuyaona. nakukumbusha hebu jibu hayo masuala.

Lakin pia nimekubainishi kuwa HUWEZI FICHA HISTORIA na siku zote HISTORIA HUWA INAJIRUDIA. Urithi wa madhara ya Ukoloni kutokana na mfumo wao wa gawanya utawale ilikuwa Ukabila. Na hilo sio siri huko Kenya na Uganda. Znz kuna yao ambayo kwa sasa SMZ imaliona na kulitatua kwa kuunda SUK.

Je Tanganyika kunani?

Kumbuka kuwa najenga hoja zangu kwa kutumia historia na wewe kama unataka nihukumu basi ujue unaihukumu Historia yenu.

Nasubiri majibu ya masuala yangu kwako.


Tanganyika iliisha rasmi 1964...labda kama imeanzishwa tena bila kujua.Sioni lolote linalotokea huku zaidi ya hizi kele zinazopigwa bila kuwa supported na facts.
Halafu kitu nisichoweza kufanya kwa haraka katika maisha yangu ya kawaida ni kukimbilia kutoa jibu kwenye suala ambalo najua sina facts...ntaanzia wapi mkuu? Ninaposema si lazima tuamini urithi wa wakoloni namaanisha. Sitanii maana si kila kitu kililenga kutusaidia sisi.
Pia ni kweli kabisa Historia ipo lakini si lazima ijirudie. Huwa tunapenda kusema "ni lazima ijurudie" maana mambo yote tunayofanya yanalenga kuwezeshwa kwa historia kujirudia.
Muhimu zaidi ya yote ni wapi tunawekeza nguvu na fikra zetu maana "pale ulipo moyo wako ndipo pia hazina yako ilipo". Ukiwekeza kwenye mambo negative utegemee kuvuna vitu negative....ukipoteza muda wako kwa mambo yasiyo na tija ndivyo pia maisha yako yatakavyokuwa hayana tija...they call the law of harvest because in our lives, we reap what we sow.
 
Tanganyika iliisha rasmi 1964...labda kama imeanzishwa tena bila kujua.Sioni lolote linalotokea huku zaidi ya hizi kele zinazopigwa bila kuwa supported na facts.
Halafu kitu nisichoweza kufanya kwa haraka katika maisha yangu ya kawaida ni kukimbilia kutoa jibu kwenye suala ambalo najua sina facts...ntaanzia wapi mkuu? Ninaposema si lazima tuamini urithi wa wakoloni namaanisha. Sitanii maana si kila kitu kililenga kutusaidia sisi.
Pia ni kweli kabisa Historia ipo lakini si lazima ijirudie. Huwa tunapenda kusema "ni lazima ijurudie" maana mambo yote tunayofanya yanalenga kuwezeshwa kwa historia kujirudia.
Muhimu zaidi ya yote ni wapi tunawekeza nguvu na fikra zetu maana "pale ulipo moyo wako ndipo pia hazina yako ilipo". Ukiwekeza kwenye mambo negative utegemee kuvuna vitu negative....ukipoteza muda wako kwa mambo yasiyo na tija ndivyo pia maisha yako yatakavyokuwa hayana tija...they call the law of harvest because in our lives, we reap what we sow.


Nilipo BLUE.

Nimeipenda sana kauli hii.

Je ukiwekeza kwene uwongo na propaganda za kizandiki utapata nini?
L
akin nitakusaidia zaidi kukwambia HISTORIA sio nadharia bali ni matukio yaliyojitokeza huko nyuma na ni lazima kuyarejea kwani ndanimwe kuna misingi ya UHURU wenu. Ndio maana tunaiheshimu na kuithamini sana historia kwa kuyaona yote mazuri na mabaya yake na kuyatendea yote haki zake kuhakikisha kile kibaya kinapotea na mema yanaimarika kwa kutumia kaanun ya uwazi na ukweli.

nafikiri umeiona kathia ya Znz ambako bila waZnz kuziona tofauti zao na kutafuta suluhu mpaka leo yangekuwepo na yangezidi kudumaza maendeleo ya jamii. Hiyo ndio historia na huo ndio umuhimu wake.

Waswahili wanasema. Mdharau mwiba ...
 
Back
Top Bottom