Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,810
- 59,359
Hivi kuna mtu yeyote anaeweza kujitosa hapa akasema na kuthibitisha kwamba kwenye UKOO wake wote hamna wezi..wadada wanaojiuza... wadada warahisi kupatikana...watu wakorofi...wavivu...wambea...wasiojua mapenzi..wanaojali/kupenda pesa (as if hao wapondaji wenyewe hawapendi) ...wahuni ...matapeli...wenye viburi...wenye dharau... wenye sura na mumbo unayoona wewe ni mabaya...wabahili...wachoyo...wanaopenda/oa/olewa kwa pesa n.k achilia mbali kwenye KABILA lake?!Kama wapo ningependa kuwajua ili na sie tusioisha kusemwa kila siku tujifunze toka kwao.
Ukweli na kwamba tabia ya mtu haitakiwi kuwa defined na wapi alipotoka (hata familia yake) bali na vile alivyo.Stereotypes hua zipo kwaajili ya wale waliotofauti na wanaokua stereotyped...kuwasaidia wale wa nje kuwalebel wenzao vibaya ili wao wajione/hisi kwamba ni bora hata kama sio kweli.Ndio maana hata wazungu (sio wote) bado wanatuona Waafrika kama wanyama..wanaamini hatuna akili japo wapo waaAfrika wenye akili kuliko wazungu wengi tu.Ila hili wazo linawafanya wao wajione wako juu.Kama ambavyo sisi wenyewe tunafanyiana kwanzia nchi na nchi..mkoa na mkoa...kabila na kabila..ukoo na ukoo na hata familia hii na ile.Kwenye swala zima la mapenzi naamini kabisa kwamba kabila haiplay role yoyote...kwahiyo achaneni na habari za sijui kabila hili hivi na lile lile.Kama unamjua mtu personally unaweza kumjudge yeye kwa vile unavyomjua na sio zaidi ya hapo.Pili....kama wewe hukupata experience nzuri na mtu wa sehemu fulani haina maana itakua hivyo hivyo kwa wengine wote.Ndio maana hata mwanamke /mwanaume unayemuona wewe kwamba hafai bado anakutana na mtu mwingine na anapendwa utadhani yeye ndio kila kitu.Kwahiyo waache wenzio nao wapate experience zao....kama wewe hukufanikiwa mwache mwingine nae ajaribu bahati yake.
Nasema yote haya maana hili swala la kuchambua makabila ya watu humu limezidi na linaboa kwakweli.Sijali kama ni langu au la mtu mwingine....ishu ni kwamba inachosha!!Mbaya zaidi ni kwamba yote mnayosema yanaweza kufanywa na yeyote hata anaetoka nchi nyingine achilia mbali wa kabila tofauti!
Alafu hivi hamchoki maana pamoja na sifa zote za ajabu ajabu mnazoyarushia haya makabila bado wadada wake wanaolewa SANA na wakaka wake wanaoa SANA ndani na nje ya makabila yao.Bado tu hamjagundua kwamba haisaiidii muachane nayo?!Maana kama ingekua inasaidia for the past few years usingesikia watu wa haya makabila wameoa wala kuolewa!
Mwisho...kama umempenda mtu na tabia yake inaendana na wewe upendavyo endelea nae...kama makabila ni muhimu sana tafuta wakwenu ili tabia zenu zifanane badala ya kuanza kuchambua ya wengine visivyo.Mapenzi kila mtu anaweza akayajua na kila mtu anaweza asiyajue...yote inategemea wawili wapendanao wanavyoyachukulia.
Ukweli na kwamba tabia ya mtu haitakiwi kuwa defined na wapi alipotoka (hata familia yake) bali na vile alivyo.Stereotypes hua zipo kwaajili ya wale waliotofauti na wanaokua stereotyped...kuwasaidia wale wa nje kuwalebel wenzao vibaya ili wao wajione/hisi kwamba ni bora hata kama sio kweli.Ndio maana hata wazungu (sio wote) bado wanatuona Waafrika kama wanyama..wanaamini hatuna akili japo wapo waaAfrika wenye akili kuliko wazungu wengi tu.Ila hili wazo linawafanya wao wajione wako juu.Kama ambavyo sisi wenyewe tunafanyiana kwanzia nchi na nchi..mkoa na mkoa...kabila na kabila..ukoo na ukoo na hata familia hii na ile.Kwenye swala zima la mapenzi naamini kabisa kwamba kabila haiplay role yoyote...kwahiyo achaneni na habari za sijui kabila hili hivi na lile lile.Kama unamjua mtu personally unaweza kumjudge yeye kwa vile unavyomjua na sio zaidi ya hapo.Pili....kama wewe hukupata experience nzuri na mtu wa sehemu fulani haina maana itakua hivyo hivyo kwa wengine wote.Ndio maana hata mwanamke /mwanaume unayemuona wewe kwamba hafai bado anakutana na mtu mwingine na anapendwa utadhani yeye ndio kila kitu.Kwahiyo waache wenzio nao wapate experience zao....kama wewe hukufanikiwa mwache mwingine nae ajaribu bahati yake.
Nasema yote haya maana hili swala la kuchambua makabila ya watu humu limezidi na linaboa kwakweli.Sijali kama ni langu au la mtu mwingine....ishu ni kwamba inachosha!!Mbaya zaidi ni kwamba yote mnayosema yanaweza kufanywa na yeyote hata anaetoka nchi nyingine achilia mbali wa kabila tofauti!
Alafu hivi hamchoki maana pamoja na sifa zote za ajabu ajabu mnazoyarushia haya makabila bado wadada wake wanaolewa SANA na wakaka wake wanaoa SANA ndani na nje ya makabila yao.Bado tu hamjagundua kwamba haisaiidii muachane nayo?!Maana kama ingekua inasaidia for the past few years usingesikia watu wa haya makabila wameoa wala kuolewa!
Mwisho...kama umempenda mtu na tabia yake inaendana na wewe upendavyo endelea nae...kama makabila ni muhimu sana tafuta wakwenu ili tabia zenu zifanane badala ya kuanza kuchambua ya wengine visivyo.Mapenzi kila mtu anaweza akayajua na kila mtu anaweza asiyajue...yote inategemea wawili wapendanao wanavyoyachukulia.